Twahara

Twahara

FIQH 1.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Twahara

FIQH
1.TWAHARA
Twahara ni neno la kiarabu lenye maana ya usafi au unadhifu. Na neno hili kisheria ni kuondoa yale yanayomzuilia mtu kuswali ambayo ni katika hdathi na najisi, kwa kutumia maji au vinavyosimama badala ya kukosekana kwa maji kama udongo.

Kuondoa najisi ni jambo la wajibu pindi mtu anapokumbuka na akiwa na uwezo wa kufanya hivyo. Kama aliposema Allah kumwambia Mtume (s.a.s): “na nguozako uzitwaharishe” (surat muzammil: 4). Na Mtume صليالله عليه وسلم amesema “haikubaliwi swala (iliyoswaliwa ) bila ya udhu”.

Kuwa twahara tofauti na kuwa ni jambo lililohimizwa sana kwenye uislamu hata Mtume صليالله عليه وسلم akasema: “uislamu ni usafi” ila pia kuna faida nyingi sana tunazipata kwa kutekeleza jambo hili:

1.Twahara ni sharti katika kuswihi kwa sala. Hadithi iliyopokelewa kutoka kwa Mtume صليالله عليه وسلم amesema:”haikubaliwi swala ya mtu aliyehuduthi (aliyejamba) mpaka atawadhe” (Bukhari na Muslim)

2.Allah amewasifia sana watu ambao wanakuwa twahara. Amesema Allah “hakika Allah anawapenda wenye kutubia na anawapenda wenye kuwa twahara” (Surat baqara aya 222).

3.Kuwa twahara ni sababu ya kutokuadhibiwa kaburini. Ni kuwa watu ambao hawajikingi na najisi kama mkojo na hawajitwaharishi wataadhibiwa makaburini. Imesimuliwa hadithi na Ibn Abas kuwa Mtume صليالله عليه وسلم alipita kwenye makaburi mawili kisha akasema : “hakika watu hawa (waliozikwa hapa ) wanadhibiwa, na si kwa makosa makubwa bali kwa hakika huyu mmoja alikuwa hajisafishi anapokojoa.….” (Ibn Majah N Abu daud na isnad ya hadithi ni sahihi)

Aina za twahara.
Basi tambua kuwa twahara ip katika makundi makuu mawili ambayo ni:

1.twahara haqiqiya: nayo ni ni kujitwaharisha na khabathi yaani najisi na inaweza kuwa kwenye mavazi au mwili.

2.Twahara hukmiyah: nayo ni kujitwaharisha na hadathi na hii inahusiana na mwili tu na aina hii imegawanyika katika makundi matatu ambayo ni:-
A)Twahara kubwa; ambayo ni kuonga (josho la kisheria)
B)Twahara ndogo; nayo ni kutawadha yaani udhu
C)Twahara iliyo badala ya aina mbili zilizotangulia nayo ni kutayamam, yaani kujitwaharisha kwa kutumia udongo.


                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2376

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Kuzika-namna ya kuzika hatua kwa hatua
Kuzika-namna ya kuzika hatua kwa hatua

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nini maana ya kusimamisha swala
Nini maana ya kusimamisha swala

Post hii inakwenda kukufundisha maana ya kusimamisha swala kama inavyotumika kisheria.

Soma Zaidi...
Sifa nyingine za kuchaguwa mchumba ambazo watu wengi hawazijui
Sifa nyingine za kuchaguwa mchumba ambazo watu wengi hawazijui

Hizi ni sifa za ziada za mchumba katika uislamu. Sifa hizi wengi hawazijui ama hawazingatii.

Soma Zaidi...
Funga ya ramadhan na nyinginezo
Funga ya ramadhan na nyinginezo

Nguzo za uislamu (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
MALI ZISIZORUHUSIWA KUTOLEWA ZAKA
MALI ZISIZORUHUSIWA KUTOLEWA ZAKA

*Suala la kumilikiwa binaadam (utumwa), japokuwa linaendelea kutajwa kwenye Sharia (katika vitabu), ni suala ambalo haliko.

Soma Zaidi...
Hukumu ya talaka iliyotolewa kabla ya tendo la ndoa
Hukumu ya talaka iliyotolewa kabla ya tendo la ndoa

Endapo mtu atamuacha mke wake kabla hata ya kukutana kimwili, basi talaka hii itahukumiwa kwa namna hii.

Soma Zaidi...