Hili ndilo hasa lengo la kuamrishwa kufunga

Hili ndilo hasa lengo la kuamrishwa kufunga

Lengo la Funga



Lengo la funga limebainishwa katika Qur-an pale ilipotolewa amri ya kufunga:


“Enyi mlioamini! Mmeamrishwa kufunga kama walivyoamrishwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Mungu ”. (2:183)


Hapa tunabainishwiwa kuwa lengo la kufunga ni kuwafanya Waumini kuwa wacha-Mungu. Neno “Taqwa ” ambalo linatafsiriwa kuwa ni “Uchamungu” lina maana pana zaidi. “Taqwa” ni hali ya kuhofu ghadhabu za Mwenyezi Mungu (s.w) ambayo humfanya mja ajiepushe mbali na yale yote yanayomghadhibisha Mwenyezi Mungu (s.w) na ayaendee mbio kwa unyenyekevu na kwa jitihada kubwa yale yote aliyoamrisha Mwenyezi Mungu (s.w) na yale yote anayoyaridhia. Maana ya ‘Taqwa’ inabainishwa vyema na Hadith ifuatayo:



Siku moja Umar (r.a) alimuuliza Ubbay bin Ka ’b (r.a) amueleweshe maana hasa ya Taqwa. Ubbay (r.a) alijibu: “Amir Muuminin, umewahi kupita njia ya kichaka chenye miba?” Umar (r.a) akajibu: “Naam, nimepita mara nyingi” Kisha Ubbay (r.a) akamuuliza ni hadhari gani uliyoichukua wakati ukipita huko? “Nilishikilia na kukusanya pamoja nguo zangu na kutembea kwa uangalifu katika kupita njia hiyo”, alisema Umar (r.a) ili sehemu yoyote ya nguo zangu isije shikwa na miba hiyo”. Kutokana na jibu hili, Ubbay (r.a) alisema: “Hii hasa ndio maana ya “Taqwa”.



Kutokana na mfano huu mtu mwenye “Taqwa” au Muttaq ni yule mwenye shauku na jitihada kubwa kuepukana na kila aina ya mwiba (uovu) katika kila hatua na kila kipengele cha maisha yake yote na wakati huo huo huwa na shauku na jitihada kubwa ya kuyakimbilia mema katika kila hatua ya maisha yake ili kupata radhi za Mwenyezi Mungu (s.w). Muttaq ni mtu mwenye cheo na hadhi kubwa sana mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w) kama tunavyofahamishwa katika Qur-an:


“... Hakika aheshimiwaye sana miongoni mwenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule aliye Muttaq (am chaye Mw enyezi Mungu zaidi) katika nyinyi. Kw a yakini Mwenyezi Mungu ni Mjuzi Mw enye khabari ya mambo yote. (49:13).



Hiki ni cheo kikubwa sana ambacho hakina mfano wake katika vyeo vya hapa ulimwenguni. Cheo hiki hakipatikani kwa kuomba kura au kwa hongo, bali kinapatikana kwa kujizatiti kujiepusha na makatazo yote ya Mwenyezi Mungu (s.w) na kujitahidi kutenda mema na kutekeleza maamrisho yote ya Mwenyezi Mungu (s.w) kwa matarajio ya kupata Radhi ya Mwenyezi Mungu (s.w).




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1188

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

JIFUNZE FIQH

Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutwaharisha aina mbalimbali za najisi

Kila najisi ina namna yake ya kutwaharisha, hata hivyo namna hizo hufanana. Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutwaharisha najisi mbalimbali.

Soma Zaidi...
benki za kiislamu na njia zake za kuingiza kipato

Benki za KiislamuBenki za Kiislamu ambazo hutoa huduma kama benki nyingine zinaendeshwa katika msingi wa biashara na sio ule wa riba.

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya hijjah na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Msimamo wa Uislamu juu ya Utumwa

- Watumwa walikuwa wakikamatwa na kutezwa nguvu bila kujali utu na ubinaadamu wao.

Soma Zaidi...
Haki za binadamu kwa ujumla (basic human rights)

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sura zinazosomwa katika Swala ya Dhuha

Swala ya Dhuha ni swala ya sunna inayosaliwa wakati wa asubuhi baada ya jua kuchomoza na kupanda angalau kiasi cha mkuki (takribani dakika 15 baada ya jua kuchomoza) mpaka kabla ya adhuhuri. Ingawa hakuna sura maalum zilizowekwa kisheria, Mtume ﷺ alisoma baadhi ya sura zenye maana ya kuhimiza kheri na shukrani.

Soma Zaidi...