Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)

Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)

Tukirejea Qur’an (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)

Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)

Tukirejea Qur’an (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a.s). Pamoja na Nabii Nuhu(a.s) kuahidiwa kuwa watu wake wa nyumbani watakuwa miongoni mwa watakaookolewa na gharka, mtoto wake alikataa kuingia kwenye jahazi(safina) na akawa ni miongoni mwa wenye kuangamia kama tunavyo jifunza katika aya zifuatazo.




Na akasema(Nuhu):”Pandeni humo, kwa jina la Mwenyezi Mungu kuwe kwenda kwake na kusimamma kwake. Hakika Mola wangu ni mwingi wa kusamehe na mwingi wa kurehemu.


Ikawa hiyo (jahazi) inakwenda nao katika mawimbi kama milima. Na Nuhu akamwita mwanawe aliyekuwa mbali amekataa kuingia jahazini: “Ewe mwanangu! Panda pamoja nasi wala usiwe pamoja na makafiri”. Na akasema (huyo mtoto)” “Nitaukimbilia Mlima utakaonilinda na maji” Akasema(Nuhu): “Hakuna leo wa kulindwa na amri ya Mwenyezi Mungu isipokuwa yule atakayemrehemu (Mwenyezi Mungu).” Mara mawimbi yakaingia baina yao na akawa miongoni mwa waliogharikishwa. (11:41-43)



Baada ya Gharika

Baada ya gharika kuisha, Nabii Nuhu(a.s) Ilibidi amuelekee Mola wake kutaka kujua ni vipi mwanawe amekuwa miongoni mwa walioangamia.




Na Nuhu alimuomba Mola wake (alipomuona mwanawe anaangamia) akasema: Ewe Mola wangu! Mwanangu ni katika watu wa nyumbani kwangu (mbona anaangamia)? Na hakika ahadi Yako ni haki; nawe ni mwenye haki kuliko mahakimu (wote).”Akasema (Mwenyezi Mungu): “Ewe Nuhu! Huyu si miongoni mwa watu wako. Yeye ni (mwenye) mwenendo usiokuwa mzuri. Basi usiniombe ambayo huyajui. Mimi nakunasihi usiwe miongoni mwa wajinga.” (Nuhu) Akasema: Ee Mola wangu! Mimi najikinga kwako nisije kukuombatena nisiyoyajua; na kama hutanisamehe na kunirehemu nitakuwa miongoni mwa watakaopata khasara.”(11:45-47)



Pia tunahamishwa juu ya kuangamia mke wa Nuhu(a.s) katika aya ifuatayo:




Mwenyezi Mungu amepiga (anapiga)mfano wa wale wabaya waliokufuru, ni mkewe Nuhu na mkewe Luti. Walikuwa chini ya waja wetu wema wawili hao miongoni mwa waja wetu (wema)’ lakini(wanawake hao), waliwafanyia khiana (waume zao watukufu hao) na (waume zao hao) hawakuweza kuwasaidia



chochote mbele ya Mwenyezi Mungu na ikasemwa: “Uingieni
Moto pamoja na hao wanaouingia.” (66:10)



Kuangamia kwa mtoto na mke wa Nuhu(a.s) pamoja na mke wa Lut(a.s) tunajifunza kuwa mtu hataokoka na ghadhabu ya Allah(s.w) kutokana a unasaba alioonao na watu wema na wala hata faidika na malipo ya amali njema walizofanya wengine. Kinyume chake hataadhibiwa mtu mwema kwa kuwa na unasaba na watu waovu maadamu anawafikishia ujumbe na wakamkanusha kama tunavyopigiwa mfano wa mke wa firaun,aliyekuwa mcha-mungu.




Na Mwenyezi Mngu amepiga, (anapiga) mfano wa wale walioamini kweli, ni mkewe Firauni, aliposema; “Ee Mola wangu! Nijengee nyumba Peponi karibu yako na uniokoe na Firauni na amali zake (mbovu), na Niokoe na watu madhalimu”(66:11)



                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 2118

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Je waislamu walishindwa vita vya Uhudi?
Je waislamu walishindwa vita vya Uhudi?

Katika vita vya Uhudi waislamu walikufa wengi kulinganisha na makafiri. Lakini makafiri walikimbia uwanja wa vita baada ya kuzidiwa. Je ni nanibalishindwa vita vya Uhudi kati ya waislamu na makafiri?

Soma Zaidi...
Maswali kuhusu Quran
Maswali kuhusu Quran

Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Nuhu(a.s)
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Nuhu(a.s)

(i) Tuanze kulingania kwa Tawhiid – kumjua Allah(s.

Soma Zaidi...
Musa(a.s) Ahamia Madiani
Musa(a.s) Ahamia Madiani

Mchana wa siku moja Musa(a.

Soma Zaidi...
Yusufu(a.s.) Akutana na Ndugu Zake
Yusufu(a.s.) Akutana na Ndugu Zake

Njaa ilitokea na ikawa hapana sehemu nyingine yoyote yenye chakula ila Misri.

Soma Zaidi...