Aina ya Magonjwa ya akili
Unyogovu (Depression ) ni mojawapo ya ugonjwa wa akili ambao unahusishwa na hisia za huzuni, kukosa matumaini, na kupoteza furaha au shauku katika shughuli za kila siku. Huu si tu hisia ya huzuni iliyokatisha tamaa, bali ni hali sugu inayoweza kuathiri mabadiliko ya mwili, mawazo, na tabia ya mtu. Unyogovu unaweza kutokea kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya kemikali katika ubongo, maumbile, mazingira, na matukio mbali mbali katika maisha ambayo kupelekea mgonjwa kuwa hivyo.
Unyogovu au Kwa kitaalamu depression ni hali ya kiakili inayoweza kuathiri njia ambavyo mtu anafikiri, anavyojihisi, na anavyofanya kazi katika maisha yake ya kila siku mara nyingi hali hii mtu ukumbana nayo kwenye mazingira ya Kila siku sio kwamba anazaliwa nayo.
Hapa kuna maelezo ya kina juu ya dalili za unyogovu au depression ambazo zinaweza kuonekana Kwa mtu na pia zinaweza zikaonekana Kwa mtu mara moja au zikatumia mda kuonekana kutokana na hali ya mtu.
Dalili za Kihisia
mtu anaweza kubadilikw taratibu kutoka kwenye tabia yake ya kawaida akaanza kuwa na huzuni inayoendelea ambayo haiwezi kabisa kutoweka,Kutokuwa na matumaini,Hisia ya kukosa matumaini kuhusu maisha au hali ya baadaye,Kukata Tamaa: Mtu anaweza kuhisi kama hakuna chochote cha maana au kizuri kinachoweza kutokea,Wasiwasi au Kukasirika Mara nyingi watu wanahisi wasiwasi, hasira, au ukosefu wa utulivu kujiweka Kando.
.Dalili za Kimwili
Mabadiliko ya Kula kupita kiasi au kupoteza hamu ya kula. Hii inaweza kusababisha kupoteza uzito au kuongeza uzito Kwa Wakati Mrefu Ndan Kuwepo kwa uchovu wa mara kwa mara bila sababu ya kimwili,maumivu Yasiyo na Sababu, Kuumwa kwa mwili kama vile maumivu ya kichwa, mgongo, au misuli ambayo hayawezi kueleweka,Usingizi Mzito au Watu wanaweza kukumbana na matatizo ya usingizi, kama vile kushindwa kulala au kulala kupita kiasi.
4. Dalili za Kijamii na Kitendo
Kukosa Hamu ya Shughuli Kupoteza hamu ya shughuli ambazo mara nyingi zilikuwa na furaha,Kujiondoa katika Mahusiano,Kutoroka kutoka kwa urafiki na familia, au kukwepa shughuli za kijamii,Mabadiliko katika Utendaji, Kushindwa kufanya kazi vizuri katika kazi, shule, au katika majukumu mengine ya kila siku.
5. Dalili za Wazo na Hisia
Mawazo ya Kufa,Watu wengine wanaweza kuwa na mawazo ya juu kuhusu kifo au kujiua, ambao ni dalili nzito ambazo zinahitaji msaada Zaidi,Kwa hiyo mtu mwenye depression anapaswa kutafutiwa tiba ipasayo baada ya kuona dalili ambazo zinampelekea kutaka kujiu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Uchunguzi wa kuharisha damu na tiba yake
Posti hii inahusu zaidi uchunguzi wa kuharisha damu na Tiba yake, ni Ugonjwa ambao unaowashambulia sana watoto hasa wenye chini ya umri wa miaka mitano, kwa hiyo huoaugonjwa tunaweza kuutambua na kutibu kwa njia zifuatazo.
Soma Zaidi...Magonjwa ya moyo
Posti hii inahusu zaidi magonjwa ya moyo, kwa kawaida watu wakisikia habari za magonjwa ya moyo huwa hawaelewi yanakuwaje kuwaje, Leo nataka niwafahamishe kuhusu magonjwa ya moyo na sehemu mbalimbali zinazoathirika.
Soma Zaidi...Dalili za saratani ya tishu (leukemia)
Posti hii inazungumzia kuhusiana na saratani za tishu ambazo kitaalamu hujulikana Kama Leukemia kawaida huhusisha seli nyeupe za damu. Seli zako nyeupe za damu ni wapiganaji hodari wa maambukizo - kwa kawaida hukua na kugawanyika kwa utaratibu, kadri mwi
Soma Zaidi...Sababu za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.
Post hii inahusu zaidi Sababu za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, hali hii uwatokea sana wanawake zaidi ya wanaume, kwa kitaalamu hali hii ya kuwa na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo huitwa cystitis.
Soma Zaidi...KUJIANDAA KWA AJILI YA KUMUONA DAKTARI
KUJIANDAA KWA AJILI YA KUMUONA DAKTARI Fanya miadi na daktari wako wa kawaida ikiwa una ishara au dalili zinazokupa wasiwasi.
Soma Zaidi...