Jinsi mimba inavyotungwa na namna ambavyo jinsia ya mtoto inavyotokea
Posti hii hasa inahusu kasoro ,utatuzi,na jinsi ya kutunga mimba kwa upande wa mwanamke na mwanaume .itatupelekea jinsi ya kuangalia kasoro na jinsi ya kutatua hizo kasoro katika jamii zetu.
KASORO KATIKA MFUMO WA UZAZI KWA MWANAUME
1.kutokana na hapo awali tunaongelea kuhusu kutatua kasoro katika mfumo wa uzazi kwa upende wa mwanaume na mwanamke kasoro zipo nyingi .ila tuanze na kasoro kwa upende wa mwanaume ambapo wanaume wengi upatwa na kasoro kadhaa katika mfumo wao moja ya kasoro ambayo uweza kuwapata wanaume ni ugumba .hii ni hali ya mwanaume kushindwa kutungisha mimba .
Ugumba kwa mwanaume hisababishwa na mambo mbalimbali ikiwemo kutoa mbegu ambazo zinakuwa chache sana hivo inapelekea kupunguza uwezekano kulifikia yai la mwanamke .kasoro nyingine ni kuwa na mbegu dhaifu ambazo zina upungufu kwa mfano kukosa mikia ,kuwa na mikia miwili ,kukosa kichwa au kuwa na umbo lisilo la kawaida yaani tunasema mbegu inakuwa haina umbo mahalamu kama mbegu zingine
Pia inapelekea kinga ya mwili inaweza kushambulia mbegu za kiume na hivyo kupunguza idadi yake vilevile kasoro nyingine korodani ya mwanaume hazitakuwa na uwezo wa kutengeneza mbegu za kiume kutokana na magonjwa au upungufu wa homoni .kasoro nyingine ya ugumba ni mirija ya kupitisha mbegu za kiume kuziba kutokana na magonjwa ya ngono kama ,vile kaswende na kisonono kwahiyo inashauriwa tusifanye ngono zembe bila kinga itatupelekea kupata matatizo ya ugumba .na kama utaona hizo kasoro ina bidi kufika kituo cha hospitali kabla ya tatizo kuwa kubwa.tumeweza kuona hio kasoro kwa upende wa mwanaume.
2. Kutokana na kasoro hizo hii ni kasoro katika upande wa uzazi wa mwanamke kama ilivyokuwa kwa mwanaume pia na mwanamke ana kasoro zake katika mfumo wake wa uzazi mojawapo ya kasoro ni ugumba kwa upande wake na tumeona mwanaume ana ugumba pia na mwanamke anaweza kuwa na ugumba unasababishwa na mambo mbalimbali ikiwemo mayai yake kushindwa kufanya kazi au kupevuka pia hali hii utokana matatizo ya utoaji wa homoni.
Matatizo hayo yanaweza kusababisha na tezi ya pituitari kushindwa kutoa homoni .vilevile,ovari kushindwa kutoa homoni ya oestrojeni au projesteroni ya kutosha .Adha ,ugumba unaweza kusababishwa na kuziba kwa mirija ya kupitisha mayai kutokana na magonjwa ya ngono kama vile kisonono,kaswende na pangusa .
Magonjwa haya yanaweza kufanya mirija iwe myembamba au iwe na makovu hivyo kuzuia yai lisiweze kupita .vilevile ugumba kwa wamama unaweza kusababiswa na uvimbe kwenye mji wa mimba ambapo hisababisha kiinitete kisiweze kujishikiza vizuri na hivyo usababisha matatizo ya mimba kutoka na hii shida ipo sana kwa wanawake kutokwa na mimba .
Utatuzi wa kasoro katika mfumo wa uzazi.
Kutokana na hayo matatizo au kasoro za mfumo wa uzazi kwa mwanaume na mwanamke matatizo hayo yote yanatibika kama mtu atawahi kwenda kituo cha afya kupata matibabu na ushauri nasaha kwa madaktari pia na kumsikiliza na kwenda kuyafanyia kazi.
