Kuongea na Allah (s.w) nyuma ya Pazia

Kuongea na Allah (s.w) nyuma ya Pazia

Hii ni njia ambayo mwanaadamu huongeleshwa moja kwa moja na Allah (s.

Download Post hii hapa

Kuongea na Allah (s.w) nyuma ya Pazia

(b)Kuongea na Allah (s.w) nyuma ya Pazia


Hii ni njia ambayo mwanaadamu huongeleshwa moja kwa moja na Allah (s.w) kwa sauti ya kawaida pasina kumuona. Kutokana na ushahidi wa Qur-an njia hii imetumika kwa Mitume na wateule wengine wa Allah (s.w).


Nabii Mussa (a.s) ni miongoni mwa Mitume waliosemeshwa na Allah (s.w).kama tunavyofahamishwa kisa chake katika Qur-an: Basi Musa alipotimiza muda, akasafiri pamoja na ahali zake (watu wake kurejea kwao Misri). Aliona moto upande wa mlimani akawaambia ahali zake; ‘Ngojeni, hakika nimeona moto, labda nitakuleteeni habari za huko au kijinga cha moto ili muote! (28:29) 8 Basi alipoufikia aliitwa kutoka upande wa kuliani wa bonde hilo katika kiwanja kilichobarikiwa, kutoka mtini: “Ewe Mussa! Bila shaka mimi ndiye Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwengu.” (28:30) Kwa njia ya nyuma ya pazia, Nabii Mussa (a.s) aliongea na Allah mara nyingi na mara zote hizo hakuweza kumuona. Alipoomba amuone alijibiwa kama inavyooneshwa katika aya zifuatazo:


Na alipofika Mussa katika miadi yetu na Mola wake akazungumza naye, (Mussa) akasema: “Mola wangu! Nionyeshe (nafsi yako) ili nikuone” Akasema (Mwenyezi Mungu): “Hutaniona, lakini tazama jabali (lililoko mbele yako) kama litakaa mahali pake utaweza kuniona”. Basi Mola wake alipojionyesha katika jabali, alilifanya liwe lenye kuvunjika vunjika na Mussa akaanguka hali ya kuzimia. Alipozindukana akasema “Utukufu ni wako. Natubu kwako, na mimi ni wa kwanza wa wanaoamini (haya)” (7:143).


Pia tunafahamishwa katika Qur-an kuwa Bibi Maryam, mama wa Nabii Issa (a.s) naye aliongeleshwa nyuma ya pazia wakati wa kumzaa Issa Bin Maryamu kama ilivyo katika aya zifuatazo: 9 “Kisha uchungu ukampeleka katika shina la mtende, (akawa anazaa na huku) anasema:“Laiti ningelikufa kabla ya haya, na ningekuwa niliyesahaulika kabisa.(19:23) Mara ikamfikia sauti kutoka chini yake ikamwambia usihuzunike. Hakika Mola wako amejaalia kijito cha maji chini yako.(19:24) na litikise kwako shina la mtende, litakuangushia tende nzuri, zilizo mbivu. (19:25) Basi ule na unywe na litulie jicho (lako). Na kama ukimuona mtu yeyote (akauliza habari juu ya mtoto huyu), sema:“Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwingi wa Rehma ya kufunga, kwa hiyo leo sitasema na mtu” (19:26).




                   



Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 2000

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Nguzo za imani katika uislamu na mafunzo yake
Nguzo za imani katika uislamu na mafunzo yake

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu nuzo 6 za imani ya uislamu na pia utajifunz akuhusu mafunzo yanayoweza kupatikana kwenye Nguzo hizi.

Soma Zaidi...
Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)
Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)

Nguzo za Imani (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maana ya Elimu katika uislamu na nani aliye elimika?
Maana ya Elimu katika uislamu na nani aliye elimika?

Hili ni swali kutoka katika maarifa ya elimu ya dini ya kiislamu kidato cha kwanza (EDK FORM 1)

Soma Zaidi...
Udhaifu wa mtazamo wa makafiri juu ya dini dhidi ya mtazamo wa uislamu
Udhaifu wa mtazamo wa makafiri juu ya dini dhidi ya mtazamo wa uislamu

Somo Hili linaeleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Shahada mbili
Shahada mbili

Kwenye mada hii tutajifunza shahada mbili,tafsiri ya shahada kstika maisha ya kila siku.

Soma Zaidi...