njia ya maandishi
(e) Njia ya Maandishi:
Njia nyingine anayoitumia Allah (s.w) katika kuwasiliana na waja wake ni njia ya maandishi, yaani maandishi yaliyoandikwa tayari.
Nabii Mussa (a.s) aliletewa ujumbe kutoka kwa Allah (s.w) kwa maandishi yaliyoandikwa tayari katika mbao kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo: “Na tukamwandikia katika mbao kila kitu mawaidha (ya kila namna) na maelezo ya kila jambo.
Basi yashike kwa imara na uwaamrishe watu wako wayashike vema haya…” (7:145) “Na Musa zilipotulia ghadhabu zake, aliziokota zile mbao.
Na katika maandiko yake (hizo mbao) ulikuwamo uwongofu na rehema kwa wale wanaomuogopa Mola wao”. (7:154). Kwa ujumla tumeona kuwa chanzo cha elimu ni “Allah (s.w). Lolote tunalolifahamu tumefunzwa na Allah kwa njia mojawapo katika njia tano tulizoziona.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Share follows: 0 |
Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 web hosting 👉4 ai web app 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 web hosting 👉4 ai web app 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Kwanini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini?
Mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)..
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Maswali kuhusu njia za kumjua mwenyezi Mungu
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu
Soma Zaidi...(c)Vipawa vya Mwanaadamu
Vipawa vya mwanaadamu ni sababu nyingine inayomfanya mwanaadamu asiweze kuishi bila ya kufuata dini moja au nyingine.
Soma Zaidi...