Navigation Menu



Zijuwe hatuwa za ukuwaji wa ujauzito na dalili za ujauzito katika miezi mitatu, miezi sita na miezi tisa

Zijuwe hatuwa za ukuwaji wa ujauzito na dalili za ujauzito katika miezi mitatu, miezi sita na miezi tisa



HATUA ZA UKUWAJI WA MIMBA NA DALILI ZAKE




Ujauzito umegawanyika katika hatua kuu tatu, au vipindi vikuu vitatu ambavyoni:-
1.trimester ya kwanza (first trimester)
Hiki ni kipindi katia ya wiki 1 mpaka 12 yaani ndani ya miezi mitatu ya kwanza. Kipindi hiki mjamzito awe makini sana kwani ni kipindi ambacho kutoka kwa ujauzito ni rahisi sana. Kipindi hiki ndicho ambacho mtoto anaanza kukuwa ubongo, uti wa mgongo na viungo vingine ama moyo na masikio. Tafiti zinaonyesha kuwa takribani asilimia 85 ya mimba zinazotoka huwa zinatoka katika kipindi hiki. Hata hivyo wanaotowa mimba pia hutoa katika kipindi hiki.



Mabadiliko ya mwili katika kipindi hiki
A.Uchovu
B.Kukosa haja kubwa
C.Kichefuchefu
D.Maumivu ya kichwa



Nini hakitakiwi kufanyika katika kipindi hiki?
A.Wacha kuvuta sigara
B.Wacha kunywa pombe
C.Wacha kutumia dawa kiholela bila ya ushauri wa daktari
D.Kuwa makini sana kwani kosaadogo ujauzito upo hatarini
E.Punguza kuchwa chai kupitiliza
F.Punguza kula samaki kwenye magobeta jaamii ya tondo




2.Trimester ya pili (second trimester)
Kipindi hiki ni kati ya wiki 13 mpaka 27 yaani kuanzia mwezi wa 3 mpaka wa 6 kwenda wa saba. Katika kipindi hiki mwanamke atafanyiwa vipimo vya utrasound kuangalia mkao wa mtoto na kama yupo katika afya njema. Katika kipindi hiki hata jinsia ya mtoto itaweza uonekana kwa ambaye anataka kuiona kwenye kipimo cha utrasound. Hapa mtoto anaweza kuishi nje ya mwili wa mama yake kuanzia wiki ya 23. na endapo mtoto atazaliwa hapa atakuwa njiti hivyo vifaa maalumu vitahitajika kumlea kabla ya kuanza kuishi huru. Katika kipindi hiki mama mjamzito atasikia vurugu za mtoto tumboni, kupiga mateke, kugeuka na nyinginezo.



Katika kipindi hiki karibia dalili zote za ujauzito za mwanzo hupotea. Nguvu itarudi vyema na utawza kulala usingizi mnono usiku. Katika kipindi hki tumbo litaanza kuonekana kukuwa. Katika kipindi hiki jiepushe sana yafuatayo:-
A.Kuvaa nguo za kubana
B.Kuwa na hasira mara kwamara. Yaani jitahidi kkutafuta furaha, kaa na maafiki cheka na furahia.
C.Usikibane tumbo hata likiwa kubwa vipi.



Katika kipindi hiki unawezakuhisi kuingulia mra kwa mara, na maumivu ya miguu. Hamu ya kula inawea kuongezeka, na uzito pia kuongezeka katika kipindi hiki. Katika kipindi hiki mwanamke anaweza kupatwa na maumivu ya mgongo. Hata hivyo anaweza kujihisi kama ana mafua ama pua zimeziba ila akifina hakuna kitu. Pia anaweza kuiona mishipa inatokeza kwa nje hasa kwenye miguu.



Katika kipindi hiki mama mjamzito ataanza kusikia mijongeo ya mtoto. Hata hivyo mtoto ataweza kuitambuwa sauti ya mama yake na watu wa karibu sana na mama yake. Baadhi ya viungo vinavyoweza kuonekana kwenye utrasound katika kipindi hiki ni kama figo, mapafu, moyo na ubongo na jinsia. Katika kipindi hiki mama mjamzito anaweza kupimwa kisukari cha mimba kuanzia wiki ya 26 mpaka 28.





