Simulizi za Hadithi EP 10 Part 3: Asubuhi yenye varangati

Simulizi za Hadithi EP 10 Part 3: Asubuhi yenye varangati

Muendelezo....

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

VARANGATI ASUBUHI;

Baada ya kugunduwa kuwa haikuwa ndoto kamaralzamani aliamini kuwa yule ndio mke ambaye baba yake alimchagulia. Hivyo akaenda kwa baba yake moja kwa moja na kumwambia “baba kuanzia sasa nimekubali kuoa” mfalme alifurahi sana. Furaha yake haikupimika maana hadi sharubu zilipepea vyema. Taarifa hii ilimchukiza sana waziri mkuu ambaye alitaka amuunganishie mwanaye aolewe na Kamaralzamani. Baada ya kitmya kidogo kamaralzamani akaongeza kusema “nitaoa tu kama utaniletea yule mwanamke niliyemuona jana usiku”

 

 

Hapo mfalme alishikwa na butwaa, jana usiku nini kilitokea kwa kamaralzamani. Mfalme ilibidi aulizie kwa walindani wa mlango wa prince. Nao walisema hawakuona mtu yeyote kuingia wala kutoka. Mfalme akadhani mwanae ana shida ya akili sasa. Kamaralzamani kythibitisha kauli yake akamuonyesha baba yake pete ya huyo mwanamke. Hali hizi zililichanganya sana baraza la mawaziri. Wapo waliokubaliana na kamaralzamani na wapo waliomuona sasa anachanganyikiwa.

 

 

Kwa upande wa pili kwa princes hali ilikuwa ni varangati.princes amekuwa kama ng’ombe aliyepandisha joto, hashikiki anamtaka mume aliyeletewa na baba yake jana usiku. Nae kuthibitisha kauli yake ni kukosekaana kwa pete yake moja. Princess alikuwa kila anapokwenda, anapolala huwa pete zake mbili anazo. Pete hizi aliachiwa na marehemu mama yake. Sasa leo pete moja kuwa haipo mikononi mwake halikuwa jambo la kawaida. Mfalme akaagiza princess awekwe chini ya ulinzi mkali huwenda akacanganyikiwa.

 

 

Kamaralzamani, naye ilibidi aongezewe ulizi. Ila alipewa ruhusa ya kutembea mjini kumtafuta huyo mwanamke kama atamuona. Hapo watu wa mjini nao wakapata kuona sura ya Kamaralzamani kwa mara ya kwanza. Wat walisifia sana uumbaji wa mwenyezi mungu rura ya kamaralzamani. Uzuri wa kamaralzamani ukaanza kuenea sasa nchini kutoka mijini kwenda vijijini. Hali hii pia ilifanywa kwa princess, kwa ulinzi kali aliruhusiwa kutembea mjini kumtafuta huyo mwanaume aliyemuona.

 

 

Hapo watu wakaanza kujuwa sura nzuri ya binti mfalme. Sifa na uzuri wa binti mfalme nazo zikazagaa nchini na maeneo ya jirani. Mwezi mmoja sasa umepita bila mafanikio. Mmoja katika mabinamu wa binti mfalme alimfuata binti mfalme na kutaka kujuwa jinsi huyo mwanaume alivyo.binamu huyu aliahidi kuwa atamtafuta hata ikiwezekana atembee dunia nzima hadi ampate. Princess akaanza kueleza sifa za mtu huyo katika sifa nyingi mwisho akaasema amafanana naye. Baada ya mazungumzo haya binamu wa bint mfamle akaahidi kuwa atatimiza ndoto ya binamu wake.

 

 

Binamu akaanza kutembea na baada ya kuda wa mwezi na nusu akafika nchini kwa wakina kmaralzamani. Mjini akakuta stori kumuhusu mtoto wa mfalme. Ila stori ile ikawa inafanana na ile ya binamu wake binti mfalme. Kijana ikabidi atafute njia ya kuonana na na mtoto wa mfalme bila mafanikio. Miezi miwili imefika sasa. Kule nyuma mtoto wa mfalme bint nurat akawa kama amechanganyikiwa mpaka mfalme akaagiza waganga waje kumuaguwa. Basi waganga wakawa wanashindana kuja kumuaguwa bila mafanikio. Ikafikia wakati mfalme akatangaza atakayemtibu na kupona binti yake ataozeshwa.

 

 

Kwa upande wa binamu wa binti mfalme aliendelea kutafuta juhudi zakuonana na kamaralzamani bila mafanikio. Sik moja akagundua kuwa alipo kamaralzamani kuna mto amabo mto huo unakwenda mnje ya ikulu. Hivyo aka kutumia njia hiyo. Siku hiyo akaogelea kisirisiri hadi akatokea kwenye bostani kubwa. Akajibanza kwenye kisima hadi uingia ndani bila hata ya kuonekana. Alipomuona tu akajuuwa ndie mwenyewe maana sifa zote alizotajiwa na binti mfalme zinafanana.

 

Kamaralzaman akamuashiria kamaralzamani asipige kelele. Kisha wakaingia ndani zaidi na kuanza kuzungumza. Binamu wa binti mfalme akazungumza kila anachokijuwa kuhusu hali ya dada yke. Kila anapozungumza kamaralzammani alikuwa akitokwa na chozi kwa furaha. Mwisho Kamaralzamani akamkumbatia binamu wa binti Mfalme na kuanza kulia kwa furaha. Kwa uthibitisho akamuonyesha ile pete. Hapo kaka binamu ndipo akaamini kabisa kuwa stori za watu hawa wawili ni za kweli. Lakini nini kilitokea bado ni hadithi nzito.

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Mankaa image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Burudani File: Download PDF Views 382

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 13: Sehemu ya sita ya safari ya Sinbad
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 13: Sehemu ya sita ya safari ya Sinbad

Muendelezo wa safari ya Sinbad iliyopo ndani ya kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA...

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 3 Part 2:  Simulizi ya tabibu wa mfalme
Simulizi za Hadithi EP 3 Part 2:  Simulizi ya tabibu wa mfalme

Simulizi ni nzuri sana maana zinafundisha na hazibagui mkubwa wala mdogo... tusikilize na kusoma kisa cha tabibu wa mfalme....kutoka katika kitabu cha kwanza cha HALIF LELA U LELA...

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 15: Hadithi ya safari ya Sinbad
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 15: Hadithi ya safari ya Sinbad

Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza muendelezo....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 7 Part 1: Aladini na taa ya mshumaa wa ajabu
Simulizi za Hadithi EP 7 Part 1: Aladini na taa ya mshumaa wa ajabu

Hii ni simulizi iliyopo ndani ya kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA......

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 12: Hadithi ya mfalme alikuwa kwenye kisima
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 12: Hadithi ya mfalme alikuwa kwenye kisima

Wapendwa tuendelee kuoata stori nzuri na za kusisimua kutoka katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP4  Part 5: Hadithi ya pili ya mtoto chongo wa mfalme
Simulizi za Hadithi EP4  Part 5: Hadithi ya pili ya mtoto chongo wa mfalme

Hadithi za HALIF LELA U LELA huwa zina muendelezo na hadidhi hii ni muondelezo wa kisa cha pili cha mtoto chongo wa mfamle ambayo imetoka ndani ya kitabu cha kwanza cha Hadithi za HALIF LELA U LELA.....

Soma Zaidi...