picha

Utaratibu wa lishe kwa watoto

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa watoto

?

6. UTARATIBU WA LISHE KWA WATOTOKila mtu anatkiwa ale chakula kwa kulingana na mahitaji ya mwili wake. Motto anatakiwa ale vyakula maalumu kwa ajili ya kumuwezesha kukuwa vizuri umbo na kiakili. Halikadhalika mama wajawazito wanatakiwa wale vyakula maalumu kwa ajili ya kuwezesha afya ya mama na motto. Wazee, vijana, wafanyakazi na wagojwa wanatakiwa wale vyakula kulingana na hali zao. Hapa tutakuletea lishe kwa kulingana na makundi ya watu.Watoto wanatakiwa kula vyakula vya protinikwa wingi ili kuwezesha ukuaji wao wa mwili na tishu. Upungufu wa protini unaweza kumpelekea mtoto awe na ukuaji hafifu. Kwa ukuaji mzuri wa meno na mifupa mtoto anatakiwa apewe vyakula vya madini kama madini ya kashian(calcium) upungufu wa madini haya huenda mtoto akawa na ukuaji mbaya wa mifupa. Madini ya zink ni muhimu pia katika ukuaji wa mtoto.Vitamini B12 ni muhimu kwa ajili ya kuhakikisha utengenezwaji wa seli nyekundu za ndamu. Pia ijulikane kuwa ukuaji mzuri wa mtoto unategemea kuwepo na damu ya kutosha mwilini ili kuweza kusafirisha gesi ya oxygeni pamoja na viinilishe(nutrients) ndani ya mwili.Vitamini ni muhimu sana katika ukuaji wa mtoto. Watoto wapewe vyakula vyenye vitamini C kwa wingi kama machungwa, mapapai. Vitamini hivi vinamuwezesha mtoto kutengeneza kinga ya mwili ili kuweza kupamabana na maradhi. Watoto pia wanatakiwa wapewe vyakula vya wanga kwa wingi ili waweze kupata nguvu ya kutosha kuweza kufanya shughuli zao kama mazoezi ya kutambaa, kukumbia, kusimama n.k.

?

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 1465

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 web hosting     ๐Ÿ‘‰2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     ๐Ÿ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     ๐Ÿ‘‰4 ai web app     ๐Ÿ‘‰5 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Huduma ya Kwanza kwa aliyepatwa na presha ya kupanda

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na presha ya kupanda

Soma Zaidi...
Huduma kwa wenye ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri

Post hii inahusu zaidi tiba na huduma kwa wenye ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri.

Soma Zaidi...
Upungufu wa protin

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa protini

Soma Zaidi...
Yajue malengo ya kusafisha vidonda.

Posti hii inahusu zaidi malengo ya kusafisha vidonda, kwa sababu Kuna watu wengine huwa wanajiuliza kwa nini nisafishe kidonda hospitalini au kwenye kituo chochote Cha afya, yafuatayo ni majibu ya kwa Nini nisafishe kidonda.

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEANGUKA KIFAFA

Kifafa kinaweza kumpata mtu muda wowte.

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENGโ€™ATWA NA NYUKI

Kungโ€™atwa na nyuki kunaweza kukahitaji huduma ya kwanza kwa haraka kama mgonjwa ana aleji na nyuki.

Soma Zaidi...