Posti hii inahusu zaidi huduma ya kwanza ya mgonjwa mwenye jeraha la kawaida kwenye ubongo, ni Tiba ambayo utolewa kulingana na dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo kama ifuayavyo.
Tiba ya mgonjwa wa jeraha la kawaida kwenye ubongo
1.Kuangalia kama Kuna sehemu yoyote ambayo mgonjwa ameumia kwa sehemu ya nje inayoonekana Moja kwa Moja kwa macho kama Kuna damu ambayo inatoka,au kama Kuna kidonda kinachoonekana au kama Kuna kitu chochote ambacho kimejishikisha kwenye sehemu yoyote ya kichwa, kama vipo jaribu kuviondoa na kama Kuna kutokwa na damu jaribu kuzuia damu isitoke kwa kufanya hivyo unapunguza maumivu kwa mgonjwa.
2.Kumpatia mgonjwa mda wa kupumzika.
Mgonjwa anapaswa kupumzika Ili aweze kurudisha mfumo wa ubongo kwenye nafasi yake au kwenye kazi yake ya kawaida kwa mfano mgonjwa wa jeraha la kawaida kwenye ubongo utapika, uona kizunguzungu, uhisi kichefuchefu,kuona kwa shida au maruweruwe hayo yote utokea kwa sababu ya mshutuko kwenye ubongo kwa hiyo mgonjwa akipata mda wa kutosha wa kupumzika anarudisha kila kitu kwenye hali ya kawaida. Kwa hiyo wahudumu wanapaswa kujulishwa hilo Ili kumpa mgonjwa mda wa kupumzika.
3. Mgonjwa anapaswa kupewa dawa za kupunguza maumivu.
Kwa sababu ya maumivu kwenye kichwa na sehemu mbalimbali za mwili mgonjwa anapaswa kupewa dawa ya maumivu , lakini sio kila dawa za maumivu zinafaa kwa mtu Mwenye jeraha la kawaida kwenye ubongo kwa Sababu nyingine nyingine zinasababisha uvujaji wa damu kuongezeka kama vile Asprini na Ibuprofen mgonjwa hapaswi kuzitumia lla Panadol au paracetamol ni nzuri, kwa hiyo wahudumu wa afya wanapaswa kujua hilo.
4.Mwamshe mgonjwa mara kwa mara na mwoji maswali Ili kuona kama amerudisha fahamu.
Mgonjwa anapaswa kuamshwa na kuulizwa maswali kama vile uko wapi?, Unaumwa wapi?, Unataka nini?, Unaumia wapi? Kwa kufanya hivyo unaweza kuona tatizo la Mgonjwa liko wapi kwa sababu wakati mwingine mgonjwa aliyepoteza fahamu huwa tunamhudumia tunavyojisikia na pengine huwa tunaongeza maumivu bila kujua Ila kwa kumuuliza mgonjwa unaweza kupata njia ya kumlaza au kumgeuza. Kwa hiyo ni vizuri kumwuliza mgonjwa Ili upatiwe urahisi wa kumhudumia.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Post hii inahusu zaidi umuhimu wa mate mdomoni, mate ni majimaji ambayo hukaa mdomoni na husaidia katika kazi mbalimbali mdomoni.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa mifupa mwilini, mifupa ni mojawapo ya tushy zilizounganika na ufanya kazi kubwa kwenye mwili.
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa fizi ambapo fizi huweza kuwa na maumivu, kuambukizwa, kuvuja damu kwenye fizi na Vidonda.
Soma Zaidi...Dalili za mimba zinaweza kuwa tata sana kuzijua mpaka upate vipimo. Kwa mfano unaweza kupatwa na maumivu yakibofu. Je unadhani nayo ni dalili ya mimba?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi viwango vitatu vya kuungua. Ili tuweze kujua mtu ameunguaje Kuna viwango vitatu vya kujua kiasi na namna mtu alivyoungua
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa watoto
Soma Zaidi...Posti hii inahusu njia na namna ya kumhudumia aliyeingiwa na nyoka. Nyoka ni kiumbe ambacho Kina sumu kali na mtu akifinywa na nyoka asipohudumiwa anaweza kupata ulemavu au kupoteza maisha
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa wazee
Soma Zaidi...Posti huu inahusu zaidi visababishi mbalimbali vya magonjwa, tunajua wazi kuwa ugonjwa ni hali ya kutokuwa kawaida kwa ogani mbalimbali kwenye mwili na kusababisha mwili kushindwa kufanya kazi zake vizuri.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kutumia dawa za kujikinga na maambukizi ya ukimwi, ni faida ambazo upatikana kwa watu wanaodhani wameambukizwa na virus vya ukimwi na kuweza kujikinga.
Soma Zaidi...