Mambo ya kuangalia kwa mtu aliyepoteza fahamu
Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuangalia kwa mtu aliyepoteza fahamu, kama mtu amepoteza fahamu Kuna mambo muhimu yanapaswa kuangaliwa kwa makini kama ifuayavyo.
Mambo ya kuangalia kwa aliyepoteza fahamu.
1. Kwanza kuangalia kama mgonjwa anapumua.
Kitu Cha kwanza kuangalia kama mtu amepoteza fahamu ni kuangalia kama mgonjwa anapumua, kama hapumui unaangalia mdomoni kama Kuna kitu labda kimeziba mdomoni pia angalia puani labda Kuna michanga imeziba hasa kwa waliopata ajali, ukikuta Kuna kitu chochote unapaswa kukitoa Ila uwe mwangalifu unapotoa vitu mdomoni usije ukavisukuma kwenye mfumo wa hewa, kwa hiyo hakikisha mgonjwa wako anapumua ndipo uendelee na mambo mengine.
2. Kuangalia kiwango Cha damu kinachotoka , kwa hiyo mgonjwa kama anatokwa na damu nyingi zinapaswa kuzuia kwa kufunga sehemu ambapo damu zinatokea, kama damu zinaendelea kutoka mgonjwa anapaswa kumpelekwa hospitalini haraka ipasavyo Ili kuongeza kiwango Cha damu. Kama ni kidogo mgonjwa anaweza akafungwa na huduma nyingine zinaweza kuendelea.
3. Kuangalia chanzo Cha kupoteza fahamu.
Baada ya kufanya hayo yote tunapaswa kujua chanzo Cha kupoteza fahamu ni nini? Kama ni mshutuko wa Moyo au kama ni kushuka kwa sukari au kama ni tatizo la moyo na mambo mengine ambayo usababisha kupoteza fahamu, ukisha tambua chanzo Cha kupoteza fahamu unaanzia kutibu kadri ya chanzo, mfano kama ni kushuka kwa sukari mpe mgonjwa vitu vya sukari au kama ni kuishiwa maji mwilini mgonjwa anapaswa kuongezewa maji na mengineyo.
4. Kama unaona hali ya mgonjwa haiwezekani kutibiwa kwa kutumia huduma ya kwanza mpeleke mgonjwa haraka sana hospitalini Ili aweze kupatiwa matibabu zaidi.kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa ugonjwa wa kupoteza fahamu upo na sababu nyingine zinaweza kutibiwa kwa kutumia huduma ya kwanza lakini hali ya mgonjwa isipobadilika mgonjwa anapaswa kumpelekwa hospitalini haraka Ili apatiwe matibabu zaidi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 web hosting 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Visababishi vya magonjwa.
Posti huu inahusu zaidi visababishi mbalimbali vya magonjwa, tunajua wazi kuwa ugonjwa ni hali ya kutokuwa kawaida kwa ogani mbalimbali kwenye mwili na kusababisha mwili kushindwa kufanya kazi zake vizuri.
Soma Zaidi...Vyakula vya kuongeza nguvu za kiume
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya vyakula vinavyoongeza nguvu za kiume
Soma Zaidi...Huwezi kuambukizwa Ukimwi kwa mambo yafuatayo
Posti hii inahusu zaidi au inapinga Imani potofu ambayo utokea kwenye jamii kwamba unaweza kuambukizwa Ukimwi kwa vitu ambavyo haviusiani na namna mtu anavyoweza kuambukizwa Ukimwi,Ila mapendekezo kuwa watu wanapaswa kujua kuwa huwezi kuambukizwa Ukimwi k
Soma Zaidi...Sababu za kumsafisha mgonjwa kinywa
Posti hii inahusu zaidi sababu za kumsafisha mgonjwa kinywa, Mgonjwa akiwa anaumwa na pia anakula chakula ni lazima asafishwe kinywa Ili kuweza kuepuka madhara mengine yanayoweza kujitokeza kwa sababu ya kuwepo kwa uchafu kinywani.
Soma Zaidi...Ijue rangi za mkojo na maana zake katika mwili kuhsu afya yako
Posti hii inahusu zaidi rangi za mkojo na maana zake, hizi ni rangi ambazo uweza kutokea kwenye mkojo wa mtu mmoja na mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa magonjwa, chakula,na mtindo wa maisha inawezekana unywaji wa maji au kutokunywa maji.
Soma Zaidi...Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa walioingiliwa na uchafu puani.(foreign body).
Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa mgonjwa alieye ingiwa na uchafu puani (foreign body)
Soma Zaidi...