Haki na wajibu kwa masikini, mafukara na wasio jiweza

Haki na wajibu kwa masikini, mafukara na wasio jiweza

Wajibu kwa Maskini na Wasiojiweza



Kila Muislamu wa kweli anawajibika kuwahurumia wanaadamu wenziwe walio katika hali mbaya ya kiuchumi kiasi cha kushindwa kupata mahitaji muhimu ya maisha kama vile chakula, kivazi, makazi ya kuishi, Elimu sahihi ya msingi, na kadhalika. Muumini kwa mujibu wa Qur-an, pamoja na sifa ~nyingine, ni yule mwenye tabia ya kuwahurumia wanaadamu wenzake wasio na uwezo na kuwawezesha kupata mahitaji ya msingi ya maisha kama vile chakula. Tunasoma katika Qur-an:



Hakika watu wazuri watakunywa kinywaji kilichochanganyika na kafuri. (Hiyo kafuri) ni mto watakaounywa waja, wa Mwenyezi Mungu; watautitirisha mtitiririsho (mzuri namna watakavyo). (Watu hao ni hawa) wanaotimiza wajibu (wao) na wanaoiogopa siku ambayo shari yake itaenea (sana). Na huwalisha chakula maskini na may atima na wafungwa, na hali ya kuwa wenyewe wanakipenda (chakula hicho). (Husema wenyewe katika nyoyo zao wanapowapa chakula hicho); "Tunakulisheni kwa ajili ya kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu (tu) hatutaki kwenu malipo wala shukurani. "Hakika sisi tunaiogopa kwa Mola wetu hiyo siku yenye shida na taabu." Basi Mwenyezi Mungu atawalinda na shari ya siku hiyo na kuwakutanisha na neema nafuraha. (76:5-1 1)



Ukiipitia Qur-an utaona imerudiwa mara nyingi katika kuainisha waumini wa kweli na wacha-Mungu kuwa ni "wale wanaosimamisha swala na kutoa yale waliyoruzukiwa na Allah (s.w) kwa njia ya kuwasaidia wanaadamu wenziwe wanaohitajia msaada. Kinyume chake, tunajifunza katika Qur-an kuwa si muumini wa kweli yule asiyejali kuwahurumia wasio jiweza:


".Je, umemuona yule anayekadhibisha dini (asiye amini malipo ya akhera)? Huyu ni yule anayemnyanyasa yatima wala hajihimizi kuwalisha maskini." (107:1-3).




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 878

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Taratibu za mirathi katika zama za ujahilia

Kabla ya kuhubiriwa uislamu watu wa Maka walikuwa na tarayibu zenye dhuluma ndani yake katika ugawaji wa mirathi.

Soma Zaidi...
Taratibu za kumuona mchumba katika uislamu

Hspa utajifunza taratibu za kuonana na mchumba katika uislamu.

Soma Zaidi...
Matendo ya hijjah na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
JIFUNZE FIQH

Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka.

Soma Zaidi...
Sunnah za funga ya ramadhan

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Waislamu wanaolazimika kufunga

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...