image

Simulizi za Hadithi EP 10 Part 4: Ndoa ya kwanza

Muendelezo.....

NDOA YA HAMU

Basi hali ikawa kama hivyo wawili hawa binamu na Kamaralzamani wakaanza kupanga njama ya kuweza kuondoka eneo lile kuelekea nchi za mbali kwa ajili ya kukutana na binti mfalme. Basi Kamaralzamani akapanga njama ya kuwa aende kuwinda ili kiruhusiwa hukohuo atoroke. Basi siku hiyo ilifata yule mgeni wa siri wa Kamaralzamani akavaa mavazi ya walinzi ili asijulikane. Kamaralzamani akaenda kumuomba ruhusa baba yake ili aende kuwinda. Mfalme alifurahi sana kuona sasa akili ya mwanae imekaa sawa. Basi msafara mkubwa ukaandaliwa wa kwenda kuwinda.

 

 

Walipofika mawindoni Kamaralzamani na mgeni wake walitoroka na kukimbia. Walipofia njia panda wakachukuwa kisu na kumchinja sungura waliyemchukuwa nyumbani. Nguo za kamaralzamani wakazijaza damu ili ijulikane amejeruhiwa na kupotelea msituni. Wawili hawa waliendelea na safari yao msituni huku wanalala. Walihofia kupitia njiani kuwa huwenda wakaonekana na watu. Mwishowe wakafika bandarini. Kamaralzamani alibadili mavazi yake na kuwa ya kawaida. Ili sijulikane akaziba na sura yake. Walipanda kwenye marekebu ya kuelekea nchi za mashariki ya kati.

 

 

Baada ya mwendo wa mwezi mmoja hatimaye wakatokea kwenye nchi ya wakina binti sulatani. Katika hali kama ile ya kuziba sura Kamaralzamani aliweza kuingia nchini kwa siri. Hali ya binti sultani ilikuwa bado mbaya na waganha walikuwa wakiongezeka kila siku. Hakuna hata mmoja aliyefanikiwa kumtibu ukiachilia mbali donge ya kumuoa endapo mtu atafanikiwa kumtibu. Hii yote ni kwa sababu maradhi ya mapenzi hayatibiwi kwa dawa za mitishamba. Sasa ni wakati wa kuona tiba sahihi ya maradhi ya mapenzi. Mipango yote ikawa inapangwa kwa usiri kabisa. Sasa binabu akaenda kwa dada yake na kumpa habari za furaha kuwa muda si mrefu atapona.

 

 

Kamaralzamani katika mavari yake ya kiganga akiwa amejichora kigangaganga akawasili mbele ya sultani na kumueleza kuwa atatibu maradhi ya binti yake hata bila ya kumgusa. Basi sultani ilibiti akahudhurie tiba hiyo. Nje ya chumba alicho binti sultani zuri kubwa la rangi ya nyekundu pembeni, nyeusi katikati na madoa meupe yapo kati ya nyekundu na nyeusi. Chetezo kikubwa kikawekwa na ubani mweupe ukachomwa. Mganga akachukuwa pete yake kwa siri na kuiweka kwenye karatasi bila hata ya mtu yeyote kumuona. Akaweza na ubani mule kishaa akaanza kunogesha uwanja. Baada ya kumaliza mbwembwe zake akachukuwa ile karatasi na kuiandika maneno kadhaa na kuivingirisha vyema na kumwambia mmoja ya wajakazi akampe binti Sultani.

 

 

Alipoifunguwa ile karatasi binti Sultani moyo ulikaribia kupasuka kwa furaha. Watu wote waliwza kusikia kicheko chake, furaha yake ilienea kwenye bostani la maua. Sultani akasema kuwa sasa mtoto wangu amepona. Sultani ilibidi atimize ahadi yake. Baada ya kuangalia maendeleo ya binti ndani ya mwezi hapo Sultania kajiridhisha kupoana kwa mwanae na harusi kubwa ilifanya baada ya masiku kadhaa. Kamaralzamani mtoto wa pekee sasa amemuoa binti sultani mtoto wa pekee. Wawili hawa walifanana kwa uzuri wao kama vile ni mapacha. Hata hivyo historia za maisha yao pia zilifanana.

 

 

Ni miezi 5 sasa imepita toka kamaralzamani aondoke nchini kwake. Kule mfalme alijuwa mwanae kipenzi ndio amefariki tena. Lakini aliendelea kujipa moyo kwa sababu haiwezekani wakose hata kidole chake. Hali hii ilikuwa ikimpa matumaini kuwa kuna siku moja atakuja kumuona. Mawazo haya yalimfanya aanze kuumwa kwa kumuwaza mwanae wa pekee. Kadri siku zilivyokuwazikienda ndipo hali ya mfalme inazidi kuwa mbaya. Taarifa hizi ziliweza kumfikia Kamaralzamani kupitia binamu yao. Hivyo akaamuwa kuwa siku oja arudi nyumbani.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Mankaa Tarehe 2024-09-10 15:10:44 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 90


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Nudhini na mtumwa
Muendelezo....... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 3: Aladini akiwa na binti wa mfalme
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 2 Part 1: Hadithi ya jini na mfanya biashara.
Hadithi hii ya jina na mfanya biashara imetoka katika kitabu cha kwanza cha simulizi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza karibu tusikilize simulizi nzuri na zakusisimua Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 15: Hadithi ya safari ya Sinbad
Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 16: Viatu vya ajabu vyaondoka na mkono wangu
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 14: Wageni
Simulizii hii ni nzuri na ni mojawapo ya hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 10: Jumba la Aladini
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Hadithi ya Nurdini Mtoto wa Waziri
Hii ni hadithi ya kitabu cha tatu cha hadithi za HALIF LELA U LELA... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 9: Hadithi ya binti wa mfalme kufichwa.
Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 14: Hadithi ya kifo cha kujionea
Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza Muendelezo wa safari ya Sinbad Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 6: Sehemu ya tatu ya safari ya Sinbad
Muendelezo wa sehemu ya tatu ya safari ya Sinbad iliyopo kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 2: Sehemu ya safari ya kwanza ya sinbad
Muendelezo wa stori ya safari ya Sinbad ambayo ipo kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...