Navigation Menu



SABABU ZINAZOPELEKEA KUJAA KWA MATE MDOMONI NA MATIBABU YAKE

Kutokwa na mate mengi mdomoni si ugojwa ni hali inayoweza kutokea kwa mtu yeyote. Mara nyingi hali hii haihitaji matibabu wa dawa, na huondoka yenyewe. Lakini hutokea baadhi ya nyakati ikawa mate yanatoka zaidi mdomoni. Je na wewe ni miongoni mwao? Makala

Hapa tutaangalia baadhi ya sababu zinazopelekea mdomo kujaa mate. Sababu hizi zipo nyingine ni kwa wanawake tu, pia zipo ambazo ni kwa watu wa jinsia zote. Tunatarajia baada ya kusoma makala hii utaweza kuzijuwa sababu zinazopelekea mdomo kujaa mate, pia utaweza kupata kujuwa nini unatakiwa ufanye kulingana na tatizo lako.


HUJAA KWA MATE MDOMONI NI NINI HASA?
Kitaalamu kitendo hiki cha kujaa kwa mate mdomoni hufahamika kama hypersalivation. Hiki ni kitendo cha mdomo kujaa mate na wakati mwengine hutokea mate yakatoka yenyewe kwenye midomo baada ya kujaa. Kitaalamu kitendo hiki sio ugonjwa ila ni dalili ya kuwepo kwa tatizo lakiafya ama kuwepo kwa jambo lililopelekea mabadiliko ya mwili na kiafya.


JE MATE NI NINI?
Mate ni kimiminika cheupe kinachopatikana mdomoni ambacho hutengenezwa kwenye tezi za mate zinazojulikana kama salivary glands. Mate yana vichochezi (enzymes) ambavyo hutumika katika mmeng'enyo wa chakula hasa chakula cha wanga mdomoni. Mate pia husaidia katika kulainisha chakula na kuweka mgomo katika hali ya usafi, usalama na ubichibichi.
Tafiti zinaeleza kuwa mtu wa kawaida anaweza kuzalisha mate yanayofikia lita moja na nusu kwa siku. mate huzalishwa kwa wingi mtu anapokula na uzalishaji huu hupunguwa pale anapolala.


MADHARA YA KUWA NA MATE KIDOGO
Kwa kuwa mate yana faida kubwa mwilini hivyo endapo uzalishaji wa mate hautakuwa wa kutosheleza madhara huweza kumpata mtu ni kama:-
1.mdomo kuwa mkavu
2.Mmeng’enyo wa chakula kutofanyika vyema mdomoni kwa vyakula vya wanga
3.Mtu anaweza kupata taabu wakati wa kumeza
4.Anaweza kupata vidonda vya mdomo
5.Mdomo utaweza kuathiriwa kwa urahisi na fangasi, bakteria na sumu na kemikali za kwenye vyakula
6.Hata kuzungumza kunaweza kuathiriwa endapo mtu atakosa mate ya kutosha


MADHARA GANI ATAYAPATA MTU KAMA ATAKUWA NA MATE MENGI ZAIDI?
Kama ilivyokuwa kuna hasara kwa mate kukosekana mwilini, halikadhalika endapo mate yatakuwa mengi zaidi pia hali hii itakuwa na madhara yake. Madhara hayo ni kama:-
1.Matatizo wakati wa kusema, yaani hatoweza kuema vyema kama mate yatakuwa yamejaa mdomoni
2.Itakuwa vigumu kuufunga mdomo
3.Pia mdomo utaweza kupata mashambulizi ya bakteria kwa urahisi.
4.Mtu atashindwa kujiamini na kukaa na watu kwa sababu ya mate yake.


NINI HUSABABISHA MDOMO KUJAA MATE?
Hizi ni katika sababu ambazo hupelekea mate kujaa mdomoni:-
1.Kuongezeka kwa uzalishwaji wa mate mdomoni
2.Kama mtu atakuwa na shida na kushindwa kumeza mate ama mdomo kuondoa mate yote wakati wa kutema
3.Kama mtu atakuwa na matatizo ya kutoweza kuufunga mdomo


NINI HUSABABISHA ONGEZEKO LA UZALISHAJI WA MATE MDOMONI
Kama ulivyoona hapo juu sababu za kuwa na mate mengi mdomoni ni ongezeko la uzalishwaji wa mate mdomoni. Sasa swali la msingi kuwa “ni nini husababisha hili ongezeko la uzalishwaji wa mate mdomoni” . Sababu gizo ni kama:-
1.Kichefuchefu
2.Homa ya asubuhi na ujauzito
3.Kama kuna maabukizi na mashambulizi ya bakteria na virusi kwenye koo, tonsil na meneo mengine ya mdomoni
4.Kama umeng’atwa na buibui mwenye sumu, ama umekula uyoga ama umeng’atwa na wadudu
5.Kama unatumia meno ya bandia
6.Kama hufanyi usafi wa kinywa kwa umakini
7.Kama una maambukizi ya T.B ama ugonjwa wa rabies
8.Kama una kiungulia cha mara kwa mara
9.Mipasuko kwenye taya ma amifupa ya taya kutojipanga vyema
10.Vidonda vywnyw mfumo wa mmeng’enye wa chakula kama mdomoni, kooni na tumboni


