Aina ya Magonjwa ya akili

Unyogovu (Depression ) ni mojawapo ya ugonjwa wa akili ambao unahusishwa na hisia za huzuni, kukosa matumaini, na kupoteza furaha au shauku katika shughuli za kila siku. Huu si tu hisia ya huzuni iliyokatisha tamaa, bali ni hali sugu inayoweza kuathiri mabadiliko ya mwili, mawazo, na tabia ya mtu. Unyogovu unaweza kutokea kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya kemikali katika ubongo, maumbile, mazingira, na matukio mbali mbali katika maisha ambayo kupelekea mgonjwa kuwa hivyo.

Unyogovu au Kwa kitaalamu depression ni hali ya kiakili inayoweza kuathiri njia ambavyo mtu anafikiri, anavyojihisi, na anavyofanya kazi katika maisha yake ya kila siku mara nyingi hali hii mtu ukumbana nayo kwenye mazingira ya Kila siku sio kwamba anazaliwa nayo.

Hapa kuna maelezo ya kina juu ya dalili za unyogovu au depression ambazo zinaweza kuonekana Kwa mtu na pia zinaweza zikaonekana Kwa mtu mara moja au zikatumia mda kuonekana kutokana na hali ya mtu.

 Dalili za Kihisia

mtu anaweza kubadilikw taratibu kutoka kwenye tabia yake ya kawaida akaanza kuwa na huzuni inayoendelea ambayo haiwezi kabisa kutoweka,Kutokuwa na matumaini,Hisia ya kukosa matumaini kuhusu maisha au hali ya baadaye,Kukata Tamaa: Mtu anaweza kuhisi kama hakuna chochote cha maana au kizuri kinachoweza kutokea,Wasiwasi au Kukasirika Mara nyingi watu wanahisi wasiwasi, hasira, au ukosefu wa utulivu kujiweka Kando.

.Dalili za Kimwili

Mabadiliko ya Kula  kupita kiasi au kupoteza hamu ya kula. Hii inaweza kusababisha kupoteza uzito au kuongeza uzito Kwa Wakati Mrefu Ndan Kuwepo kwa uchovu wa mara kwa mara bila sababu ya kimwili,maumivu Yasiyo na Sababu, Kuumwa kwa mwili kama vile maumivu ya kichwa, mgongo, au misuli ambayo hayawezi kueleweka,Usingizi Mzito au Watu wanaweza kukumbana na matatizo ya usingizi, kama vile kushindwa kulala au kulala kupita kiasi.

4. Dalili za Kijamii na Kitendo

Kukosa Hamu ya Shughuli Kupoteza hamu ya shughuli ambazo mara nyingi zilikuwa na furaha,Kujiondoa katika Mahusiano,Kutoroka kutoka kwa urafiki na familia, au kukwepa shughuli za kijamii,Mabadiliko katika Utendaji, Kushindwa kufanya kazi vizuri katika kazi, shule, au katika majukumu mengine ya kila siku.

5. Dalili za Wazo na Hisia

Mawazo ya Kufa,Watu wengine wanaweza kuwa na mawazo ya juu kuhusu kifo au kujiua, ambao ni dalili nzito ambazo zinahitaji msaada Zaidi,Kwa hiyo mtu mwenye depression anapaswa kutafutiwa tiba ipasayo baada ya kuona dalili ambazo zinampelekea kutaka kujiu.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Salvatory image Tarehe: 1970-01-01 03:33:45 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 331

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 web hosting    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Zijue dalili za maambukizi ndani ya sikio na madhara yake

Sikio ni mojawapo ya milango ya fahamu inayotumiwa kwa ajili ya kusikia, Kuna wakati mwingine hushambulia na bakteria na virusi

Soma Zaidi...
Dalili za madhara ya figo

Posti hii inahusu dalili za figo.figo husawazisha maji mwilini pamoja na kuchuja mkojo.

Soma Zaidi...
Vyanzo vya sumu mwilini.

Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya kuwepo kwa sumu mwilini, kwa sababu kuna wakati mwingine tunapata magonjwa na matatizo mbalimbali ya ki afya tunaangaika huku na huko kumbe sababu kubwa ni kuwepo kwa sumu mwilini na vyanzo vya sumu hiyo ni kama ifuatavy

Soma Zaidi...
Dalili za saratani (cancer)

Posti hii inahusu zaidi dalili za kansa, ni dalili ambazo utokea kwa mtu Mwenye tatizo la ugonjwa wa Kansa ingawa sio lazima dalili hizi kutokea tukadhani kuwa ni Kansa Ila zilizonyingi huwa ni kweli dalili za kansa.

Soma Zaidi...
Tiba ya vidonda vya tumbo na dawa zake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu Tina ya vidonda vya tumbo na dawa zake

Soma Zaidi...
Dalili za saratani ya ini

Posti hii inahusu zaidi dalili za saratani ya ini, ni baadhi ya Dalili ambazo zinaweza kujitokeza na kuona kwamba mtu fulani ana saratani ya ini.

Soma Zaidi...
Fikra potofu kuhusu vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya fikra potofu kuhusu vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri.

Posti hii inahusu zaidi kuwepo kwa vipele kwenye midomo na sehemu za siri .Ni ugonjwa ambao kwa kitaalamu huitwa herpes zoster

Soma Zaidi...
Madhara ya ugonjwa wa madonda ya koo usipotibiwa

Posti hii inahusu zaidi madhara ya ugonjwa wa madonda ya koo usipotibiwa, ugonjwa huu usipotibiwa unaweza sababisha madhara mbalimbali kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...