Huduma ya kanza kwa mgonjwa mwenye jeraha la kawaida kwenye ubongo

Huduma ya kanza kwa mgonjwa mwenye jeraha la kawaida kwenye ubongo

Posti hii inahusu zaidi huduma ya kwanza ya mgonjwa mwenye jeraha la kawaida kwenye ubongo, ni Tiba ambayo utolewa kulingana na dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo kama ifuayavyo.

Tiba ya mgonjwa wa jeraha la kawaida kwenye ubongo

1.Kuangalia kama Kuna sehemu yoyote ambayo mgonjwa ameumia kwa sehemu ya nje inayoonekana Moja kwa Moja kwa macho kama Kuna damu  ambayo inatoka,au kama Kuna kidonda kinachoonekana au kama Kuna kitu chochote ambacho kimejishikisha kwenye sehemu yoyote ya kichwa, kama vipo jaribu kuviondoa na kama Kuna kutokwa na damu jaribu kuzuia damu isitoke kwa kufanya hivyo unapunguza maumivu kwa mgonjwa.

 

2.Kumpatia mgonjwa mda wa kupumzika.

Mgonjwa anapaswa kupumzika Ili aweze kurudisha mfumo wa ubongo kwenye nafasi yake au kwenye kazi yake ya kawaida kwa mfano mgonjwa wa jeraha la kawaida kwenye ubongo utapika, uona kizunguzungu, uhisi kichefuchefu,kuona kwa shida au maruweruwe hayo yote utokea kwa sababu ya mshutuko kwenye ubongo kwa hiyo mgonjwa akipata mda wa kutosha wa kupumzika anarudisha kila kitu kwenye hali ya kawaida. Kwa hiyo wahudumu wanapaswa kujulishwa hilo Ili kumpa mgonjwa mda wa kupumzika.

 

3. Mgonjwa anapaswa kupewa dawa za kupunguza maumivu.

Kwa sababu ya maumivu kwenye kichwa na sehemu mbalimbali za mwili mgonjwa anapaswa kupewa dawa ya maumivu , lakini sio kila dawa za maumivu zinafaa kwa mtu Mwenye jeraha la kawaida kwenye ubongo kwa Sababu nyingine nyingine zinasababisha uvujaji wa damu kuongezeka kama vile Asprini na Ibuprofen mgonjwa hapaswi kuzitumia lla Panadol au paracetamol ni nzuri, kwa hiyo wahudumu wa afya wanapaswa kujua hilo.

 

4.Mwamshe mgonjwa mara kwa mara na mwoji maswali Ili kuona kama amerudisha fahamu.

Mgonjwa anapaswa kuamshwa na kuulizwa maswali kama vile uko wapi?, Unaumwa wapi?, Unataka nini?, Unaumia wapi? Kwa kufanya hivyo unaweza kuona tatizo la Mgonjwa liko wapi kwa sababu wakati mwingine mgonjwa aliyepoteza fahamu huwa tunamhudumia tunavyojisikia na pengine huwa tunaongeza maumivu bila kujua Ila kwa kumuuliza mgonjwa unaweza kupata njia ya kumlaza au kumgeuza. Kwa hiyo ni vizuri kumwuliza mgonjwa Ili upatiwe urahisi wa kumhudumia.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views: 1531

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 web hosting     👉3 ai web app     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Haya hayawezi kuambukiza UKIMWI

Somo hili linakwenda kukuletea mambo ambayo hayawezi kuambukiza UKIMWI

Soma Zaidi...
Maana ya afya

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maana ya afya

Soma Zaidi...
Huwezi kuambukizwa Ukimwi kwa mambo yafuatayo

Posti hii inahusu zaidi au inapinga Imani potofu ambayo utokea kwenye jamii kwamba unaweza kuambukizwa Ukimwi kwa vitu ambavyo haviusiani na namna mtu anavyoweza kuambukizwa Ukimwi,Ila mapendekezo kuwa watu wanapaswa kujua kuwa huwezi kuambukizwa Ukimwi k

Soma Zaidi...
Huduma kwa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi

Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo wagonjwa wanaoishi na maambukizi ya virus vya ukimwi wanaweza kupata, huduma hii utolewa hasa kwa wale ambao wamejitokeza kupima afya zao na kujua wazi hali zao na kwa wale wanaofatilia huduma hii wanaweza kuishi vizu

Soma Zaidi...
Huduma ya kwanza kwa mgonjwa aliyepata ajali ya kichwa

Ajali ya kichwa na ajali inayotolewa kwenye sehemu mbalimbali za kichwa, ambavyo husababishwa madhara kwa aliyepata ajali hiyo

Soma Zaidi...
Maumivu ya kifua yanayosababishwa na kupungua kwa mtiririko wa Damu kwenye moyo.

 Maumivu ya kifua yanayosababishwa na kupungua kwa mtiririko wa damu kwenye misuli ya moyo, kitaalamu huitwa Angina ni dalili ya Ugonjwa wa ateri ya Coronary. Ugonjwa huu kawaida hufafanuliwa kama kufinya, shinikizo, uzito, kubana au maumivu kwenye

Soma Zaidi...