picha

Huduma ya kanza kwa mgonjwa mwenye jeraha la kawaida kwenye ubongo

Posti hii inahusu zaidi huduma ya kwanza ya mgonjwa mwenye jeraha la kawaida kwenye ubongo, ni Tiba ambayo utolewa kulingana na dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo kama ifuayavyo.

Tiba ya mgonjwa wa jeraha la kawaida kwenye ubongo

1.Kuangalia kama Kuna sehemu yoyote ambayo mgonjwa ameumia kwa sehemu ya nje inayoonekana Moja kwa Moja kwa macho kama Kuna damu  ambayo inatoka,au kama Kuna kidonda kinachoonekana au kama Kuna kitu chochote ambacho kimejishikisha kwenye sehemu yoyote ya kichwa, kama vipo jaribu kuviondoa na kama Kuna kutokwa na damu jaribu kuzuia damu isitoke kwa kufanya hivyo unapunguza maumivu kwa mgonjwa.

 

2.Kumpatia mgonjwa mda wa kupumzika.

Mgonjwa anapaswa kupumzika Ili aweze kurudisha mfumo wa ubongo kwenye nafasi yake au kwenye kazi yake ya kawaida kwa mfano mgonjwa wa jeraha la kawaida kwenye ubongo utapika, uona kizunguzungu, uhisi kichefuchefu,kuona kwa shida au maruweruwe hayo yote utokea kwa sababu ya mshutuko kwenye ubongo kwa hiyo mgonjwa akipata mda wa kutosha wa kupumzika anarudisha kila kitu kwenye hali ya kawaida. Kwa hiyo wahudumu wanapaswa kujulishwa hilo Ili kumpa mgonjwa mda wa kupumzika.

 

3. Mgonjwa anapaswa kupewa dawa za kupunguza maumivu.

Kwa sababu ya maumivu kwenye kichwa na sehemu mbalimbali za mwili mgonjwa anapaswa kupewa dawa ya maumivu , lakini sio kila dawa za maumivu zinafaa kwa mtu Mwenye jeraha la kawaida kwenye ubongo kwa Sababu nyingine nyingine zinasababisha uvujaji wa damu kuongezeka kama vile Asprini na Ibuprofen mgonjwa hapaswi kuzitumia lla Panadol au paracetamol ni nzuri, kwa hiyo wahudumu wa afya wanapaswa kujua hilo.

 

4.Mwamshe mgonjwa mara kwa mara na mwoji maswali Ili kuona kama amerudisha fahamu.

Mgonjwa anapaswa kuamshwa na kuulizwa maswali kama vile uko wapi?, Unaumwa wapi?, Unataka nini?, Unaumia wapi? Kwa kufanya hivyo unaweza kuona tatizo la Mgonjwa liko wapi kwa sababu wakati mwingine mgonjwa aliyepoteza fahamu huwa tunamhudumia tunavyojisikia na pengine huwa tunaongeza maumivu bila kujua Ila kwa kumuuliza mgonjwa unaweza kupata njia ya kumlaza au kumgeuza. Kwa hiyo ni vizuri kumwuliza mgonjwa Ili upatiwe urahisi wa kumhudumia.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 1203

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 ai web app     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Mfuno wa damu na makundi manne ya damu na asili yake nani anayepasa kutoa damu?

Posti hii inakwenda kukujuza kuhusu makundi manne ya damu, asili yake, maana ya antijeni na antibody, pia utajifunza kuhusu mfumo wa Rh. Mwisho utajifunza watu wanaopasa kutoa damu.

Soma Zaidi...
Zijue faida za mate mdomoni

Post hii inahusu zaidi umuhimu wa mate mdomoni, mate ni majimaji ambayo hukaa mdomoni na husaidia katika kazi mbalimbali mdomoni.

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa mtu aloanguka kifafa

Somo hili linakwenda kukueleza jinsi ya kumfanyia huduma ya Kwanza kwa mtu aloanguka kifafa

Soma Zaidi...
Jinsi moyo unavyosukuma damu

Post hii inahusu zaidi jinsi moyo unavyosukuma damu, moyo ni ogani ambayo usukuma damu kwenye sehemu mbalimbali za mwili.

Soma Zaidi...
Mbinu za kuondoa sumu mwilini.

Posti hii inahusu zaidi mbinu za kuondoa sumu mwilini, ni njia mbalimbali ambazo uweza kutumika ili kuondoa sumu mwilini.

Soma Zaidi...
Malengo ya kutibu ukoma

Posti hii inahusu zaidi malengo ya kutibu ukoma, ni malengo ambayo yamewekwa na wizara ya afya ili kuweza kutokomeza ukoma kwenye jamii

Soma Zaidi...