Namna ya kumsaidia mtoto mwenye degedege
Degedege ni ugonjwa unaoshambulia sana watoto chini ya miaka mitano,na uwaletea matatizo mengi pamoja na kuwepo kwa ulemavu na vifo vingi vinavyosababishwa na ugonjwa huu.
Zifuatazo ni njia za kumsaidia mtoto kama amepatwa na degedege,
1. Mlaze mtoto kwenye sehemu ambayo itazuia kungata ulimi, kwa sababu mtoto akiachwa na degedege atasikia maumivu kwenye ulimi na anaweza kushindwa kunyonya au kula
2. Kama Kuna makohozi yoyote yanayombana kifuani au kohoni inabidi yatolewe kwa sababu yanaweza kuingia kwenye mfumo wa hewa na kuleta matatizo mengine
3.mpatie mtoto dawa ambazo zinahitajika kwa ajili ya kuzuia degedege, dawa hizi ziwe zimeagizwa na daktari hizo dawa zipo hospitalini na uponyesha ugonjwa huu.
4. Hakikisha kwamba kiasi Cha sukari kwenye mwili ni Cha kawaida, kama sukari haiko kwenye kiwango chake jaribu kufanya iwe kwenye kiwango na pia angalia kiasi Cha madini kwenye mwili
5. Angalia kama joto la mwili liko kawaida, kama haliko kawaida mpatie dawa za kushusha joto la mwili, angalia pia msukumo wa damu, pia upumuaji,mapigo ya moyo yanaendaje, hakikisha kila kitu kwenye mwili Kiko kawaida
6. Hakikisha mtoto Yuko sehemu nzuri ambayo hawezi kuanguka na hakikisha mtoto anaangaliwa mda wote Ili kuepuka madhara mbalimbali yanayoweza kutokea wakati anahudumiwa
7. Endelea kuangalia chanzo Cha degedege kama ni maambukizi kutokana na magonjwa nyemelezi au ni bakteria au ni virusi, kama ni ugonjwa wowote inabidi kutibiwa mara Moja.
Angalisho kama mtoto bado ana degedege usimpe kitu chochote Cha kula kwa kupitia mdomoni maana chakula kinaweza kuingia kwenye mfumo wa hewa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Mem mtoto ang almeza sumu yapanya ila tulimpa maziwa kwan inaweza leta madhara kwabaadae mana atukumpeleka hosptal
Maziwa ni mojakati ya vinywaji ambavyo ni dawa na hutumikakutoa huduma ya kwanza pale mtu anapomeza ama kula sumu. Huduma ya kwanza hii inaweza kuokoa maisha na wakati mwingine inaweza kuwa ndio dawa kabisa wala hakuna haja ya kufika Kituo cha afya.
Soma Zaidi...Sababu za kumwosha Mgonjwa mwili mzima.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kumwosha Mgonjwa mwili mzima,ni sababu ambazo umsaidie mgonjwa ili aweze kupata nafuu mapema na kumsaidia kama tutakavyoona hapo chini
Soma Zaidi...Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa walioingiliwa na uchafu puani.(foreign body).
Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa mgonjwa alieye ingiwa na uchafu puani (foreign body)
Soma Zaidi...Huduma ya kwanza kwa mwenye jeraha linalotoa damu
Posti inahusu huduma ya kwanza kwa mwenye jeraha linalotoa damu.huduma ya kwanza Ni kumsaidia mtu alie pata jeraha au ajali kabla hajamwona dactari au kufika hospitalinia.
Soma Zaidi...Njia za kupunguza uzito na kitambi
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kupunguza tatizo la kuwepo kwa uzito mkubwa pamoja na kitambi
Soma Zaidi...Njia ambazo maradhi huambukizwa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo maradhi huambukizwa
Soma Zaidi...