JINSI YA KUTUNGA MIMBA. 1. Mwanaume na mwanamke wana huwezo wa kutunga mimba pale gameti za kike na za kiume kuungana au wengine wanasema ,zaigoti, wakati wa kujamiana mwanaume hutoa manii zenye gameti ume kutoka kwenye korodani kupitia mirija ya manii , urethra hadi uume .manii zenye gameti gameti ume huingia katika mwili wa mwanamke kupitia sehemu ya uke.mwanamke hutoa gameti uke kutoka kwenye ovari na kushuka kupitia mirija ya falopio.kama kama gameti ume zikiungana na gameti uke mimba utungwa .apo ndo jinsi mimba inatungwa kwa mwanaume na mwanamke pia apo apo tunaweza kupata watoto
Kuna njia za kupata au kutunga mimba ya pacha
1.hiii kwa jamii zingine zinaeleza kwamba ukipata pacha wawili nyie mnakuwa mna mikosi au mmeraniwa na mwenyezi mungu ambacho kitu sio cha ukweli kwahio inabidi jamii itambuwe kwamba watoto mapacha sio mikosi bali watoto mapacha wanapatikana pale.mwanamke anapojifungua mtoto mmoja kwa kila ujauzito .
Hata hivyo.mara chache mwanamke anaweza kujifungua wawili au zaidi kwa mpigo mmoja tu .mwanamke akijifungua watoto wawili au zaidi kwa ujauzito mmoja ,watoto hao huitwa pacha a aa. Pacha hao wanaweza kufanana au kutofanana.
Tuangalie kidogo apa jinsi ya mtoto kutokwa.Gameti uke kutoka kwenye ovari imebeba chembeuzi ya aina mmoja inayoitwa x hivyo,kila yai linalotoka tayari kwa kurutubishwa hubeba chembeuzi X.Gameti imebeba moja Kati ya chembeuzi za aina mbili yaani X au Y endapo chembeuzi X kutoka kwa mwanaume itakutana na chembe X kutoka kwa mwanamke.mtoto wa kike hutungwa .
Kama chembeucheuzi Y kutoka kwa mwanaume itakutana na chembe X kutoka kwa mwanamke .mtoto wa kiume hutungwa .hivyo basi anayehusika na upatikanaji wa jinsi ya mtoto ni mzazi wa kiume.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 ai web app 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Mbinu za kupunguza Kichefuchefu
Point hii inahusu zaidi mbinu za kupunguza Kichefuchefu hasa kwa wagonjwa na watumiaji wa madawa mbalimbali yanayoweza kusababisha kichefuchefu.
Soma Zaidi...Nna mimba ya miez miezi mitano 5 naruhusiwa kula papai kwa wing
Miongoni mwa matunda yenye virutubisho vingi ni pamoja na papai, nanasi, tikiti, palachichi, pera, karoti, hindi na boga. Lakini katika matunda haya yapo ambayo kwa mimba changa anatakiwa awe makini, kama papai na nanasi. Sasa vipi kuhusu mimba ya
Soma Zaidi...maumivu sehemu zinazoota mavuzi na kuwa namaumiv wakat wa haja ndogo na pia kwenye kichwa cha uume kunakua kama kunavimba
Je kupata maumivu sehemu zinazoota mavuzi na kuwa namaumiv wakat wa haja ndogo na pia kwenye kichwa cha uume kunakua kama kunavimb hizo syo dalili moja wapi?
Soma Zaidi...Kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa Ute wakati wa tendo la ndoa,ni Dalili ya kuwepo kwa kiwango kikubwa cha estrogen kwenye mwili ukilinganisha na homoni ya projestoren.
Soma Zaidi...Huduma kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi
Posti hii inahusu msaada kwa mwenye maumivu ya tumbo la hedhi, hizi ni huduma ambazo utolewa kwa wale wenye maumivu ya tumbo la hedhi.
Soma Zaidi...