Ni zipi siku ambazo ni haramu kufunga? na ni kwa nini hairuhusiwi kufunga katika siku hizo

Ni zipi siku ambazo ni haramu kufunga? na ni kwa nini hairuhusiwi kufunga katika siku hizo

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Ni zipi siku ambazo ni haramu kufunga? na ni kwa nini hairuhusiwi kufunga katika siku hizo

Siku Zilizoharamishwa Kufunga Sunnah



(i)Siku kuu za Iddil-Fitri na Iddil-Hajj



Imeharamishwa kufunga katika siku hizi kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo:
Abu Sayyid al-Khudri (r.a) ameeleza kwamba Mtume (s.a.w) amesema: Hakuna funga katika siku mbili - siku ya (Iddil) Fitr na siku ya (Idd ya) kuchinja.” (Bukhari na Muslim).



(ii)Siku za Tashriq
Siku za Tashriq ni mwezi 11 hadi 13 Dhul-Hijjah. Ni haram kufunga
katika siku hizi kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo:
Ibn Al-Hazali(r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Siku za Tashriqu ni siku za kula na kunywa na kumkumbuka Allah (s.w) (kwa Takbira). (Muslim).



(iii)Siku ya Shaka
Siku ya Shaka ni siku moja kabla ya Ramadhani. Yaani mwezi 30 Shaabani ambapo inawezekana ikawa ni siku ya kufunga. Mtume (s.a.w) amekataza kufunga sunnah katika siku hii ya mashaka ila kwa yule mwenye ada ya kufunga. Kwa mfano mtu mwenye ada ya kufunga Jumatatu ameruhusiwa kufunga endapo siku hiyo itaangukia Jumatatu. Hadith ifuatayo inabainisha makatazo haya:



Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuw a Mtume wa Allah amesema: “Usifunge siku moja au mbili kabla ya Ramadhani ila kwa mtu yule mwenye ada ya kufunga funga fulani (k.m. funga ya Alhamisi), yeye anaruhusiwa kufunga ” (Muslim).



Inatakiwa siku moja au mbili kabla ya Ramadhani tusifunge ili tuweze kuukabili tukiwa na nguvu mpya na ili tutofautishe funga ya Ramadhani na funga za Sunnah.



(iv) Siku ya Ijumaa
Mtume (s.a.w) amekataza funga ya Sunnah katika siku ya Ijumaa tu, lakini kama mtu ana tabia ya kufunga sunnah, ikatokea siku ya Ijumaa ni miongoni mwa siku anazofunga, basi hapana ubaya. Tunajifunza haya katika Hadith zifuatazo:



Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Na asifunge siku ya Ijumaa yeyote miongoni mwenu; ila tu akiwa ameanza kufunga kabla yake au ameendelea kufunga baada yake”. (Muslim).



Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Usiuchopoe usiku kabla ya Ijumaa ukafanya usiku pekee kwa kusimama kwa swala na usiichague siku ya Ijumaa pekee kati ya siku za wiki kuwa ndio siku ya kufunga, ila kama mmoja wenu ana tabia ya kufunga sunnah na ikatokea siku ya Ijumaa imeangukia katika tarehe anayopaswa kufunga. ” (Muslim).




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2570

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Jinsi ya kutawadha kama aalivyotawadha Mtume Muhammad (s.a.w)
Jinsi ya kutawadha kama aalivyotawadha Mtume Muhammad (s.a.w)

Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutawadha kama vile ambavyo alitawadha Mtume

Soma Zaidi...
Mgawanyo wa mirathi kutoka kwenye Quran
Mgawanyo wa mirathi kutoka kwenye Quran

Quran imegawanya mirathi katika haki. Mgawanyo huu ndio unaotakiwa utumike na si vinhinevyo.

Soma Zaidi...
JIFUNZE FIQH
JIFUNZE FIQH

Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka.

Soma Zaidi...
Dhamana ya Kuchunga Ahadi Katika Uislamu
Dhamana ya Kuchunga Ahadi Katika Uislamu

Kuchunga au kutekeleza ahadi ni miongoni mwa vipengele muhimu vya tabia ya muumini wa kweli.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa funga ya ramadhan
Umuhimu wa funga ya ramadhan

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Taratibu za kumuona mchumba katika uislamu
Taratibu za kumuona mchumba katika uislamu

Hspa utajifunza taratibu za kuonana na mchumba katika uislamu.

Soma Zaidi...
Maswali juu ya Mambo anayopaswa kufanyiwa maiti ya muislamu
Maswali juu ya Mambo anayopaswa kufanyiwa maiti ya muislamu

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...