Simulizi za Hadithi EP 10 Part 4: Ndoa ya kwanza

Simulizi za Hadithi EP 10 Part 4: Ndoa ya kwanza

Muendelezo.....

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

NDOA YA HAMU

Basi hali ikawa kama hivyo wawili hawa binamu na Kamaralzamani wakaanza kupanga njama ya kuweza kuondoka eneo lile kuelekea nchi za mbali kwa ajili ya kukutana na binti mfalme. Basi Kamaralzamani akapanga njama ya kuwa aende kuwinda ili kiruhusiwa hukohuo atoroke. Basi siku hiyo ilifata yule mgeni wa siri wa Kamaralzamani akavaa mavazi ya walinzi ili asijulikane. Kamaralzamani akaenda kumuomba ruhusa baba yake ili aende kuwinda. Mfalme alifurahi sana kuona sasa akili ya mwanae imekaa sawa. Basi msafara mkubwa ukaandaliwa wa kwenda kuwinda.

 

 

Walipofika mawindoni Kamaralzamani na mgeni wake walitoroka na kukimbia. Walipofia njia panda wakachukuwa kisu na kumchinja sungura waliyemchukuwa nyumbani. Nguo za kamaralzamani wakazijaza damu ili ijulikane amejeruhiwa na kupotelea msituni. Wawili hawa waliendelea na safari yao msituni huku wanalala. Walihofia kupitia njiani kuwa huwenda wakaonekana na watu. Mwishowe wakafika bandarini. Kamaralzamani alibadili mavazi yake na kuwa ya kawaida. Ili sijulikane akaziba na sura yake. Walipanda kwenye marekebu ya kuelekea nchi za mashariki ya kati.

 

 

Baada ya mwendo wa mwezi mmoja hatimaye wakatokea kwenye nchi ya wakina binti sulatani. Katika hali kama ile ya kuziba sura Kamaralzamani aliweza kuingia nchini kwa siri. Hali ya binti sultani ilikuwa bado mbaya na waganha walikuwa wakiongezeka kila siku. Hakuna hata mmoja aliyefanikiwa kumtibu ukiachilia mbali donge ya kumuoa endapo mtu atafanikiwa kumtibu. Hii yote ni kwa sababu maradhi ya mapenzi hayatibiwi kwa dawa za mitishamba. Sasa ni wakati wa kuona tiba sahihi ya maradhi ya mapenzi. Mipango yote ikawa inapangwa kwa usiri kabisa. Sasa binabu akaenda kwa dada yake na kumpa habari za furaha kuwa muda si mrefu atapona.

 

 

Kamaralzamani katika mavari yake ya kiganga akiwa amejichora kigangaganga akawasili mbele ya sultani na kumueleza kuwa atatibu maradhi ya binti yake hata bila ya kumgusa. Basi sultani ilibiti akahudhurie tiba hiyo. Nje ya chumba alicho binti sultani zuri kubwa la rangi ya nyekundu pembeni, nyeusi katikati na madoa meupe yapo kati ya nyekundu na nyeusi. Chetezo kikubwa kikawekwa na ubani mweupe ukachomwa. Mganga akachukuwa pete yake kwa siri na kuiweka kwenye karatasi bila hata ya mtu yeyote kumuona. Akaweza na ubani mule kishaa akaanza kunogesha uwanja. Baada ya kumaliza mbwembwe zake akachukuwa ile karatasi na kuiandika maneno kadhaa na kuivingirisha vyema na kumwambia mmoja ya wajakazi akampe binti Sultani.

 

 

Alipoifunguwa ile karatasi binti Sultani moyo ulikaribia kupasuka kwa furaha. Watu wote waliwza kusikia kicheko chake, furaha yake ilienea kwenye bostani la maua. Sultani akasema kuwa sasa mtoto wangu amepona. Sultani ilibidi atimize ahadi yake. Baada ya kuangalia maendeleo ya binti ndani ya mwezi hapo Sultania kajiridhisha kupoana kwa mwanae na harusi kubwa ilifanya baada ya masiku kadhaa. Kamaralzamani mtoto wa pekee sasa amemuoa binti sultani mtoto wa pekee. Wawili hawa walifanana kwa uzuri wao kama vile ni mapacha. Hata hivyo historia za maisha yao pia zilifanana.

 

 

Ni miezi 5 sasa imepita toka kamaralzamani aondoke nchini kwake. Kule mfalme alijuwa mwanae kipenzi ndio amefariki tena. Lakini aliendelea kujipa moyo kwa sababu haiwezekani wakose hata kidole chake. Hali hii ilikuwa ikimpa matumaini kuwa kuna siku moja atakuja kumuona. Mawazo haya yalimfanya aanze kuumwa kwa kumuwaza mwanae wa pekee. Kadri siku zilivyokuwazikienda ndipo hali ya mfalme inazidi kuwa mbaya. Taarifa hizi ziliweza kumfikia Kamaralzamani kupitia binamu yao. Hivyo akaamuwa kuwa siku oja arudi nyumbani.

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Mankaa image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Burudani File: Download PDF Views 414

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 15: Hadithi ya safari ya Sinbad
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 15: Hadithi ya safari ya Sinbad

Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza muendelezo....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 12: Tabibu asimulia hadithi
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 12: Tabibu asimulia hadithi

Hii ni hadithi iliyopo ndan ya kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 18: Binti wa pili mwimba mashahiri mwenye makovu
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 18: Binti wa pili mwimba mashahiri mwenye makovu

Mwendelezo wa hadithi kutoka kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA......

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 4: Kilema mtanashati asiye na mkono
Simulizi za Hadithi EP 6 Part 4: Kilema mtanashati asiye na mkono

Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili.....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 7: Sehemu ya nne ya safari ya Sinbad
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 7: Sehemu ya nne ya safari ya Sinbad

Muendelezo wa hadithi ya safari ya safari ya Sinbad iliyopo kwenye hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza.....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 17: Ufupisho wa ALIFU LELA U LELA KITABU CHA KWANZA
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 17: Ufupisho wa ALIFU LELA U LELA KITABU CHA KWANZA

Huu ni ufupisho mfupi kuhusiana na kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA...

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 17: Hadithi ya Malipo ya wema ni wema
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 17: Hadithi ya Malipo ya wema ni wema

Mwendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza.....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 11: Kisa cha Kalid na Jalid
Simulizi za Hadithi EP 4 Part 11: Kisa cha Kalid na Jalid

Tuendelee kusikiliza na kusoma visa, hadithi, na simulizi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza tuwe pamoja mpka mwisho......

Soma Zaidi...