Kuangamizwa Firauni na Majeshi Yake
Baada ya ushindi alioupata Musa(a.s) dhidi ya wachawi, umati wa watu waliokuwa wamekusanyika kushuhudia mapambano baina ya haki na batili, waliona ukweli kuwa Musa(a.s) ndiye kiongozi halali anayepaswa kutiiwa, na haifai kabisa kutiiwa Firauni dhalimu. Kuanzia hapo waliomuamini Musa wakapata adha na mateso zaidi kutoka kwa Firauni. Ndipo Allah(s.w) alipomuamuru Musa(a.s):
โNenda na waja wangu wakati wa usiku(mtoke nchini Misri), bila shaka mtafuatwa (26:52)
Na yalipokutana majeshi mawili. Watu wa Musa walisema. Hakika tutakamatwa. Musa akasema: La, kwa yakini Mola wangu Yu pamoja nami bila shaka ataniongoza.(26:61-62)
WanaIsrailwalikuwa wamekwama kuendeleana safari kutokana na kuzuiwa na bahari hali ya kuwa Firauni na majeshi yake yamekwisha wakaribia. Kwa huruma na rehema zake, Allah(s.w) akamuongoza Musa kwa kumwambia:
Bahari iligawanyika sehemu mbili na kuwacha njia ambayo Nabii Musa alipita na watu wake kwa salama. Lakini majeshi ya Firaun yalipofika katikati,maji ya bahari yalirudi katika nafasi yake na kuangamizwa yote. Firaun akawa anatapatapa, akijitupa huku na kule na akaona kuwa hapana nusra ila kutoka kwa Allah(s.w) ndipo akatoa shahada kuwa:
...............Naamini ya kwamba hakuna Mola aabudiwaye kwa haki ila Yule wanayemuamini wana wa Israeli, na mimi ni miongoni mwa wanaotii (10:90)
(Malaika wakamwambia)โ Sasa (ndio unaamini)! hali uliasi kabla ya hapo na ukawa miongoni mwa waharibifu. Basi leo tutakuokoa kwa kuuweka mwili wako ili uwe dalili kwa ajili ya wa nyuma yako. Na watu wengi wameghafilika na ishara zetu.(10:91-92)
Huo ukawa ndio mwisho wa utawala wa kifirauni.
Umeionaje Makala hii.. ?
Vita vya Ahzab- Maquraish waliungana na mayahudi, wanafiki na makabila mengine ya waarabu baada ya kuona kuwa wao peke yao hawawezi kuufuta Uislamu.
Soma Zaidi...Katika kufikisha ujumbe huu kwa watu wake Nuhu(a.
Soma Zaidi...Kutokana na kisha hiki cha Nabii Ayyuub(a.
Soma Zaidi...KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee โAbdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana.
Soma Zaidi...Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Uchaguzi wa โUmar bin Khattab kuwa Khalifa wa Pili.
Soma Zaidi...Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 16. Hapa utajifunza maandalizi wa mjadala wa ndoa hizi.
Soma Zaidi...