Sifa za Imamu Imamu ni kiongo kuongoza swala:
1. Mwenye zi. Mtu yeyote mwenye sifa zifuatazo anaweza
kuweza kuisoma Qur-an vizuri na mwenye
kuielewa vizuri.
2. Anayefahamu na kuelewa vizuri hadithi na Sunnah.
3. Mwenye tabia njema na siha nzuri.
4. Mwenye umri mkubwa (sifa hizi zizingatiwe kwa mfuatano wake).
Kama itatokea kwenye msikiti mmoja kuna watu wengi wenye sifa hizi, itabidi ipigwe kura. Pia kiongozi au mtu mwenye mamlaka katika jamii atakuwa ndiye mwenye haki ya kuwa Imamu. Hali kadhalika mtu akiwa nyumbani kwake, atakuwa ndiye mwenye haki ya kuwa Imamu. Sifa hizi zinabainishwa katika Hadithi ifuatayo:
Abu Mas ’ud amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Yule aliye na uwezo mkubwa zaidi wa kusoma Kitabu cha Allah (Qur-an) atakuwa Imamu wao. Kama watakuwa sawa kwa kusoma Qur-an basi atakuwa Imamu yule aliye na ujuzi mkubwa wa Hadithi, na kama wako sawa basi yule aliyetangulia kuhajiri (kuham a kutoka Makka kw enda Madina) na kama wako sawa katika kuhajiri, basi yule aliye na umri mkubwa kuliko wote ndiye atakayekuwa Imamu. Hakuna mtu atakaye kuwa Imamu wa yule aliyemzidi madaraka (au yule aliye na mamlaka juu yake) na wala hatakaa katika nyumba yake kwa kumpa heshima mpaka apate ridhaa yake. Na hakuna mtu atakayekuwa Imamu katika nyumba au familia ya mwingine. (Muslim).
Imamu wa msikiti atakapochaguliwa hapatakuwa na mwingine kuswalisha bila ruhu sa yake. Ni vibaya mno kujipachika Uimamu mahali bila ya ridhaa ya watu unaowaongoza. Aliyejipachika Uimamu swala yake haitasihi.
Ibn Umar amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema kuwa watu w atatu ambao sw ala zao hazitakubaliwa ni: “Yule anayeswalisha w atu na huku hawamtaki, anayekuja kwenye swala nyuma (kuja kwenye swala baada ya wakati kupita, pia kuswali mwenyewe nyuma ya mstari), na yule anayemfanya mwanamke huru kuwa mtumwa”.(Abu Daud, Ibn Majah).
Kumfuata Imamu baada ya kuwekwa ni jambo la lazima. Hata kama Imamu huyo atafanya makosa au dhambi kubwa kiasi gani kabla Waislamu hawajamtoa na kumweka mwingine itabidi lazima wamfuate kutokana na Hadithi ifuatayo:-
Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah (s.a.w) amesema, “Jihadi ni wajibu chini ya Amir yeyote akiwa mcha-Mungu, au si mcha-Mungu na hata kama atakuwa amefanya madhambi makubwa, na swala ni wajibu nyuma ya kila Imamu akiwa mcha-Mungu au si mcha-Mungu na hata akiwa amefanya madhambi makubwa ”. (Abu Daudi)
Inavyotakiwa, kama Imamu ataonekana kuwa anakiuka miiko ya Kiislamu kwa kutenda yale yaliyokatazwa katika Uislamu, kama vile zinaa, ulevi, wizi, n.k. itabidi Waislamu wamtoe kwenye Uimamu na kuweka Imamu mwingine mwenye sifa zilizotajwa. Kabla ya kuchagua mwingine watawajibika kumfuata Imamu huyo huyo muovu.Hekima yake ni kuepusha ugomvi, mifarakano baina ya waislamu.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Post hii itakufundisha mambo ambayo yatasababisha swqla yako isikubaliwe.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza utaratibu wa hutuba ya ndoa ya kiislamu. Sharti za jutuba ya ndoa na jinsibya kuozesha
Soma Zaidi...Post hii fupi itakwenda kukujulisha utaratibu wa kula daku.
Soma Zaidi...Kuchukuwavudhu ni ibada, lakini pia ni matendo ya kuufanya mwilivuwe safi. Katika post nitakwenda kukifundisha namna ya kutia udhu katika uislamu.
Soma Zaidi...(b) WarumiJamii ya Warumi nayo ni miongoni mwa jamii zinazohesabika kuwa zilianza kustaarabika mapema katika historia ya ulimwengu.
Soma Zaidi...Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako.
Soma Zaidi...Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Kwenye kipengele hichi tutajifinza vyanzo mbalimbali vya sheria ua kiislamu.
Soma Zaidi...