Vyumba vidogo vidogo kwenye chumba cha upasuaji

Post hii inahusu zaidi juu ya vyumba vidogo vidogo ambavyo Vimo kwenye chumba cha upasuaji, ingawa chumba cha upasuaji ni kimoja ila kuna vyumba vingine vidogo ambavyo vinatumika kwa kazi mbalimbali kama tutakavyoona.

Vyumba vidogo vidogo kwenye chumba cha upasuaji.

1.chumba cha mapokezi na kuruhusu mgonjwa kutoka kwenye upasuaji.

Hiki ni mojawapo ya vyumba vidogo ambavyo Vimo kwenye chumba cha upasuaji katika chumba hiki mgonjwa upokelewa na kuangalia kama ana sifa za kuingia kwenye upasuaji na vile vile kwenye chumba hiki mgonjwa akimaliza kufanyiwa upasuaji upitia hapa ili kuhakikisha kuwa kama mgonjwa yu hai au ana tatizo lolote lililompata kama mgonjwa yuko vizuri huweza kupelekwa kwenye chumba muhimu kwa ajili ya kupona.

 

2.Chumba cha mtoa dawa ya usingizi,

Hiki ni chumba maalum ambako mtoa huduma ya usingizi ukutana na mgonjwa na kumuuliza pamoja na kujadiliana kuhusu dawa ya usingizi anayotaka kupewa kama ni ya mwili mzima au niya nusu kwa hiyo Mgonjwa uweza kuchagua, pamoja na uchaguzi wa mgonjwa na mtoa huduma hii anapaswa kumshauri kulingana na hali halisi ya mgonjwa.

 

3.Chumba cha kupumzika Mgonjwa baada ya upasuaji.

Hiki ni chumba ambacho mgonjwa anapumzika baada ya upasuaji katika chumba hiki mgonjwa uangaliwa zaidi na kupewa huduma zote mpaka pale atakapopona na kurudia kwenye hali yake ya kawaida kwenye chumba hiki panapaswa kuwepo na gasi ya oxygen, maji ya kutosha kwa ajili ya mgonjwa mgonjwa anapaswa  kuwa makini ili kuepuka matatizo baada ya upasuaji kama vile kuishiwa damu na mengine kama hayo.

 

4.Chumba maalum cha kusafishia vifaa.

Hiki ni chumba ambacho vifaa vyote vinavyotumika wakati wa upasuaji vinasafishiwa kwa hiyo chumba hiki kinapaswa kuwepo kwa maji safi ya sabuni, maji yenye chlorine, maji ya kusuuzia na baada ya kutoa uchafu huu vinapaswa kupelekwa ili kuingizwa na kuua bakteria wote na mtu anayefanya kazi kwenye chumba hiki anapaswa kuwa na Elimu  ya kutosha na awe amesomea kazi hiyo kwa kufanya hivyo wadudu wote wataweza kufa na kuzuiliwa kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

 

5. Chumba cha kubadilishia nguo.

Tukumbuke kuwa kabla ya kuanza upasuaji ni lazima kubadilisha nguo za nyumbani na kuvaa nguo za upasuaji hii ufanyika ili kuzuia kusambaa kwa bakteria kutoka kwa mhudumu kwenda kwa mgonjwa kwa hiyo ndo maana kuna chumba maalum kwa ajili ya kubadilisha nguo

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Afya File: Download PDF Views 644

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

darasa la lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...
Zijuwe faida za kiafya za kula Zabibu

Kula zabibubkina faida nyingi kwa afya yako.

Soma Zaidi...
Madhara kwa wasiofanya mazoezi

Posti hii inahusu zaidi madhara mbalimbali ambayo yanaweza kutokea kwa watu wasiofanya mazoezi, mazoezi ni kama tiba kwa namna Moja au nyingine ila Kuna madhara ambayo yanaweza kutokea kwa wale ambao hawafanyi mazoezi.

Soma Zaidi...
NAMNA YA KUTUNZA AFYA KUANZIA JIKONI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Dondoo za afya 41-60

Somo Hili linakwenda kukuletea dondoo mbalimbali za afya

Soma Zaidi...
Vipi mkojo unaeleza kuhusu afya ya mtu

Hapa tutajifunza namna ambavyo mkojo unaweza kueleza kuhusu hali ya kiafya ya mtu

Soma Zaidi...
MAWAKALA WA KUSABABISHA NA KUSAMBAZA MARADHI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
MAWAKALA WA MARADHI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...