image

Ni zipi sifa za imamu wa swala?

Ni zipi sifa za imamu wa swala?

Sifa za Imamu Imamu ni kiongo kuongoza swala:



1. Mwenye zi. Mtu yeyote mwenye sifa zifuatazo anaweza
kuweza kuisoma Qur-an vizuri na mwenye
kuielewa vizuri.
2. Anayefahamu na kuelewa vizuri hadithi na Sunnah.
3. Mwenye tabia njema na siha nzuri.
4. Mwenye umri mkubwa (sifa hizi zizingatiwe kwa mfuatano wake).



Kama itatokea kwenye msikiti mmoja kuna watu wengi wenye sifa hizi, itabidi ipigwe kura. Pia kiongozi au mtu mwenye mamlaka katika jamii atakuwa ndiye mwenye haki ya kuwa Imamu. Hali kadhalika mtu akiwa nyumbani kwake, atakuwa ndiye mwenye haki ya kuwa Imamu. Sifa hizi zinabainishwa katika Hadithi ifuatayo:



Abu Mas ’ud amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Yule aliye na uwezo mkubwa zaidi wa kusoma Kitabu cha Allah (Qur-an) atakuwa Imamu wao. Kama watakuwa sawa kwa kusoma Qur-an basi atakuwa Imamu yule aliye na ujuzi mkubwa wa Hadithi, na kama wako sawa basi yule aliyetangulia kuhajiri (kuham a kutoka Makka kw enda Madina) na kama wako sawa katika kuhajiri, basi yule aliye na umri mkubwa kuliko wote ndiye atakayekuwa Imamu. Hakuna mtu atakaye kuwa Imamu wa yule aliyemzidi madaraka (au yule aliye na mamlaka juu yake) na wala hatakaa katika nyumba yake kwa kumpa heshima mpaka apate ridhaa yake. Na hakuna mtu atakayekuwa Imamu katika nyumba au familia ya mwingine. (Muslim).



Imamu wa msikiti atakapochaguliwa hapatakuwa na mwingine kuswalisha bila ruhu sa yake. Ni vibaya mno kujipachika Uimamu mahali bila ya ridhaa ya watu unaowaongoza. Aliyejipachika Uimamu swala yake haitasihi.



Ibn Umar amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema kuwa watu w atatu ambao sw ala zao hazitakubaliwa ni: “Yule anayeswalisha w atu na huku hawamtaki, anayekuja kwenye swala nyuma (kuja kwenye swala baada ya wakati kupita, pia kuswali mwenyewe nyuma ya mstari), na yule anayemfanya mwanamke huru kuwa mtumwa”.(Abu Daud, Ibn Majah).



Kumfuata Imamu baada ya kuwekwa ni jambo la lazima. Hata kama Imamu huyo atafanya makosa au dhambi kubwa kiasi gani kabla Waislamu hawajamtoa na kumweka mwingine itabidi lazima wamfuate kutokana na Hadithi ifuatayo:-



Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah (s.a.w) amesema, “Jihadi ni wajibu chini ya Amir yeyote akiwa mcha-Mungu, au si mcha-Mungu na hata kama atakuwa amefanya madhambi makubwa, na swala ni wajibu nyuma ya kila Imamu akiwa mcha-Mungu au si mcha-Mungu na hata akiwa amefanya madhambi makubwa ”. (Abu Daudi)
Inavyotakiwa, kama Imamu ataonekana kuwa anakiuka miiko ya Kiislamu kwa kutenda yale yaliyokatazwa katika Uislamu, kama vile zinaa, ulevi, wizi, n.k. itabidi Waislamu wamtoe kwenye Uimamu na kuweka Imamu mwingine mwenye sifa zilizotajwa. Kabla ya kuchagua mwingine watawajibika kumfuata Imamu huyo huyo muovu.Hekima yake ni kuepusha ugomvi, mifarakano baina ya waislamu.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1230


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Faida na umuhimu wa ndoa katika jamii
Hapa utajifunza faida za ndoa katika Jamii na kwa wanadamu kiafya, kiroho, kiuchumi Soma Zaidi...

Hawa ndio wanaoruhusiwa kurithi
Hii ni orodha ya watu ambao wanaweza kurithi malibya marehrmu. Soma Zaidi...

Sifa za imamu wa swala ya jamaa
Post hii inakwenda kukupa sifa za imamu wa msikitini anayepasa kuswalisha swala ya jamii. Soma Zaidi...

Maana ya shahada kama nguzo ya kwanza ya uislamu
4. Soma Zaidi...

Kujitwaharisha najisi kubwa najisi ya mbwa na Nguriwe
Soma Zaidi...

Yaliyo haramu kwa mtu asiyekuwa na udhu
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ambauo ni haramu kwa mtu asiye na udhu. Soma Zaidi...

Mwenendo wa mwenye kunuia hijjah na umrah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mambo yenye kufunguza swaumu (funga)
Soma Zaidi...

Sera ya uchumi katika uislamu
Hapa utajifunza sera za kiuchumi katika uchumi wa kiislamu. Hapa utajifunza sera kuu tatu za uchumi wa kiislamu. Soma Zaidi...

Kwanini wengi wanaohijji hawafikii lengo la hijjah zao
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

SHARTI ZA KUWAJIBIKA KWA ZAKA
Soma Zaidi...

Watu hawa huruhusiwi kuwaoa katika uislamu
Hapa utajifunza watu ambao ni halali kuwaoa na wale ambao ni haramu kuwaoa. Soma Zaidi...