image

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 5: Nani ni binti?

Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili....

BINTI HUYU NI NANI?

Siku iliyofuata nilioga mapema, kisha nikavaa ngu zangu safi na kuelekea pale dukani. Loo! Yule binti akaja tena, alipokuja moja kwa moja akakaa karibu nami na kutoa kitambaa kilichofungwa bundu. Kisha akaniambia “ Chukuwa hii malipo yako kwa bidhaa yako siku ya jana”. nikachukuwa na kumpatia muuzaji wangu ahifadhi. Sikuwa na haja ya kuhakiki kama pesa imetimia ama laa.

 

 

 

Basi nikaendelea kuzungumza naye maneno ya hapa na pale. Kisha nikaanza kuchomekea maneno ya ishara. Bila shaka alizifahamu vyema ishara zangu. Kwa ghafla alionyesha kukasirika na ndipo alisimama na kuondoka zake. Nilijijutia nafsi yangu kwa nini nimeongea naye kwa ishara za mapenzi. Aliondoka tena bila hata kuniambia anaitwa nani na wapi anakaa. Aluondoka hata sijazungumza hasa nini kipo moyoni kwangu.

 

 

 

Hakika siku hiyo niliiona ndefu sana na sikuweza kula chochote. Nilipata pia kujiwazia huenda binti yule sio mtu wa kawaida, huenda ni jini ama malaika ametumwa kuja kunijaribu. Siku ya tatu yake nikaamua kutembea mjini nkiamini huenda nikakutana naye kwa bahati mbaya. Loo! Sikuiliisha bila hata kukutana na sura yake.

 

 

 

Siku ya nne nilikaa kenye duka lile na ghafla akanijia bibi mmoja. Akanieleza kuwa ameagizwa na bosi wake aje anichukuwe ana mazungumzo. Bibi alikuwa ni mjakazi katika jumba la kitajiri. Nilifahamu hilo baada ya kuona mavazi yake. Nilikubali wito kwa kuamini atakuwa ni yule mrembo aliyeteka hsia zangu, aliyechukuwa moyo wangu, aliyenikosesha hamu ya kula wala kulala.

 

 

 

Niliongozana na bibi yule hata tukafika kwenye nyumba ya wageni. Hap akanieleza niingie kwani bosi wake yumbo ndani. Nilipoingia tu nikakaribishwa na manukato yanayonukia kwa uzuri sana, Loo! Alikuwa ni yule mrembo, alikuwa amependeza sana siku hii. Alvaa mavazi marefu yenye rangi za kuvitia kama tausi. Akanikaribisha kwnye busati lililotandika katikati ya chumba.

 

 

 

Hapo wakaja mabinti wengine wawili vigori, wakaleta vinywaji na kukaa pembeni. Akanieleza kuwa hawa pia ni wafanya kazi wake. Hawezi kukaa peke yake kwani faragha ya mwanaume na mwanamke wasio oana hairuhusiwi kwenye dini. Basi tulianza kuzungumza hapa na pale wakati huo mabinti wale wapo. Mwisho niamueleza uhalizi wa moyo wangu juu yake, ni kiasi gani ninampenda, ni taabu gani nimeipata kwa siku tatu hizi toka niutane naye.

 

 

 

Nilimueleza vyeote kuhusu kuwa sikuwa na usingizi wala sikuona tamu ya chakual. Wakati wote niliokuwa nachungumza yeye alikuwa akitokwa na machozi tuu. Moja wa mabinti wale akachukuwa kitambaa cha hariri kilicho zungushiwa na dhahabu nyekundu, na kutiwa manukato yanayonukia kama miski nyekundu ya kutoka india. Alimfuta machozi kisha akasema “ kwa hakika unayoyasema ndiyo yaliyomkuta bosi wetu, toka majuzi anakazi ya kukuwaza, kukutaja, kukufikiria, hali, halali, hanywi kwa upendo alionao kwako”.

 

 

 

Nilitamani kumfuta machozi ila nikaogopa kumvunjia heshima mbele ya wafanyakazi wake. Ndipo akasema kuwa “ kwa hakika walioyasema ndugu zangu ni sahihi, wewe ni mtu wa kwanza kukupenda, na amini nakupenda kweli, naomba tuoane. Kwani siwezi kukukosa tena, siwezi kuonja tena adhabu ya kuwa mbali nawe, uso wako kama lulu kwangu, katu sichoki kukutazama, tabasamu lako…… mmmhmmh nakupenda sana.”

 

 

Basi aliendelea kuzungumza kisha tukakubaliana kuwa tuoane ila ndoa iwe kwa siri kwa sababu, mimi ni mtu ambaye bado ni mgeni hivyo haitakuwa vyema kutangaza harusi yetu, na mimi ninatambulikamkwa utajiri nilio nao, hivyo wanaweza kukufanyia fitina, na hata kukuumiza. Siku ilofata ilikuwa ni ijumaa. Basi akanielekeza kwake ili niende baada ya kuswali ijumaa ili ndoa ikafanyike. Basi tukaagana pale na mimi nikaondoka na wao wakaelekea zao.

 

 

 

Sikuwa na haja tena ya kulijuwa jina lake maana niliamini kuwa nitalijuwa siku ya harusi. Nilijuwa kuwa yeye ni tajiri na ni mtoto wa tajiri. Niliamini ili niweze kuishi naye ni lazima nitumie pesa vyema. Basi siku hiyo sikuweza tena kulala kwa kuisubiri asubuhi ifike, ili nikamuoe kipenzi maridhawa.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Mankaa Tarehe 2024-09-10 10:56:17 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 45


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Simulizi za Hadithi EP 3 Part 5: Simulizi ya samaki wa ajabu
Simulizii hii inapatikana kwenye hadhithi za HALIF LELA U LELA katika kitabu cha kwanza.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 17: Ufupisho wa ALIFU LELA U LELA KITABU CHA KWANZA
Huu ni ufupisho mfupi kuhusiana na kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 16: Kitabu cha ajabu
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 1: Hadithi ya chongo watatu, watoto wa mfalme na wanawake wa Baghdad.
Skmulizii hii pia imetoka kitabu cha kwanza cha HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 3 Part 1: Kisa cha mvuvi na jini
Simulizii hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha HALIF LELA U LELA .... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 25: Kaka wa nne wa kinyozi
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 20: Kinyozi maishani mwangu
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 7: Sehemu ya nne ya safari ya Sinbad
Muendelezo wa hadithi ya safari ya safari ya Sinbad iliyopo kwenye hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 18: Hadithi ya fundi cherehani
Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Rafiki wa ukweli
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 10: Jumba la Aladini
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 10 Part 3: Asubuhi yenye varangati
Muendelezo.... Soma Zaidi...