Hii ni njia ambayo mwanaadamu huongeleshwa moja kwa moja na Allah (s.
Hii ni njia ambayo mwanaadamu huongeleshwa moja kwa moja na Allah (s.w) kwa sauti ya kawaida pasina kumuona. Kutokana na ushahidi wa Qur-an njia hii imetumika kwa Mitume na wateule wengine wa Allah (s.w).
Nabii Mussa (a.s) ni miongoni mwa Mitume waliosemeshwa na Allah (s.w).kama tunavyofahamishwa kisa chake katika Qur-an: Basi Musa alipotimiza muda, akasafiri pamoja na ahali zake (watu wake kurejea kwao Misri). Aliona moto upande wa mlimani akawaambia ahali zake; ‘Ngojeni, hakika nimeona moto, labda nitakuleteeni habari za huko au kijinga cha moto ili muote! (28:29) 8 Basi alipoufikia aliitwa kutoka upande wa kuliani wa bonde hilo katika kiwanja kilichobarikiwa, kutoka mtini: “Ewe Mussa! Bila shaka mimi ndiye Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwengu.” (28:30) Kwa njia ya nyuma ya pazia, Nabii Mussa (a.s) aliongea na Allah mara nyingi na mara zote hizo hakuweza kumuona. Alipoomba amuone alijibiwa kama inavyooneshwa katika aya zifuatazo:
Na alipofika Mussa katika miadi yetu na Mola wake akazungumza naye, (Mussa) akasema: “Mola wangu! Nionyeshe (nafsi yako) ili nikuone” Akasema (Mwenyezi Mungu): “Hutaniona, lakini tazama jabali (lililoko mbele yako) kama litakaa mahali pake utaweza kuniona”. Basi Mola wake alipojionyesha katika jabali, alilifanya liwe lenye kuvunjika vunjika na Mussa akaanguka hali ya kuzimia. Alipozindukana akasema “Utukufu ni wako. Natubu kwako, na mimi ni wa kwanza wa wanaoamini (haya)” (7:143).
Pia tunafahamishwa katika Qur-an kuwa Bibi Maryam, mama wa Nabii Issa (a.s) naye aliongeleshwa nyuma ya pazia wakati wa kumzaa Issa Bin Maryamu kama ilivyo katika aya zifuatazo: 9 “Kisha uchungu ukampeleka katika shina la mtende, (akawa anazaa na huku) anasema:“Laiti ningelikufa kabla ya haya, na ningekuwa niliyesahaulika kabisa.(19:23) Mara ikamfikia sauti kutoka chini yake ikamwambia usihuzunike. Hakika Mola wako amejaalia kijito cha maji chini yako.(19:24) na litikise kwako shina la mtende, litakuangushia tende nzuri, zilizo mbivu. (19:25) Basi ule na unywe na litulie jicho (lako). Na kama ukimuona mtu yeyote (akauliza habari juu ya mtoto huyu), sema:“Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwingi wa Rehma ya kufunga, kwa hiyo leo sitasema na mtu” (19:26).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Ninichanzo cha Elimu? (EDK form 1 Dhanaya Elimu)
Soma Zaidi...Je ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya kuwa na dini?. Vipawa alivyopewa na Allahni jibu tosha juu ya swali jilo
Soma Zaidi...Faradhi kwa maiti ya muislamu (edk form 2:dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Uislamu unaitazama dini katika nyanja zote za maisha ya mwanadamu. Hii ni tofauti na mtazamo wa kikafiri juu ya dini.
Soma Zaidi...Katika kipengele hich tutajifunza dhana ya ibada katika uislamu,maana ua ibada
Soma Zaidi...عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم قَالَ: "مَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاَللَّهِ وَالْيَوْمِ...
Soma Zaidi...