NINI HUSABABISHA KUSHINDWA KUMEZA MATE AMA KUTEMA MATE YOTE?
Kama tulivyoona kuwa katika sababu zinazopelekea mate kujaa mdomoni ni kushindwa kuyameza yote, ama kuyatema yote. Sasa ni kitu gani husababisha hali hii?
1.Kuwa na shida ya kiafya kwenye mfumo wa fahamu
2.Kuwa na shida ya kiafyakwenye figo


SABABU NYINGINE ZINAZOPELEKEA MDOMO KUJAA MATE
1.Mpangilio mbaya wa meno
2.Majeraha kwenye mdomo
3.Hewa mbaya
4.Upungufu wa maji mwilini
5.Matatizo kwenye mfumo wa fahamu hasa katika kuhisi ladha ya chakula
6.Kama una maradhi ya pneumonia


NINI UFANYE KAMA UNA HILI TATIZO:
1.Kwa kupitia dalili zilizotajwa hapo juu, angalia ambayo huwenda ndio sababu kwako.
2.Kawaida tatizo hili halihitaji dawa, ila kama imezidi fika hospitali kwa uchunguzi zaidi.
3.Fika kituo cha afya kwa vipimo zaidi kama hali yako itaendelea kwa muda bila kurudi nyuma.

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 2766


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zifazofanana:-

Visababishi vya maambukizi kwenye milija na ovari
Posti hii inahusu zaidi visababishi vya maambukizi kwenye milija na, ni mambo yanayosababisha maambukizi kwenye milija na ovari. Soma Zaidi...

Naomb niulize ukiingiliana na mwanmke mweny ukimwi unaweza kuambikizwa na kusaambaaa kwa mda gan ndan ya mwil
Muda gani ukimwi huweza kuonekana mwilini ama kugundulika kama umeathirika, ni dalili zipo hujitokeza punde tu utakapoathirika Soma Zaidi...

Ugonjwa wa pepopunda kwa watoto
Pepopunda ni ugonjwa hatari wa kutishia maisha unaosababishwa na sumu inayojulikana Kama tetanospasmin inayotolewa kwenye majeraha yaliyoambukizwa. Bakteria ya pepopunda huingia kwenye mwili wa mtoto mchanga kupitia kisiki cha kitovu ambacho kimekatwa na Soma Zaidi...

nahis miguu pamoja na mikono kuishiwa nguvu ni mgongo kuuma ni dalili za ugonjwa gan ?
mm nahis miguu pamoja na mikono kuishiwa nguvu ni mgongo kuuma ni dalili za ugonjwa gan ? Soma Zaidi...

Maumivu ya magoti.
Maumivu ya magoti ni malalamiko ya kawaida ambayo huathiri watu wa umri wote. Maumivu ya goti yanaweza kuwa matokeo ya jeraha, kama vile ligament iliyopasuka au cartilage iliyochanika. Soma Zaidi...

ATHARI ZA KIAFYA ZA KUTOTIBU MALARIA AU KUCHELEWA KUTIBU MALARIA
Pindi malaria isipotibiwa inaweza kufanya dalili ziendelee na hatimaye kusababisha kifo. Soma Zaidi...

Tatizo la ngozi kuwasha (ugonjwa wa kuwashwa kwa ngozi
Dermatitis ni hali inayofanya ngozi yako kuwa nyekundu na kuwasha. Ni kawaida kwa watoto, lakini inaweza kutokea katika umri wowote. Hakuna tiba iliyopatikana ya ugonjwa wa Dermatitis Soma Zaidi...

IJUWE MINYOO, SABABU ZAKE, ATHARI ZA MINYOO, MATIBABU YAKE NA KUPAMBANA KWAKE
Soma Zaidi...

Dalilili za homa ya manjano
posti hii inahusu dalili za Homa ya Manjano ni maambukizi ya virusi yanayoenezwa na aina fulani ya mbu. Maambukizi hayo ni ya kawaida zaidi na kuathiri wasafiri na wakazi wa maeneo hayo. Soma Zaidi...

Chanzo cha VVU na UKIMWI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyanzo m ali mbali vinavyohisiwa kuwa chanzo cha UKIMWI Soma Zaidi...