haya ndiyo mambo yanayaribu swala na yanayobatilisha swala

haya ndiyo mambo yanayaribu swala na yanayobatilisha swala

Mambo yanayobatilisha Swala



Mtu akiwa katika swala yuko katika hali maalum na haruhusiwi kufanya kitu kingine nje ya swala hata vile vitendo vya kawaida alivyovizoea. Hivyo ukiwa ndani ya swala ukifanya au kukitokea moja ya mambo yafuatayo, swala yako itakuwa imebatilika na itabidi uanze upya.



(a) Kutoelekea Qibla kwa kifua pasi na dharura yoyote ya kisheria. (b) Kupatikana na hadathi kubwa, ndogo au ya kati na kati.
(c) Kufikwa na najisi mwilini, nguoni au mahali pa kuswalia.
(d) Kuvukwa na nguo ukawa uchi. Wanaume wanaovaa shati fupi wajihadhari sana hapa kwani,hasa wakati wa kurukuu na kusujudu, migongo yao (viuno vyao) chini ya usawa wa kitovu (panda za makalio) huwa wazi na hivi huhesabiwa kuwa wako uchi.
(e) Kusema au kutamka makusudi lau herufi moja yenye kuleta maana nje ya maneno ya swala.Mtume (s.a.w) amesema: gHakika ya hii swala, haifai ndani yake maneno ya watu kwani swala yenyewe ni Tasbih, Takbir na kusoma Qur-an. (Muslim)
(f) Kula au kunywa japo kwa kusahau. (g) Kufanya jambo lisilowiana na swala mfululizo mara tatu. (h) Kuiacha nguzo yoyote ya swala
(i) Ukizidisha nguzo yoyote ya swala makusudi.
(j) Kumtangulia Imam au kuchelewa kwa nguzo mbili za kimatendo kwa makusudi.
(k) Kutia nia ya kuikata swala au kujishauri moyoni kuwa uikate au usiikate swala.
(l) Kuwa na shaka kuwa umetimiza au hujatimiza sharti au nguzo yoyote ya swala.
(m) Kupotewa na akili au kulala ndani ya swala.
(n) Kutoa Salaam kwa makusudi kabla ya kwisha swala.
(o) Kuswalishwa na asiyekuwa Muislamu.
(p) Kukhalifu utaratibu wa nguzo za swala, yaani kutangulia kutekeleza nguzo ya swala kabla ya kutekeleza nguzo inayostahiki kutangulia katika utaratibu wa swala.
(q) Kuleta dua ya kuomba kitu haramu au muhali.
(r) Kumshirikisha Allah (s.w) katika kuleta dua yaani kuleta dua ya kuomba kitu cha halali lakini humuombi Allah (s.w) peke yake.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2156

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 web hosting    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Ni nini maana ya swala

Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu maana halisi ya ibada ya swala.

Soma Zaidi...
Sunnah za swaumu, sunnah ambazo zinaambatans ns kufungabmwezi wa Ramadhani

Yajuwe mambo ambayo yanapendeza kuyafanya wakati ukiwa umefunga Ramadhani.

Soma Zaidi...
Hijja na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Lengo la funga linavyofikiwa

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Faida za kuswali swala za sunnah

Posti hii inakwenda kukufundisha kuhush swala za sunnah.

Soma Zaidi...
udhaifu wa hoja za kuunga mkono kuzibiti uzazi na uzazi wa mpango

Udhaifu wa Hoja za Kudhibiti Uzazi:Hoja nyingi zinazotolewa kuunga mkono udhibiti wa uzazi zimejengwa juu ya hali na mazingira ya maisha yaliyoletwa na utamaduni na maendeleo ya nchi za Ulaya na Marekani.

Soma Zaidi...
Jinsi ambavyo msafiri anatakiwa aswali akiwa safarini

Postvhiibinakwenda kukufundisha kuhusu swala ya msafiri na jinsi ya kuiswali.

Soma Zaidi...