picha

Utaratibu wa lishe kwa watoto

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa watoto

?

6. UTARATIBU WA LISHE KWA WATOTOKila mtu anatkiwa ale chakula kwa kulingana na mahitaji ya mwili wake. Motto anatakiwa ale vyakula maalumu kwa ajili ya kumuwezesha kukuwa vizuri umbo na kiakili. Halikadhalika mama wajawazito wanatakiwa wale vyakula maalumu kwa ajili ya kuwezesha afya ya mama na motto. Wazee, vijana, wafanyakazi na wagojwa wanatakiwa wale vyakula kulingana na hali zao. Hapa tutakuletea lishe kwa kulingana na makundi ya watu.Watoto wanatakiwa kula vyakula vya protinikwa wingi ili kuwezesha ukuaji wao wa mwili na tishu. Upungufu wa protini unaweza kumpelekea mtoto awe na ukuaji hafifu. Kwa ukuaji mzuri wa meno na mifupa mtoto anatakiwa apewe vyakula vya madini kama madini ya kashian(calcium) upungufu wa madini haya huenda mtoto akawa na ukuaji mbaya wa mifupa. Madini ya zink ni muhimu pia katika ukuaji wa mtoto.Vitamini B12 ni muhimu kwa ajili ya kuhakikisha utengenezwaji wa seli nyekundu za ndamu. Pia ijulikane kuwa ukuaji mzuri wa mtoto unategemea kuwepo na damu ya kutosha mwilini ili kuweza kusafirisha gesi ya oxygeni pamoja na viinilishe(nutrients) ndani ya mwili.Vitamini ni muhimu sana katika ukuaji wa mtoto. Watoto wapewe vyakula vyenye vitamini C kwa wingi kama machungwa, mapapai. Vitamini hivi vinamuwezesha mtoto kutengeneza kinga ya mwili ili kuweza kupamabana na maradhi. Watoto pia wanatakiwa wapewe vyakula vya wanga kwa wingi ili waweze kupata nguvu ya kutosha kuweza kufanya shughuli zao kama mazoezi ya kutambaa, kukumbia, kusimama n.k.

?

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 1452

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 web hosting     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Madhara ya ulevi

Poshi hii inahusu madhara ya ulevi.Utegemezi wa pombe kwa kawaida humaanisha kuwa mtu anatumia kiasi kikubwa cha pombe na kuna masuala kuhusu kupoteza udhibiti.

Soma Zaidi...
Namna ya kuchoma chanjo

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuchoma chanjo, ni njia ambazo utumika kutoa chanjo kwa watoto na watu wazima kwa utaratibu uliowekwa.

Soma Zaidi...
Mkojo usio wa kawaida huwa na vitu vifuatavyo.

Posti hii inahusu zaidi Aina ya mkojo usiokuwaa wa kawaida uwa na vitu vifuatavyo, ukiona dalili kama hizo wahi mapema hospitalini Ili upatiwe huduma.

Soma Zaidi...
Zijue sababu za chakula kushindwa kumengenywa kwenye tumbo.

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali za chakula kushindwa kumengenywa kwenye tumbo,ni sababu mbalimbali hasa za kiafya kama tutakavyoona hapo mbeleni

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA MTU ANAYETOKWA NA DAMU YA PUA

Kama mtu anatokwa na damu za pua, basi juwa kuwa anahitaji huduma ya kwanza.

Soma Zaidi...
Njia za kukabiliana na minyoo

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na minyoo

Soma Zaidi...