Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuangalia kwa mtu aliyepoteza fahamu, kama mtu amepoteza fahamu Kuna mambo muhimu yanapaswa kuangaliwa kwa makini kama ifuayavyo.
Mambo ya kuangalia kwa aliyepoteza fahamu.
1. Kwanza kuangalia kama mgonjwa anapumua.
Kitu Cha kwanza kuangalia kama mtu amepoteza fahamu ni kuangalia kama mgonjwa anapumua, kama hapumui unaangalia mdomoni kama Kuna kitu labda kimeziba mdomoni pia angalia puani labda Kuna michanga imeziba hasa kwa waliopata ajali, ukikuta Kuna kitu chochote unapaswa kukitoa Ila uwe mwangalifu unapotoa vitu mdomoni usije ukavisukuma kwenye mfumo wa hewa, kwa hiyo hakikisha mgonjwa wako anapumua ndipo uendelee na mambo mengine.
2. Kuangalia kiwango Cha damu kinachotoka , kwa hiyo mgonjwa kama anatokwa na damu nyingi zinapaswa kuzuia kwa kufunga sehemu ambapo damu zinatokea, kama damu zinaendelea kutoka mgonjwa anapaswa kumpelekwa hospitalini haraka ipasavyo Ili kuongeza kiwango Cha damu. Kama ni kidogo mgonjwa anaweza akafungwa na huduma nyingine zinaweza kuendelea.
3. Kuangalia chanzo Cha kupoteza fahamu.
Baada ya kufanya hayo yote tunapaswa kujua chanzo Cha kupoteza fahamu ni nini? Kama ni mshutuko wa Moyo au kama ni kushuka kwa sukari au kama ni tatizo la moyo na mambo mengine ambayo usababisha kupoteza fahamu, ukisha tambua chanzo Cha kupoteza fahamu unaanzia kutibu kadri ya chanzo, mfano kama ni kushuka kwa sukari mpe mgonjwa vitu vya sukari au kama ni kuishiwa maji mwilini mgonjwa anapaswa kuongezewa maji na mengineyo.
4. Kama unaona hali ya mgonjwa haiwezekani kutibiwa kwa kutumia huduma ya kwanza mpeleke mgonjwa haraka sana hospitalini Ili aweze kupatiwa matibabu zaidi.kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa ugonjwa wa kupoteza fahamu upo na sababu nyingine zinaweza kutibiwa kwa kutumia huduma ya kwanza lakini hali ya mgonjwa isipobadilika mgonjwa anapaswa kumpelekwa hospitalini haraka Ili apatiwe matibabu zaidi.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Posti hii inahusu zaidi matokeo ya maambukizi kwenye milija na ovari, ni matokeo apatayo mtu mwenye maambukizi kwenye milija na ovari.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu kushiriki-ngono-na-mtu-aliye-na-vvu-na-ukimwi
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya vyakula vinavyoongeza nguvu za kiume
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi hatua za kufuata unapohisi umeambukizwa na virus vya ukimwi. Kwa sababu watu wengi wanakuwa na kiwewe anapohisi ameambukizwa na virus vya ukimwi kwa hiyo wanapaswa kufanya yafuatayo.
Soma Zaidi...Unapokuwa na kizunguzungu unashindwa kuudhibiti mwili wako, unaweza kuanguka kabisa.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kumwosha Mgonjwa mwili mzima,ni sababu ambazo umsaidie mgonjwa ili aweze kupata nafuu mapema na kumsaidia kama tutakavyoona hapo chini
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa aliyeungua
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu Mambo yanayopunguza nguvu za kiume
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na kwikwi
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea kuhusiana na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kqa mgonjwa aliyeingiliwa na kitu au uchafu kwenye sikio.
Soma Zaidi...