picha

Yajuwe mandalizi ya Ibada ya hija

Yajuwe mandalizi ya Ibada ya hija

Maandalizi ya Safari ya Hija



Maandalizi ya Hija hayaanzii kwenye miezi ya Hija, bali huanzia mbali katika umri wa mtu. Tunafahamu kuwa utekelezaji wa Ibada ya Hija unahitaji kuwa na uwezo wa kifedha (kimali). Hivyo Muislamu wa kweli katika kuchuma na kutumia mali yake, hana budi kuzingatia suala la nguzo ya Zaka na nguzo ya Hija. Muislamu atakapoweka mbele yake wazo la kutoa Zaka na Kuhiji, daima atachunga mipaka ya Mwenyezi Mungu (s.w) katika kuchuma kwake, kwani anafahamu wazi kuwa mali iliyochumwa kwa njia za haramu haifai kutolea Zaka au Kuhijia. Hebu tuzingatie hadithi ifuatayo:



Ibn Umar amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Swala haikubaliwi bila ya Twahara, wala Sadaqa haikubaliwi kama inatolewa kutokana na mali iliyochumwa kwa njia za haramu. (Muslim).



Halikadhalika, kutokana na hadithi hii, Hija haitasihi endapo mtu atahiji kwa kutumia mali iliyopatikana kwa njia za haramu. Hivyo, fikra ya kuhiji, humzoesha Muumini kuchunga mipaka ya Mwenyezi Mungu katika uchumi.



Pia fikra ya Hija humzoesha Muumini kutumia mali yake kwenye mambo muhimu tu ili kumuwezesha kuweka akiba kwa ajili ya Hija. Yaani fikra ya kutekeleza nguzo hii, humuepusha na ubadhirifu au utumiaji bila ya haja na bila ya ratiba.



Mtu anayekusudia kuhiji azidishe kutenda wema. Ajizatiti katika kusimamisha swala tano, kutoa Zaka, kufunga Ramadhani, kuwahurumia wanyonge kwa kuwapa misaada wanayohitajia na kusuhubiana vizuri na watu wote kwa ujumla. Amuombe msamaha kila aliyemkosea na amsamehe kila aliyemkosea. Pia mwenye kunuia Hija anatakiwa ajitahidi kujiepusha na maovu na azidishe kuomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu (s.w) kwa yote aliyokosea kwa kujua au kutojua na yaliyowazi au yaliyofichikana. Katika Qur-an Mwenyezi Mungu (s.w) anaagiza kwa wanaokusudia kuhiji:


β€œNa anayekusudia kufanya Hija katika miezi hiyo, basi asiseme maneno machafu, wala asifanye vitendo vichafu wala asibishane katika hiyo Hija. Na kheri yoyote mnayoifanya Mw enyezi Mungu anajua …” (2:197)



Utaona mtu mwenye fikra ya kutekeleza ibada ya Hija daima atakuwa mwangalifu katika mwenendo wake wa kila siku. Atajitahidi kutekeleza maamrisho yote ya Mwenyezi Mungu (s.w) na kujiepusha na makatazo yake yote atajitahidi kuwatendea wema wanaadamu wenzake na kila mara atakuwa mwenye kujiandaa kuitika mwito wa Mola wake (Labbayka), kama vile mtu anayejiandaa kukutana na Mola wake kwa kifo, muda mfupi ujao.






                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1607

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 web hosting    πŸ‘‰2 Dua za Mitume na Manabii    πŸ‘‰3 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰4 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰5 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Kuenea kwa dhana ya udhibiti uzazi na uzazi wa mpango

Kustawi kwa Kampeni ya Kudhibiti UzaziMiongoni mwa sababu zilizosaidia kustawi kwa kampeni hii ni matokeo ya mapinduzi ya viwanda (Industrial revolution) ya huko Ulaya.

Soma Zaidi...
Je ni kwa nini lengo la finga halifikiwi kwa wafungaji

Lengo la funga ni kuwa mchamungu sasa ni kwa nini wafungaji hawalifikii lengo hili na kuwa wachamungu.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya swala

Jifunze namna ya kuswali, zijuwe aina za swala na ujifunze masharti ya swala, kwa nini swala hazijibiwi? nini kifanyike?

Soma Zaidi...
MTAZAMO NA HUKUMU YA KUPANGA UZAZI WA MPANGO KWENYE UISLAMU

Atika uislamu swala la kupanga uzazi linaruhusiwa endapo kutakuwa na sababu maalumu za kisheria.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya uchumi katika uislamu

Katikabuislamu dhana ya uchumi imetofautiana na dhana ya kidunia hivi leo ambapo kamari na riba ni moja ya vitu muhimu katika uchumi.

Soma Zaidi...
Shart kuu nne za swala

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu masharti ya swala.

Soma Zaidi...
Kusimamisha Swala na kuamrisha mema

Swala iliyosimamishwa vilivyo ndiyo nyenzo kuu ya kumtakasa Muislamu na kumpa sifa zinazomuwezesha kustahiki kufanya kazi takatifu ya kusimamisha Uislamu katika jamii.

Soma Zaidi...
Aina za twahara na aina za najisi

Katika post hii utakwenda kuzijuwa aina za twahara katika uislamu. Utaviona vigawanyo vya twahara kulingana na maulamaa wa Fiqh

Soma Zaidi...