Hali ya kuzuiliana kurithi katika uislamu
KuzuilianaTumeona kuwa wanaume wenye kurithi ni 15 na wanawake wanaorithi ni 10.
Kuzuiliana
Tumeona kuwa wanaume wenye kurithi ni 15 na wanawake wanaorithi ni 10. Lakini wote hawa 25 wakikutana pamoja hawawezi kurithi wote bali baadhi yao huwazuilia wengine wasipate kitu au wasipate fungu kubwa. Katika kipengele hiki tunaonyesha wanaozuiliwa na wasiozuiliwa.
1.Mtoto mwanamume hazuiliwi na mtu.
2.Mjukuu huzuiliwa na mtoto mwanamume na kila mtoto wa kiume aliyeko mbali huzuiliwa na aliyoko karibu na marehemu. 3.baba hazuiliwi na mtu.
4.Babu wa upande wowote huzuiliwa na baba au babu wa karibu zaidi (kama vile baba yake baba humzuilia babu yake baba).
5.Ndugu wa kwa baba huzuiliwa na ndugu wa kwa baba na mama; na kila amzuiliaye yeye (huyo ndugu wa kwa baba na mama) vile vile huzuiliwa na dada wa kwa baba na mama akiwa pamoja na binti au binti wa mtoto wa kiume (mjukuu) au wote wawili.
6.Ndugu wa kwa mama huzuiliwa na mtoto au mtoto wa mtoto mwanamume au baba au babu.
7.Mume hazuiliwi na mtu wala
8.Mke hazuiliwi na mtu.
9.Binti hazuiliwi.
1O.Mama hazuiliwi.
11.Bibi huzuiliwa na mama.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 web hosting 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Jinsi ambavyo mtu anazuiliwa kurithi mali ya marehemu
Endapo mtu yupp katika orodha ya wanaotakiwa kutithi, anaweza kuzuiliwa kurithi kwa kuzingatia haya.
Soma Zaidi...Hili ndio lengo la kufunga.
Ni kwa nini Allah ametutaka tugunge. Je kuna lengo gani hasa katika kufunga.
Soma Zaidi...Tofauti kati ya hijjah na umrah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Jukumu la serikali katika kuzuia dhuluma
Serikali ina nafasi kubwa katika kuzuia dhulma na kufanya uchumibuwe huru kuyokana na dhulma.
Soma Zaidi...