Wapinzani wa Ujumbe wa Hud(a.s)

Waliomuamini Mtume Hud(a.

Wapinzani wa Ujumbe wa Hud(a.s)

Wapinzani wa Ujumbe wa Hud(a.s)


Waliomuamini Mtume Hud(a.s) walikuwa watu wachache na wengi walipinga ujumbe wake. Waliongozwa na Wakuu wa jamii.



“Wakasema wakuu waliokufuru katika kaumu yake, sisi tunakuona umo katika upumbavu na tunakuona u miongoni mwa waongo.” (7:66).



Katika kuupinga ujumbe wa Mtume Hud (a.s), makafiri walitoa hoja zifuatazo:



Kwanza,walidai kuwa hawako tayari kuacha kuabudu yale waliyokuwa wakiabudu wazee wao.




Wakasema: “Je! umetujia ili tumuabudu Mwenyezi Mungu peke yake na tuache waliyokuwa wakiabudu baba zetu? Basi tuletee unayotuahidi ikiwa ni miongoni mwa wasemao kweli.” (7:70).



Pili,walidai kuwa Hud(a.s) alikuwa mzushi kama wazushi wengine waliotokea katika zama mbali mbali na hasa pale alipowaambia watu watafufuliwa baada ya kufa na kulipwa kwa yale waliyoyafanya hapa duniani.



“Hayakuwa haya (ya kuja watu kusema kuwa wao ni Mitume) ila ni tabia ya watu wa (tangu) kale. Wala sisi hatutaadhibiwa (kama unavyodai na walivyodai hao).” (26:137-138)



“Je anakuahidini ya kwamba mtakapokufa na mkawa udongo na mifupa, kuwa mtatolewa, (mtafufuliwa)?” Hayawi hayo mnayoahidiwa.(23:35-36).



Hakuwa huyu (anayejiita Mtume) ila ni mtu anayemzulia Mwenyezi Mungu uwongo, wala sisi si wenye kumuamini. “(23:38)



Tatu,walidai kuwa Hud (a.s) alikuwa mpumbavu au mjinga.

“Wakasema wakuu waliokufuru katika kaumu yake, “Sisi tunakuona umo katika upumbavu na tunakuona u miongoni mwa waongo”. (7:66).



Nne, walidai kuwa hakuwa Mtume kwa kuwa alikuwa mtu ana yekula na kunywa kama wao:




Na wakubwa katika watu wake waliokufuru na kukadhibisha makutano ya akhera, na tuliwatajirisha katika maisha ya dunia, walisema: “Hakuwa huyu ila ni mtu kama nyinyi, anakula katika vile mnavyokula na anakunywa katika vile mnavyokunywa.” (23:33)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1254

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Nani alikuwa ni Sahaba wa kwanza kufariki akiwa Shahidi

Sahaba wa kwanz akufariki akiwa shahidi, alifariki kwa sababu ya mateso aliyoyapata kutoka kwa Makafiri wa ki Quraysh

Soma Zaidi...
Hija ya kuaga kwa mtume, na hutuba ya mwisho aliyotowa mtume katika hija

Mwaka mmoja baada ya msafara wa Tabuuk Bara Arab zima ilikuwa chini ya Dola ya Kiislamu.

Soma Zaidi...
tarekh 4

KUANGAMIZWA KWA JESHI LA TEMBOTukio la pili ni lile tukio la tembo, na ilikuwa hivi:- Kiongozi mmoja wa kiyemeni aliyetambulika kwa jina la Abrah aliona waarabu kutoka maeneo mbalimbali wanafunga misafara kuelekea Makkah kwa lengo la kwenda kuhiji.

Soma Zaidi...
Kulingania Uislamu kwa Jamii Nzima

Baada ya miaka mitatu ya Utume, Muhammad(s.

Soma Zaidi...
Kibri cha Ibilis na Uadui Wake Dhidi ya Binadamu

Ibilis ni katika jamii ya majini aliyekuwa pamoja na Malaika wakati amri ya kumsujudia Adam inatolewa.

Soma Zaidi...