zijuwe faida za kula njegere kiafya na umuhimu wa kula jegere pia jifunze njegere zina kazi gani mwilini?
Njegere ni katika mboga jamii ya kunde. Njegere ni katika mboga tamu kama hujawahi jaribu kuila, tafuta siku ujaribu. Lakini mboga hii ukiacha mbali na utamu wake njegere zimekuwa zikitajwa sana katika njanja za afya. Hivi unazijuwa faida za kula njegere?. hakika ni nyingi sana faida za njegere kiafya, kimwili na hata kwa utamu. Makala hii inakwenda kukuletea faida za kiafya za kula njegere.
Faida za kula njegere
1.Njegere zina virutubisho vingi sana ukilinganisha na mboga nyingi. Njegere zina vitamini A, vitamin K, Vitamini B na Vitamini C. pia njegere zina madini ya chuma, manganense, phosphorus, na folate. Pia negere zina protini na kamakamba. Katika mboga njegere ni katika mboka iliyokusanta protini kwa wingi sana.
2.Husaidia katika kudhibiti kiwango cha sukari mwilini. Yaani husaidia katika kudhibiti matumizi ya sukari ndani ya mwili wako. Husaidia kuwapa nafuu watu wenye isukari type 2 diabetes. Hali hii husaidia katika kuboresha afya ya moyo.
3.Njegere husaidia katika kuboresha afya ya mfumo wa mmengβenyo wa chakula. Kama unasumbuliwa na kukosa haja kubwa basi njegere ndio mtatuzi wako. Njegere husaidia katika kuondoa vimbe zilizopo kwenye njia ya chakula na kufanya choo kiwe kizito na rahisi kupita kwa urahisi. Njegere husaidia katika kuzuia saratani ya utumbo mkubwa na kusaidia katika kuondosha chakula chote kupitia haja.
4.Njegere huliunda mwili dhidi ya maradhi hatari kama saratani, maradhi ya moyo na kisukari. Kwa sifa hii njegere ni mboga pekee ambayo unatakiwa uile mara nyingi sana kwa lengo la kujikinga na maradhi haya. Hata hivyo kwa ambaye ni mgonjwa tayari mboga hii itamsaidia kupunguza uzito wa tatizo.
A.Husaidia kuzuia maradhi ya moyo: njegere zina madini ya magnesium, potassium na calcium. Ulaji wa chakula chenye madini haya kwa wingi husaidia katika kuzuia shinikizo la juu la damu (presha ya kupanda) ambayo ndio chanzo kikuu cha maradhi ya moyo. Pia ndani ya njegere kula flavonols, carotenoids na vitamini C. wa pamoja husaidia katika kupunguza uwezekano wa kupata maradhi ya moyo kwa sababu huzuia uharibifu wa seli.
B.Husaidia kuzuia saratani: njegere zina uwezo wa kuzuia uotaji wa vimbe ndani ya mwili ambazo ndio mizizi ya saratani. Pia ndani ya njegere kuna saponin nichembechembe inayojulikana kama kipingamizi cha saratani. Hata hivyo vitamini K ndani ya njegere vinatambulika vyema kuwa na msaada mkubwa katika kuzuia aina mbalimbali za saratani.
C.Nyuzinyuzi na protini katika njegere husaidia sana katika kudhibiti kiwango cha sukari kwenye damu, na matumizi ya sukari mwilini.pia vitamini B, K, A, C na madini ndani ya ngegere husaidi katika kulinda mwili dhidi ya kisukari.
5.Njegere husaidia katika kuboresha afya ya mifupa.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu umuhimu wa kitunguu maji mwilini
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kutumia maembe kiafya, tunajua wazi kuwa maembe ni tunda ambalo lina umuhimu kwenye afya na uwa na vitamini C kwa hiyo tunapaswa kujua faida zake kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Makala hii inakwenda kukueleza faida za kula maboga, na mbegu zake kwa afya yako
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi kazi ya majani ya mstafeli dhidi ya bakteria na fangasi, pamoja na kutibu saratani mbalimbali na upambana na fangasi na bakteria kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza maana ya Vitamini C, mwaka vilipogunduliwa na aliyegundua vitamini C
Soma Zaidi...vitamini B vipo katika makundi mengi kma aB1, B2, B3, B5, B6, B7 na B12. Makala hii itakwenda kukutajia kazi kuu za Vitamini B katika miili yetu
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi virutubisho vya mwili, ni aina tano za vyakula ambayo ufanya kazi mbalimbali kwenye sehemu za mwili wa binadamu.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi virutubisho vilivyomo kwenye parachichi, tunajua sana kuwa parachichi ina virutubisho vingi ambavyo vinaweza kuleta faida nyingi kwenye mwili kama yalivyo matunda na vyakula vingine.
Soma Zaidi...