Haki na wajibu kwa masikini, mafukara na wasio jiweza

Haki na wajibu kwa masikini, mafukara na wasio jiweza

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Haki na wajibu kwa masikini, mafukara na wasio jiweza

Wajibu kwa Maskini na Wasiojiweza



Kila Muislamu wa kweli anawajibika kuwahurumia wanaadamu wenziwe walio katika hali mbaya ya kiuchumi kiasi cha kushindwa kupata mahitaji muhimu ya maisha kama vile chakula, kivazi, makazi ya kuishi, Elimu sahihi ya msingi, na kadhalika. Muumini kwa mujibu wa Qur-an, pamoja na sifa ~nyingine, ni yule mwenye tabia ya kuwahurumia wanaadamu wenzake wasio na uwezo na kuwawezesha kupata mahitaji ya msingi ya maisha kama vile chakula. Tunasoma katika Qur-an:



Hakika watu wazuri watakunywa kinywaji kilichochanganyika na kafuri. (Hiyo kafuri) ni mto watakaounywa waja, wa Mwenyezi Mungu; watautitirisha mtitiririsho (mzuri namna watakavyo). (Watu hao ni hawa) wanaotimiza wajibu (wao) na wanaoiogopa siku ambayo shari yake itaenea (sana). Na huwalisha chakula maskini na may atima na wafungwa, na hali ya kuwa wenyewe wanakipenda (chakula hicho). (Husema wenyewe katika nyoyo zao wanapowapa chakula hicho); "Tunakulisheni kwa ajili ya kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu (tu) hatutaki kwenu malipo wala shukurani. "Hakika sisi tunaiogopa kwa Mola wetu hiyo siku yenye shida na taabu." Basi Mwenyezi Mungu atawalinda na shari ya siku hiyo na kuwakutanisha na neema nafuraha. (76:5-1 1)



Ukiipitia Qur-an utaona imerudiwa mara nyingi katika kuainisha waumini wa kweli na wacha-Mungu kuwa ni "wale wanaosimamisha swala na kutoa yale waliyoruzukiwa na Allah (s.w) kwa njia ya kuwasaidia wanaadamu wenziwe wanaohitajia msaada. Kinyume chake, tunajifunza katika Qur-an kuwa si muumini wa kweli yule asiyejali kuwahurumia wasio jiweza:


".Je, umemuona yule anayekadhibisha dini (asiye amini malipo ya akhera)? Huyu ni yule anayemnyanyasa yatima wala hajihimizi kuwalisha maskini." (107:1-3).




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1008

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Aina za talaka, sharti zake na taratibu za kutaliki katika uislamu
Aina za talaka, sharti zake na taratibu za kutaliki katika uislamu

Maana: ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa baina ya mume na mke mbele ya mashahidi wawili kwa kuzingatia sheria ya Kiislamu.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuelekea qibla katika swala.
Jinsi ya kuelekea qibla katika swala.

Je unadhani ni kwa nini waislamu wanaelekea kibla, na jinsi gani utaweza kukipata kibla.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya swala
Mafunzo ya swala

Jifunze namna ya kuswali, zijuwe aina za swala na ujifunze masharti ya swala, kwa nini swala hazijibiwi? nini kifanyike?

Soma Zaidi...
Zijuwe nguzo tano  za uislamu na maana zake katika sheria ya uislamu
Zijuwe nguzo tano za uislamu na maana zake katika sheria ya uislamu

Hili ni somo letu la kwanza kwenye mtiririko huu wa darsa za fiqh. Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya uislamu na nguzo zake.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kujitwaharisha Najisi hafifu na najisi ndogo
Jinsi ya kujitwaharisha Najisi hafifu na najisi ndogo

Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi hafifu na najisi ndogo.

Soma Zaidi...
sunnah za swala
sunnah za swala

Sunnah za SwalaSunnah za Swala Vipengele vya sunnah katika swala ni vile ambavyo mwenye kuswali akivitenda husaidia sana kukuza daraja ya swala yake na kuipa nguvu na msukumo mkubwa wa kuiwezesha kufikia lengo lililokusudiwa kwa urahisi zaidi.

Soma Zaidi...