picha

Utaratibu wa lishe kwa watoto

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa watoto

?

6. UTARATIBU WA LISHE KWA WATOTOKila mtu anatkiwa ale chakula kwa kulingana na mahitaji ya mwili wake. Motto anatakiwa ale vyakula maalumu kwa ajili ya kumuwezesha kukuwa vizuri umbo na kiakili. Halikadhalika mama wajawazito wanatakiwa wale vyakula maalumu kwa ajili ya kuwezesha afya ya mama na motto. Wazee, vijana, wafanyakazi na wagojwa wanatakiwa wale vyakula kulingana na hali zao. Hapa tutakuletea lishe kwa kulingana na makundi ya watu.Watoto wanatakiwa kula vyakula vya protinikwa wingi ili kuwezesha ukuaji wao wa mwili na tishu. Upungufu wa protini unaweza kumpelekea mtoto awe na ukuaji hafifu. Kwa ukuaji mzuri wa meno na mifupa mtoto anatakiwa apewe vyakula vya madini kama madini ya kashian(calcium) upungufu wa madini haya huenda mtoto akawa na ukuaji mbaya wa mifupa. Madini ya zink ni muhimu pia katika ukuaji wa mtoto.Vitamini B12 ni muhimu kwa ajili ya kuhakikisha utengenezwaji wa seli nyekundu za ndamu. Pia ijulikane kuwa ukuaji mzuri wa mtoto unategemea kuwepo na damu ya kutosha mwilini ili kuweza kusafirisha gesi ya oxygeni pamoja na viinilishe(nutrients) ndani ya mwili.Vitamini ni muhimu sana katika ukuaji wa mtoto. Watoto wapewe vyakula vyenye vitamini C kwa wingi kama machungwa, mapapai. Vitamini hivi vinamuwezesha mtoto kutengeneza kinga ya mwili ili kuweza kupamabana na maradhi. Watoto pia wanatakiwa wapewe vyakula vya wanga kwa wingi ili waweze kupata nguvu ya kutosha kuweza kufanya shughuli zao kama mazoezi ya kutambaa, kukumbia, kusimama n.k.

?

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 1508

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 ai web app     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Kwanini mbu hawezi kuambukiza ukimwi

Somo Hili linakwenda kukueleza sababu za kwanini mbu hawezi kuambukiza ukimwi

Soma Zaidi...
Namna ya kuchoma chanjo

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuchoma chanjo, ni njia ambazo utumika kutoa chanjo kwa watoto na watu wazima kwa utaratibu uliowekwa.

Soma Zaidi...
Zijue dalili za upungufu wa maji mwilini

Posti hii inaelezea kuhusiana na upungufu wa maji mwilini

Soma Zaidi...
Je, utamsaidia vipi mtu aliyeumwa na nyuki?

Posti hii inazungumzia kuhusiana na kumsaidia mwenye aliyeumwa na nyuki.nyuki na wadudu ambao wakikushambulia Sana na ukikosa msaada unaweza kufa au kuwa katika Hali mbaya.

Soma Zaidi...
huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu sikioni

Post hii inahusu huduma ya kwanza kwa mtu aliyeingiwa na uchafu au kitu chochote sikioni. Sikio ni mojawapo ya milango ya fahamu ambapo hutumika kusikia, Kuna wakati vitu uingia ndani yake na kuleta madhara

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu vitamini C na kazi zake

Makala hii itakujulisha kazi kuu za vitamini C mwilini. Hapa pia utatambuwa ni kwa nini tunahitaji vitamini C na wapi tutavipata

Soma Zaidi...