Menu



Simulizi za Hadithi EP 10 Part 4: Ndoa ya kwanza

Muendelezo.....

NDOA YA HAMU

Basi hali ikawa kama hivyo wawili hawa binamu na Kamaralzamani wakaanza kupanga njama ya kuweza kuondoka eneo lile kuelekea nchi za mbali kwa ajili ya kukutana na binti mfalme. Basi Kamaralzamani akapanga njama ya kuwa aende kuwinda ili kiruhusiwa hukohuo atoroke. Basi siku hiyo ilifata yule mgeni wa siri wa Kamaralzamani akavaa mavazi ya walinzi ili asijulikane. Kamaralzamani akaenda kumuomba ruhusa baba yake ili aende kuwinda. Mfalme alifurahi sana kuona sasa akili ya mwanae imekaa sawa. Basi msafara mkubwa ukaandaliwa wa kwenda kuwinda.

 

 

Walipofika mawindoni Kamaralzamani na mgeni wake walitoroka na kukimbia. Walipofia njia panda wakachukuwa kisu na kumchinja sungura waliyemchukuwa nyumbani. Nguo za kamaralzamani wakazijaza damu ili ijulikane amejeruhiwa na kupotelea msituni. Wawili hawa waliendelea na safari yao msituni huku wanalala. Walihofia kupitia njiani kuwa huwenda wakaonekana na watu. Mwishowe wakafika bandarini. Kamaralzamani alibadili mavazi yake na kuwa ya kawaida. Ili sijulikane akaziba na sura yake. Walipanda kwenye marekebu ya kuelekea nchi za mashariki ya kati.

 

 

Baada ya mwendo wa mwezi mmoja hatimaye wakatokea kwenye nchi ya wakina binti sulatani. Katika hali kama ile ya kuziba sura Kamaralzamani aliweza kuingia nchini kwa siri. Hali ya binti sultani ilikuwa bado mbaya na waganha walikuwa wakiongezeka kila siku. Hakuna hata mmoja aliyefanikiwa kumtibu ukiachilia mbali donge ya kumuoa endapo mtu atafanikiwa kumtibu. Hii yote ni kwa sababu maradhi ya mapenzi hayatibiwi kwa dawa za mitishamba. Sasa ni wakati wa kuona tiba sahihi ya maradhi ya mapenzi. Mipango yote ikawa inapangwa kwa usiri kabisa. Sasa binabu akaenda kwa dada yake na kumpa habari za furaha kuwa muda si mrefu atapona.

 

 

Kamaralzamani katika mavari yake ya kiganga akiwa amejichora kigangaganga akawasili mbele ya sultani na kumueleza kuwa atatibu maradhi ya binti yake hata bila ya kumgusa. Basi sultani ilibiti akahudhurie tiba hiyo. Nje ya chumba alicho binti sultani zuri kubwa la rangi ya nyekundu pembeni, nyeusi katikati na madoa meupe yapo kati ya nyekundu na nyeusi. Chetezo kikubwa kikawekwa na ubani mweupe ukachomwa. Mganga akachukuwa pete yake kwa siri na kuiweka kwenye karatasi bila hata ya mtu yeyote kumuona. Akaweza na ubani mule kishaa akaanza kunogesha uwanja. Baada ya kumaliza mbwembwe zake akachukuwa ile karatasi na kuiandika maneno kadhaa na kuivingirisha vyema na kumwambia mmoja ya wajakazi akampe binti Sultani.

 

 

Alipoifunguwa ile karatasi binti Sultani moyo ulikaribia kupasuka kwa furaha. Watu wote waliwza kusikia kicheko chake, furaha yake ilienea kwenye bostani la maua. Sultani akasema kuwa sasa mtoto wangu amepona. Sultani ilibidi atimize ahadi yake. Baada ya kuangalia maendeleo ya binti ndani ya mwezi hapo Sultania kajiridhisha kupoana kwa mwanae na harusi kubwa ilifanya baada ya masiku kadhaa. Kamaralzamani mtoto wa pekee sasa amemuoa binti sultani mtoto wa pekee. Wawili hawa walifanana kwa uzuri wao kama vile ni mapacha. Hata hivyo historia za maisha yao pia zilifanana.

 

 

Ni miezi 5 sasa imepita toka kamaralzamani aondoke nchini kwake. Kule mfalme alijuwa mwanae kipenzi ndio amefariki tena. Lakini aliendelea kujipa moyo kwa sababu haiwezekani wakose hata kidole chake. Hali hii ilikuwa ikimpa matumaini kuwa kuna siku moja atakuja kumuona. Mawazo haya yalimfanya aanze kuumwa kwa kumuwaza mwanae wa pekee. Kadri siku zilivyokuwazikienda ndipo hali ya mfalme inazidi kuwa mbaya. Taarifa hizi ziliweza kumfikia Kamaralzamani kupitia binamu yao. Hivyo akaamuwa kuwa siku oja arudi nyumbani.

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Mankaa image Tarehe 2024-09-10 15:10:44 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 220


Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zifazofanana:-

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 12: Sehemu ya tano ya safari ya Sinbad
Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 9: Hadithi ya binti wa ndotoni.
Simulizi hii pia inapatikana kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 18: Binti wa pili mwimba mashahiri mwenye makovu
Mwendelezo wa hadithi kutoka kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Mtumwa wa mfalme na mawaziri
Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha tatu..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 9: Hadithi ya binti wa mfalme kufichwa.
Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 1: Aladini na taa ya mshumaa wa ajabu
Hii ni simulizi iliyopo ndani ya kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 2: Kisa cha kinyozi msiri..
Karibuni tuendelee kusimuliana stori za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza, stori nzuri sana na za kuvutia zimeandaliwa kwaajili ya kujifunza na kujiburudisha pia..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 2 Part 3: Hadithi ya mzee wa pili na mbwa wawili weusi.
Simulizi za HALIF LELA U LELA ni nziri sana tuwe pamoja kusikiliza kisa cha mzee wa pili na mbwa wawili weusi... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 13: Jaribio kwa Aladini kwa mara ya kwanza
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 9: Hadithi ya deni la mapenzi
Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili.... Soma Zaidi...