image

MALI ZISIZORUHUSIWA KUTOLEWA ZAKA

*Suala la kumilikiwa binaadam (utumwa), japokuwa linaendelea kutajwa kwenye Sharia (katika vitabu), ni suala ambalo haliko.

MALI ZISIZORUHUSIWA KUTOLEWA ZAKA

HAIRUHUSIWI ZAKA

*Suala la kumilikiwa binaadam (utumwa), japokuwa linaendelea kutajwa kwenye Sharia (katika vitabu), ni suala ambalo haliko. Uislam tangu siku za Mtume s.a.w. umehimiza kwa kila hali kuwacha huru, kama vile kuwa ni kafara ya makosa tafauti, pia kuwa ni miongoni mwa sadaqa. Yote haya yamebainishwa wazi kabisa kwa Qauli za Mwenyezi Munguna Hadithi za Mtume s.a.w. Uislam ulifanya hivi ili kuondoa binaadam kummiliki binaadam.
Hatakiwi kutoa Zaka kafiri, hata ikiwa ni kafiri wa tangu asili; haya ni kutokana na qauli ya Amir-l-Muuminiina Sayyidna Abu Bukar Al Siddiq r.a.;

 

.
"Hii sadaqa ya fardhi alioifaridhisha Mtume s.a.w. juu ya Waislam". Kafiri, wakati ni kafiri haitakiwi Zaka kutoka kwake. Ama murtadi, yaani yule aliekuwa Islam kisha akaacha Uislam na kuingia ukafirini; yeye inamlazim juu yake yote yale ya Sharia yaliokuwa yakimlazim haliyakuwa ni Muislam, miongoni mwayo ni Zaka. Vilevile haimlazim Zaka mtu anaemilikiwa, kwani mwenye kumilikiwa hawezi kumiliki; hivi ni kwa Qauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu:    "……mtumwa aliemilikiwa, asiye weza kitu, ..........". ( Annahal : 75).

 

Aliemilikiwa, yeye na anachomiliki yeye ni cha bwana wake. Wala hakuna kutolewa Zaka kwa mali ya kwiba au kughusubiwa (kunyan'ganya), au mali iliowekwa amana na mwenyewe amekanusha kutoa Zaka, mali ya aina hii haujuzu kutolewa Zaka; hivi ni kwa vile haijuzu kutumiwa mali haya (hayakumilikiwa kihalali). Lakini basi, itabakia juu yake, yaani juu ya yale mali waajibu wa kutolewa Zaka, lakini haitalazimika kutolewa Zaka mpaka mali hayo yarejee kwa mwenyewe wa halali. Ikiwa mali yataharibika kabla ya kurejea kwa mwenyewe, itaondoka waajibu wa kutolewa Zaka mali hayo.

 

Vilevile mali ambayo iko deni (rahani) kwa mtu mwengine, mali hii hailazimiki Zaka yake mpaka irejee kwa mwenyewe. Mali ilio okotwa, (iliompotea mwenyewe) ikipitiwa na mwaka bila ya kujuulikana mwenyewe; Zaka ya mali hii itatolewa na mwenyewe pale atapoipokea hii mali yake, baada ya kuonekana (kuokotwa) na akakabidhiwa mwenyewe. Ama akijuulikana mwenyewe, na akaimiliki yule alieiokota basi yeye ndie ataeitolea Zaka mali hii kwa mujib wa shuruti na kutaanguka kulazimika kutolewa Zaka na yule mwenye mali wa asli.

 

Akiwa mtu atamiliki mali iliofikia kiwango cha kutolewa Zaka, haitafanywa hivyo mpaka mali hayo yapitiwe na mwaka; hivi ni kwa qauli ya Mtume s.a.w.:  .  Maana ya Hadithi hii ni kama hivi:
"Hakuna Zaka katika mali mpaka ipitiwe na mwaka". (Imehadithiwa na Abu Daud)
Vilevile wanyamahoa wanaofugwa na kulishiwa kwa majani na vyakula vya kulishiwa, si wenye kulishiwa machungani; hawa hawatolewi Zaka.
Hili limetolewa dalili kwa qauli ya Sayyidna Abu Bakar r.a.:

 

"Katika kondoo/mbuzi Zaka, na katika kondoo/mbuzi wenye kulishia machungani, wakiwa arubaini mpaka mia na ishirini hutolewa mbuzi mmoja". (Imehadithiwa na Al Bukhary).
Na hawa wanyamahoa wenye kujuzu kutolewa Zaka wenye kulishia machungani iwe ni katika machunga ya halali, si yenye haraam ndani yake; kama vile kuchungwa katika ardhi ilioghusubiwa, yaani ilionyan'ganywa; wanyama hao hawatafaa kutolewa Zaka.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 248


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake
Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

Kwanini lengo la funga halifikiwi na wafungaji wengi
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Hali ya kuzuiliana kurithi katika uislamu
KuzuilianaTumeona kuwa wanaume wenye kurithi ni 15 na wanawake wanaorithi ni 10. Soma Zaidi...

Ni yapi mambo yanayoharibu Swaumu na Mambo yanayobatilisha funga
Soma Zaidi...

Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf Soma Zaidi...

maana ya Eda na aina zake
Ni kipindi au muda wa kungojea mwanamke aliyepewa talaka (aliyeachwa) au kufiwa na mumewe kabla ya kuolewa na mume mwingine. Soma Zaidi...

mambo gani ni haramu kwa mwenye damu ya Hedhi na nifasi (damu ya uzazi)
Soma Zaidi...

Eda ya kufiwa na hukumu zake
Soma Zaidi...

MTAZAMO NA HUKUMU YA KUPANGA UZAZI WA MPANGO KWENYE UISLAMU
Atika uislamu swala la kupanga uzazi linaruhusiwa endapo kutakuwa na sababu maalumu za kisheria. Soma Zaidi...

Hizi ndio nyakati za swala tano na jinsi ya kuchunga nyakati za swala.
Posti hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi yavkuchunga nyakatibza swala tano. Soma Zaidi...

Twahara
FIQH 1. Soma Zaidi...

kwa nini riba ni haramu?
Soma Zaidi...