3.Trimester ya tatu (third trimester)
Kipindi hiki huanzia wiki ya 28 mpaka 40, yaani kuanzia miezi 7 kwa makadirio. Katika kipindi hiki mara kwa mara utahitajika kumuona daktari kwa vipimo zaidi. Daktari atakuwa anakuangalia maendeleo yako kwa jumla na afya ya ujauzito wako. Atakuwa anakucheki:-
A.Anapima mkojo kuangalia protini
B.Atakuwa analkuangalia shinikizo la damu (presha)
C.Atasikiliza mapigo ya moyo wa mtoto
D.Atakuwa akipima njia ya uzaziatakuwa acheki miguu na mikono kama itakuwa inavimba.



Pia daktari anaweza kukupima uwepo wa bakteria wanaoitwa Group B streptococcus (GBS) kwenye uke. Uwepo wa bakteria hawa unaweza kuhatarisha afya ya mtoto anayezaliwa. Katika kipindi hiki ni vyema kuanza kufuatilia habari za kujifungua, mazoezi ya kujifungua na namna ya kujiandaa.



Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1608


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

mkewang alikuwa anasumbuliwa na tumbo kama siku tatu lika tuliya saivi analalamika kiuno na mgongo vina muuma nini tatizo tockt
Maumivu ya tumbo nakiuno kwa mwanamke yanahitaji uangalizi wakina. Kwani kuna sababu nyingi ambazo zinawezakuwa ni chanzo. Soma Zaidi...

Nini husababisha upungufu wa nguvu za kiume
Post hii itakujulidha mambo ambayo hupunguza nguvu za kiume Soma Zaidi...

Dalili za kupata uvimbe kwenye kizazi (fibroid)
Post hii inaenda kufundisha kuhusiana na uvimbe wa kizazi kwa wanawake. Uvimbe wa kizazi no uvimbe ambao hutokea kwenye tumbo la kizazi ambao unaweza kuwa ndan ya kizazi uvimbe huu ndan ya mwanamke hujulikana kama (uterine myoma au fibroid). Uvi Soma Zaidi...

Mimba iliyotungia nje, sababu zake na dalili zake. Nini kifanyike kuizuia?
Mimba hatari iliyotungia nje ya mji wa mimba, ni zipi dalili zake na ni kivipo mimba inatungia nje? Soma Zaidi...

Huduma kwa wanaopata hedhi zaidi ya mara moja kwa mwezi
Posti hii inahusu zaidi huduma kwa wanaoingia kwenye siku zao zaidi ya mara moja kwa mwezi. Soma Zaidi...

Utaratibu kwa wajawazito na wanaonyonshesha wakiwa na virusi vya ukimwi na ukimwi
Je kuna madhara kwa mwenye virusi vya ukimwi kunyonyesha ama kubeba mimba, na nini afyanye kama ameshabeba mimba ama kama ananyonyesha Soma Zaidi...

je maumivu ya nyonga na tumbo la chini ni dalili ya mimba?
Nina swali langu:-je maumivu ya nyonga na tumbo la chini ni dalili ya mimba? Soma Zaidi...

KUWAHI KUMALIZA TENDO LA NDOA MAPEMA: kumwaga mbegu mapema
Hii ni hali inayowapata sana wanaume huwa wanamaliza hamu ya tendo la ndoa mapema kabla ya mwenza kuridhika. Soma Zaidi...

Ni ili sababu ya kutokea kwa tezi dume
Tezidume ni moja ya magonjwa hayari yanayotokea katika mwili wa mwanaume.Hapa nimekuandalia sababu za kutokea kwa tezi dume. Soma Zaidi...

Ujue Ute kwenye uke
Post hii inahusu zaidi Ute ambao umo kwenye uke, Ute huu utofautiana kulingana na hali ya mama aliyonayo, kama mama ana mimba uke utakuwa tofauti na yule ambaye hana mimba au kama Ute una una magonjwa na hivyo utakuwa tofauti. Soma Zaidi...