Kuangamizwa Firauni na Majeshi Yake
Baada ya ushindi alioupata Musa(a.s) dhidi ya wachawi, umati wa watu waliokuwa wamekusanyika kushuhudia mapambano baina ya haki na batili, waliona ukweli kuwa Musa(a.s) ndiye kiongozi halali anayepaswa kutiiwa, na haifai kabisa kutiiwa Firauni dhalimu. Kuanzia hapo waliomuamini Musa wakapata adha na mateso zaidi kutoka kwa Firauni. Ndipo Allah(s.w) alipomuamuru Musa(a.s):
βNenda na waja wangu wakati wa usiku(mtoke nchini Misri), bila shaka mtafuatwa (26:52)
Na yalipokutana majeshi mawili. Watu wa Musa walisema. Hakika tutakamatwa. Musa akasema: La, kwa yakini Mola wangu Yu pamoja nami bila shaka ataniongoza.(26:61-62)
WanaIsrailwalikuwa wamekwama kuendeleana safari kutokana na kuzuiwa na bahari hali ya kuwa Firauni na majeshi yake yamekwisha wakaribia. Kwa huruma na rehema zake, Allah(s.w) akamuongoza Musa kwa kumwambia:
Bahari iligawanyika sehemu mbili na kuwacha njia ambayo Nabii Musa alipita na watu wake kwa salama. Lakini majeshi ya Firaun yalipofika katikati,maji ya bahari yalirudi katika nafasi yake na kuangamizwa yote. Firaun akawa anatapatapa, akijitupa huku na kule na akaona kuwa hapana nusra ila kutoka kwa Allah(s.w) ndipo akatoa shahada kuwa:
...............Naamini ya kwamba hakuna Mola aabudiwaye kwa haki ila Yule wanayemuamini wana wa Israeli, na mimi ni miongoni mwa wanaotii (10:90)
(Malaika wakamwambia)β Sasa (ndio unaamini)! hali uliasi kabla ya hapo na ukawa miongoni mwa waharibifu. Basi leo tutakuokoa kwa kuuweka mwili wako ili uwe dalili kwa ajili ya wa nyuma yako. Na watu wengi wameghafilika na ishara zetu.(10:91-92)
Huo ukawa ndio mwisho wa utawala wa kifirauni.
Umeionaje Makala hii.. ?
Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 17. Historia ya Bi Khadija na familia yake.
Soma Zaidi...Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Kutokana na Historia ya Nabii Musa na Harun(a.
Soma Zaidi...Kama tulivyoona katika maisha ya Mtume Ibrahim(a.
Soma Zaidi...