Kuongea na Allah (s.w) nyuma ya Pazia

Hii ni njia ambayo mwanaadamu huongeleshwa moja kwa moja na Allah (s.

Kuongea na Allah (s.w) nyuma ya Pazia

(b)Kuongea na Allah (s.w) nyuma ya Pazia


Hii ni njia ambayo mwanaadamu huongeleshwa moja kwa moja na Allah (s.w) kwa sauti ya kawaida pasina kumuona. Kutokana na ushahidi wa Qur-an njia hii imetumika kwa Mitume na wateule wengine wa Allah (s.w).


Nabii Mussa (a.s) ni miongoni mwa Mitume waliosemeshwa na Allah (s.w).kama tunavyofahamishwa kisa chake katika Qur-an: Basi Musa alipotimiza muda, akasafiri pamoja na ahali zake (watu wake kurejea kwao Misri). Aliona moto upande wa mlimani akawaambia ahali zake; ‘Ngojeni, hakika nimeona moto, labda nitakuleteeni habari za huko au kijinga cha moto ili muote! (28:29) 8 Basi alipoufikia aliitwa kutoka upande wa kuliani wa bonde hilo katika kiwanja kilichobarikiwa, kutoka mtini: “Ewe Mussa! Bila shaka mimi ndiye Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwengu.” (28:30) Kwa njia ya nyuma ya pazia, Nabii Mussa (a.s) aliongea na Allah mara nyingi na mara zote hizo hakuweza kumuona. Alipoomba amuone alijibiwa kama inavyooneshwa katika aya zifuatazo:


Na alipofika Mussa katika miadi yetu na Mola wake akazungumza naye, (Mussa) akasema: “Mola wangu! Nionyeshe (nafsi yako) ili nikuone” Akasema (Mwenyezi Mungu): “Hutaniona, lakini tazama jabali (lililoko mbele yako) kama litakaa mahali pake utaweza kuniona”. Basi Mola wake alipojionyesha katika jabali, alilifanya liwe lenye kuvunjika vunjika na Mussa akaanguka hali ya kuzimia. Alipozindukana akasema “Utukufu ni wako. Natubu kwako, na mimi ni wa kwanza wa wanaoamini (haya)” (7:143).


Pia tunafahamishwa katika Qur-an kuwa Bibi Maryam, mama wa Nabii Issa (a.s) naye aliongeleshwa nyuma ya pazia wakati wa kumzaa Issa Bin Maryamu kama ilivyo katika aya zifuatazo: 9 “Kisha uchungu ukampeleka katika shina la mtende, (akawa anazaa na huku) anasema:“Laiti ningelikufa kabla ya haya, na ningekuwa niliyesahaulika kabisa.(19:23) Mara ikamfikia sauti kutoka chini yake ikamwambia usihuzunike. Hakika Mola wako amejaalia kijito cha maji chini yako.(19:24) na litikise kwako shina la mtende, litakuangushia tende nzuri, zilizo mbivu. (19:25) Basi ule na unywe na litulie jicho (lako). Na kama ukimuona mtu yeyote (akauliza habari juu ya mtoto huyu), sema:“Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwingi wa Rehma ya kufunga, kwa hiyo leo sitasema na mtu” (19:26).




                   



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 2443

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 web hosting    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Maswali kuhusu njia za kumjua mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Tawhiid

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Ni Ipi Elimu yenye manufaa

Elimu inaweza kugawanyika katika makundibmrngine mawili ambayo ni elimu yenye manufaa na elimubisiyi na manufaa

Soma Zaidi...
Mgawanyiko wa Elimu katika mtazamo wa Uislamu

Katika Uislamu elimu imegawanyika katika Elimu ya muongozo na elimu ya mazingira.

Soma Zaidi...
Ni lipi lengo la Elimu katika yislamu?

Ni lipi lengo kuu la Elimu katika uislamu (Edk form 1 Dhanaya Elimu)

Soma Zaidi...
KUAMINI MITUME WA ALLAH (S.W)

Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya Mitume wa Allah (s.

Soma Zaidi...
(c)Vipawa vya Mwanaadamu

Vipawa vya mwanaadamu ni sababu nyingine inayomfanya mwanaadamu asiweze kuishi bila ya kufuata dini moja au nyingine.

Soma Zaidi...
Mgawanyiko wa Elimu kwa mtazamo wa kikafiri

Kwa mtazamo wa kikafiri elimu imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Elimu ya dunia na Elimu ya akhera.

Soma Zaidi...