Mambo ya kuangalia kwa mtu aliyepoteza fahamu
Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuangalia kwa mtu aliyepoteza fahamu, kama mtu amepoteza fahamu Kuna mambo muhimu yanapaswa kuangaliwa kwa makini kama ifuayavyo.
Mambo ya kuangalia kwa aliyepoteza fahamu.
1. Kwanza kuangalia kama mgonjwa anapumua.
Kitu Cha kwanza kuangalia kama mtu amepoteza fahamu ni kuangalia kama mgonjwa anapumua, kama hapumui unaangalia mdomoni kama Kuna kitu labda kimeziba mdomoni pia angalia puani labda Kuna michanga imeziba hasa kwa waliopata ajali, ukikuta Kuna kitu chochote unapaswa kukitoa Ila uwe mwangalifu unapotoa vitu mdomoni usije ukavisukuma kwenye mfumo wa hewa, kwa hiyo hakikisha mgonjwa wako anapumua ndipo uendelee na mambo mengine.
2. Kuangalia kiwango Cha damu kinachotoka , kwa hiyo mgonjwa kama anatokwa na damu nyingi zinapaswa kuzuia kwa kufunga sehemu ambapo damu zinatokea, kama damu zinaendelea kutoka mgonjwa anapaswa kumpelekwa hospitalini haraka ipasavyo Ili kuongeza kiwango Cha damu. Kama ni kidogo mgonjwa anaweza akafungwa na huduma nyingine zinaweza kuendelea.
3. Kuangalia chanzo Cha kupoteza fahamu.
Baada ya kufanya hayo yote tunapaswa kujua chanzo Cha kupoteza fahamu ni nini? Kama ni mshutuko wa Moyo au kama ni kushuka kwa sukari au kama ni tatizo la moyo na mambo mengine ambayo usababisha kupoteza fahamu, ukisha tambua chanzo Cha kupoteza fahamu unaanzia kutibu kadri ya chanzo, mfano kama ni kushuka kwa sukari mpe mgonjwa vitu vya sukari au kama ni kuishiwa maji mwilini mgonjwa anapaswa kuongezewa maji na mengineyo.
4. Kama unaona hali ya mgonjwa haiwezekani kutibiwa kwa kutumia huduma ya kwanza mpeleke mgonjwa haraka sana hospitalini Ili aweze kupatiwa matibabu zaidi.kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa ugonjwa wa kupoteza fahamu upo na sababu nyingine zinaweza kutibiwa kwa kutumia huduma ya kwanza lakini hali ya mgonjwa isipobadilika mgonjwa anapaswa kumpelekwa hospitalini haraka Ili apatiwe matibabu zaidi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Namna ya kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha mwenyewe ni
Posti hii inahusu njia za kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha wenyewe, hali hii uwa inawapata wagonjwa wale ambao hawawezi kujilisha wenyewe tunaweza kuwalisha kwa njia zifuatazo.
Soma Zaidi...Namna ya kumfanyia usafi Mgonjwa kwa mwili mzima.
Posti hii inahusu namna ya kumfanyia mgonjwa usafi mwili mzima, ni njia ambazo utumika kumfanyia mgonjwa usafi mwili mzima au kumwosha Mgonjwa hasa wale walio mahututi na hawawezi kuamka kitandani.
Soma Zaidi...Fahamu kuhsu vitamini E na kazi zake mwilini
Je unazijuwa faida za kuwa na vitamini E mwilini mwako.Unahani utapata matatizo yapi ya kiafya endapo utakuwa na upungufu wa vitamini E mwilini? Makala hii ni kwa ajili yako.
Soma Zaidi...Njia za kukabiliana na presha ya kushuka
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na presha ya kushuka
Soma Zaidi...Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na shambulio la moyo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na shambulio la moyo
Soma Zaidi...Madhara ya kuchelewa kutibu tatizo la kiafya
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea endapo tatizo halijatibiwa.
Soma Zaidi...