Warithi wasio na mafungu maalumu katika uislamu

Hapa utajifunza watu wanaorithi bila ya kuwekewa mafungu maalumu au viwango maalumi vya kurithi.

Asaba - Warithi wasio na mafungu maalum

 


Asaba ni warithi wasiowekewa fungu maalum na hustahiki kupata mali yote ikiwa hapana wenye mafungu au kupata kilichobakia baada ya wenye mafungu kuchukua haki yao. Asaba wenyewe wako wa ama tatu:
(a)Asaba kwa nafsi yake.
(b)Asaba wa pamoja na mtu mwingine.
(c)Asaba kwa sababu ya mtu mwingine.
(a)Asaba kwa nafsi yake

 

(a)Asaba kwa nafsi yake
Ni wale wanaume tu ambao uhusiano wao na huyu marehemu haukuingiliwa na mwanamke. Nao ni hawa wafuatao:
I .Mtoto mwanamume.
2.Mjukuu (mwanamume).
3. Baba.
4.Babu (baba yake baba).
5.Ndugu wa kwa baba na mama.
6.Ndugu wa kwa baba.
7.Mtoto mwanamume wa ndugu wa kwa baba na mama.
8.Mtoto mwanamume wa ndugu wa kwa baba.
9.Ami wa kwa baba na mama.
1O.Ami wa kwa baba.
11.Mtoto mwanamume waAmi wa kwa baba na mama.
12.Mtoto mwanamume waAmi wa kwa baba.
13.Bwana na bibi mwenye kumuacha mtumwa huru.
14.Asaba wa mwenye kuacha huru mtumwa.

 


(b)Asaba wa Pamoja na mtu mwingine:
I .Binti akiwa pamoja na kijana mwanamume.
2.Binti wa mtoto wa kiume (mjukuu) akiwa pamoja na mtoto
mwanamume wa mtoto mwanamume (mjukuu wa kiume).
3. Dada wa kwa baba na mama akiwa pamoja na ndugu wa kwa
baba na mama.
4.Dada wa kwa baba akiwa pamoja na ndugu wa kwa baba.
5.Dada wa kwa baba na mama au wa kwa baba akiwa pamoja na babu.

 


(c) Asaba kwa sababu ya mtu mwingine:
Ni dada wa kwa baba na mama au wa kwa baba tu atakapokuwa pamoja na binti au binti wa mtoto wa kiume au wote wawili.

 


Musharakah - Kushirikiana fungu:
Ingawa asaba wote utaratibu wao wa kurithi ni mmoja lakini nani kati yao mwenye haki zaidi ya kurithi pindi wakitokea pamoja itategemea na uzawa wa karibu na uwiano wa uhusiano na maiti. Kwa mfano, uhusiano wa kwa baba na mama una nguvu zaidi kuliko uhusiano wa kwa baba tu, kwa hiyo, asaba wa kwa baba na mama ana haki ya kurithi kuliko asaba wa kwa baba tu.

 


Tumefahamu kwamba asaba hana fungu, bali huchukua urithi wote kama hakuna mwenye fungu, au huchukua kilicho bakia baada ya wenye mafungu kuchukua chao au hukosa kabisa kama hakuna kilicho bakia au wakati mwingine asaba wenye daraja sawa na mwenye fungu, watashirikiana fungu hilo. Kwa mfano: Amekufa mtu akaacha mume, mama, ndugu wa kwa mama zaidi ya mmoja na ndugu wa kwa baba na mam


 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1759

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 web hosting    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Twahara na umuhimu wake katika uislamu

Katika post hii utajifunza maana ya twahara kiligha na kishria. Pia utajifunza umuhimu wake

Soma Zaidi...
NI LIPI HASA LENGO LA KUFARADHISHWA SWALA ZA FARADHI NA KUWEPO KWA SWALA ZA SUNNAH (SUNA)

Lengo la Kusimamisha SwalaBila shaka swala imepewa umuhimu mkubwa kiasi cha kufanywa nguzo kubwa ya Uislamu kutokana na lengo lake.

Soma Zaidi...
msimamo wa uislamu juu ya kupanga uzazi na uzazi wa mpango

Msimamo wa Uislamu juu ya kudhibiti uzaziKama tulivyoona, msukumo wa kampeni ya kudhibiti kizazi, umetokana na mfumo mbaya wa kijamii na kiuchumi ulioundwa na wanadamu kutokana na matashi yao ya ubinafsi.

Soma Zaidi...
TOFAUTI KATI YA MAKATOZO NA MAAMRISHO KATIKA SUNNAH

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ عَبْدِ الرَّحْمَنِ بْنِ صَخْرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: سَمِعْت رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم يَقُولُ: "م...

Soma Zaidi...
Zijuwe nguzo tano za uislamu na maana zake katika sheria ya uislamu

Hili ni somo letu la kwanza kwenye mtiririko huu wa darsa za fiqh. Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya uislamu na nguzo zake.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kufanya suluhu kati ya mume na mke.

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kufanya suluhu katika ndoa.

Soma Zaidi...