image

Kuangamizwa Firauni na Majeshi Yake

Kuangamizwa Firauni na Majeshi Yake

Kuangamizwa Firauni na Majeshi Yake


Baada ya ushindi alioupata Musa(a.s) dhidi ya wachawi, umati wa watu waliokuwa wamekusanyika kushuhudia mapambano baina ya haki na batili, waliona ukweli kuwa Musa(a.s) ndiye kiongozi halali anayepaswa kutiiwa, na haifai kabisa kutiiwa Firauni dhalimu. Kuanzia hapo waliomuamini Musa wakapata adha na mateso zaidi kutoka kwa Firauni. Ndipo Allah(s.w) alipomuamuru Musa(a.s):

β€œNenda na waja wangu wakati wa usiku(mtoke nchini Misri), bila shaka mtafuatwa (26:52)





Na yalipokutana majeshi mawili. Watu wa Musa walisema. Hakika tutakamatwa. Musa akasema: La, kwa yakini Mola wangu Yu pamoja nami bila shaka ataniongoza.(26:61-62)



WanaIsrailwalikuwa wamekwama kuendeleana safari kutokana na kuzuiwa na bahari hali ya kuwa Firauni na majeshi yake yamekwisha wakaribia. Kwa huruma na rehema zake, Allah(s.w) akamuongoza Musa kwa kumwambia:

Bahari iligawanyika sehemu mbili na kuwacha njia ambayo Nabii Musa alipita na watu wake kwa salama. Lakini majeshi ya Firaun yalipofika katikati,maji ya bahari yalirudi katika nafasi yake na kuangamizwa yote. Firaun akawa anatapatapa, akijitupa huku na kule na akaona kuwa hapana nusra ila kutoka kwa Allah(s.w) ndipo akatoa shahada kuwa:
...............Naamini ya kwamba hakuna Mola aabudiwaye kwa haki ila Yule wanayemuamini wana wa Israeli, na mimi ni miongoni mwa wanaotii (10:90)





(Malaika wakamwambia)” Sasa (ndio unaamini)! hali uliasi kabla ya hapo na ukawa miongoni mwa waharibifu. Basi leo tutakuokoa kwa kuuweka mwili wako ili uwe dalili kwa ajili ya wa nyuma yako. Na watu wengi wameghafilika na ishara zetu.(10:91-92)

Huo ukawa ndio mwisho wa utawala wa kifirauni.



                   



           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 379


Download our Apps
πŸ‘‰1 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰2 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰3 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

HISTORIA YA NABII ADAM
Soma Zaidi...

Harun(a.s), Achaguliwa Kuwa Msaidizi Musa(a.s) na kumkabili (kumlingania) firauni
Nabii Musa(a. Soma Zaidi...

Vita vya wenyewe kwa wenyewe baada ya kif cha khalifa Uthman
Soma Zaidi...

Historia ya uislamu wakati wa Makhalifa wanne: Abubakar, Umar, Uthman na Ally
Soma Zaidi...

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za kiafrika hapo zamani
3. Soma Zaidi...

Sababu ya uislamu kuwa ndiyo dini sahihi pekee
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Chokochoko na Upinzani wakati wa khalifa uthman khalifa wa Tatu
KUPOROMOKA KWA DOLA YA KIISLAMU ALIYOICHA MTUME(S. Soma Zaidi...

Historia ya Vijana wa Pangoni
Makafiri wa Kiquraish walikuwa na tabia ya kumghasi Mtume(s. Soma Zaidi...

Adam(a.s) na Mkewe Katika Pepo
Adam(a. Soma Zaidi...

Uteuzi wa Uthman bin Al-'Afan khalifa wa Tatu baada ya Mtume
Soma Zaidi...

Uendeshaji wa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII LUT(A.S) NA WATU WA SODOMA NA GOMORA
Mtume Lut(a. Soma Zaidi...