picha

DALILI ZA UGONJWA WA MALARIA, (homa,uchovu, kutapika, kichefuchefu, maumivu ya kichwa n.k)

DALILI ZA UGONJWA WA MALARIA, (homa,uchovu, kutapika, kichefuchefu, maumivu ya kichwa n.k)

DALILI ZA MALARIA

 

Dalili za malaria huenda pia zikafungamana na maradhi mengine, lakini endapo zikikusanyika pamoja kwa asilimia kubwa vitakuwa vinaonyesha uwepo wa malaria. Kumbuka hizi ni dalili tu, lakini ni vyema kupima ili kuwa na uhakika zaidi kabla ya kumeza dawwa.

 

Homa, homa ni kupanda kwa joto mwilini. Kikawaida homa ni dalili za maradhi mengi sanaila leo nitakueleza homa ya malaria ilivyo. Kikawaida hima ya malaria inaweza kuambatana na mambo kadhaa wa kadhaa. Mambo hayo ni kama


Kuhisi baridi, kutetemeka na kutaka kuotea jua ama moto. Haijalishi ni saa ngapi iwe mchana ama usiku lakini mgonjwa atahisi baridi kali sana. Na inaweza kumsababishia hali ya kutetemeka viungo ama taya za mdomo wake kugongana kwa baridi. Hivyo endapo homa itaungana na hali hii huenda ni malaria. Lakini haitishi, inaweza pia kuambatana na japo hili hap chini:-

 

Maumivu ya kichwa, uchovu na maumivu ya misuli pamoja na viungio. Endapo homa ya mgojwa itaambatana na baridi, kisha ikafuatiwa na maumivu ya kichwa, maumivu haya yanaambatana na misuli kuuma pamoja na viungio. Mgonjwa anahisi katikati ya akutano ya viungio kama kuna vuta. Halli hizi zikikusanyika kwa pamoja huashiria malaria.

 

Mvurugiko wa tumbo unaopelekea kichefuchefu, ama kuharisha, ama kutapika ama vyote kwa pamoja. Mgonjwa anaweza kupata hali moja kati ya hizi ama akawa nazo zote. Mgonjwa anaweza kutapika maji ama chakula alichokula ama anaweza kutapika ile tunayoita nyongo. Hali hizi zinaweza kumpelekea mgonjwa akachoka sana. Tofauti na kuchoka huku lakini hatakuwa na hamu ya kula, na hata ladha ya chakula inabadilika na kuwa kichungu.

 

Uchovu, kukosa hamu ya kula, maumivu ya viungo, kuchanganyikiwa, maumivu ya kichwa, kutapika ama kuharishah. Hizi ni katika dalili za malaria.

 



                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 6639

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 web hosting     πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰6 ai web app    

Post zinazofanana:

Dalili zinazonesha kuungua kwa Mdomo (burning mouth)

Ugonjwa wa mdomo unaoungua ni neno la kimatibabu kwa ajili ya kuungua kinywani kwa mara kwa mara (kwa muda mrefu) bila sababu dhahiri. Usumbufu huo unaweza kuathiri ulimi wako, ufizi, midomo, ndani ya mashavu yako, paa la mdomo wako au maeneo yaliyoenea

Soma Zaidi...
Pumu (Asthma): Dalili za mwanzo na jinsi ya kuepuka mashambulizi.

Pumu (Asthma) ni ugonjwa sugu wa njia ya hewa unaoathiri mamilioni ya watu duniani. Makala haya yanalenga kutoa ufahamu wa kina kuhusu dalili za mwanzo ambazo mara nyingi hupuuzwa, mazingira yanayochochea mashambulizi, na mikakati madhubuti ya kudhibiti ugonjwa huu. Kwa kufuata mwongozo huu, wagonjwa wanaweza kupunguza hatari ya mashambulizi ya ghafla na kuboresha ubora wa maisha yao.

Soma Zaidi...
je kukohoa kunaweza kuwa ni dalili ya minyoo?

Dalili za minyoo zipo nyingi kama kuumwa na tumbo, tumbo kujaa gesi, uchovu, kukosa hamu ya kula, kupata choo chenye uteute na kupunguwa uzito. je kukohoa kunaweza kuwa ni dalili ya minyoo?

Soma Zaidi...
Visababishi vya ugonjwa wa Varicose vein

Posti hii inahusu zaidi visababishi mbalimbali vya ugonjwa wa vericose veini, ni visababishi mbalimbali ambavyo utokea kwenye mtindo wa maisha kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya tumbo kwa chini uapande wa kushoto

Zijuwe sababu kuu zinazokufanya ukahisi maumivu makali ya tumbo kwa chini upande wa kushoto

Soma Zaidi...