Jinsi ya kuoga josho la kiislamu ( janaba, hedhi na nifasi)
Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kuoga josho kisheria.
Masharti ya Kuoga
Masharti ya kuoga ni sawa tu na yale masharti ya udhu ila hapa yanahusu mwili mzima.
Nguzo za Kuoga
Kwanza, kutia nia moyoni kuwa unaoga kwa madhumuni ya kujitwaharisha, kutokana na janaba, hedhi, au nifasi. Mahali pa nia ni moyoni na wakati wa kunuiwa ni pale unapoanza kuosha kiungo cha kwanza.
Pili, kueneza maji mwili mzima. Ili kuhakikisha kuwa umeeneza maji mwili mzima ni vyema ufuate mafundisho ya Mtume (s.a.w). Mtume katika kuoga alikuwa akianza kwa kuosha sehemu za siri, kisha alikuwa akitia udhu, kisha alikuwa akijimiminia maji kichwani mara tatu, kisha alikuwa akieneza maji mwili mzima kwa kuanzia upande wa kulia na kumalizia upande wa kushoto, pote mara tatu tatu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 web hosting 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Mambo anayofanyiwa mtu anayekaribia kufa
Haya ni maandalizi anayofanyiwa mtu aliye katika kilevi cha kifo yaani sakaratul maut
Soma Zaidi...msimamo wa uislamu juu ya kupanga uzazi na uzazi wa mpango
Msimamo wa Uislamu juu ya kudhibiti uzaziKama tulivyoona, msukumo wa kampeni ya kudhibiti kizazi, umetokana na mfumo mbaya wa kijamii na kiuchumi ulioundwa na wanadamu kutokana na matashi yao ya ubinafsi.
Soma Zaidi...