picha

Vyumba vidogo vidogo kwenye chumba cha upasuaji

Post hii inahusu zaidi juu ya vyumba vidogo vidogo ambavyo Vimo kwenye chumba cha upasuaji, ingawa chumba cha upasuaji ni kimoja ila kuna vyumba vingine vidogo ambavyo vinatumika kwa kazi mbalimbali kama tutakavyoona.

Vyumba vidogo vidogo kwenye chumba cha upasuaji.

1.chumba cha mapokezi na kuruhusu mgonjwa kutoka kwenye upasuaji.

Hiki ni mojawapo ya vyumba vidogo ambavyo Vimo kwenye chumba cha upasuaji katika chumba hiki mgonjwa upokelewa na kuangalia kama ana sifa za kuingia kwenye upasuaji na vile vile kwenye chumba hiki mgonjwa akimaliza kufanyiwa upasuaji upitia hapa ili kuhakikisha kuwa kama mgonjwa yu hai au ana tatizo lolote lililompata kama mgonjwa yuko vizuri huweza kupelekwa kwenye chumba muhimu kwa ajili ya kupona.

 

2.Chumba cha mtoa dawa ya usingizi,

Hiki ni chumba maalum ambako mtoa huduma ya usingizi ukutana na mgonjwa na kumuuliza pamoja na kujadiliana kuhusu dawa ya usingizi anayotaka kupewa kama ni ya mwili mzima au niya nusu kwa hiyo Mgonjwa uweza kuchagua, pamoja na uchaguzi wa mgonjwa na mtoa huduma hii anapaswa kumshauri kulingana na hali halisi ya mgonjwa.

 

3.Chumba cha kupumzika Mgonjwa baada ya upasuaji.

Hiki ni chumba ambacho mgonjwa anapumzika baada ya upasuaji katika chumba hiki mgonjwa uangaliwa zaidi na kupewa huduma zote mpaka pale atakapopona na kurudia kwenye hali yake ya kawaida kwenye chumba hiki panapaswa kuwepo na gasi ya oxygen, maji ya kutosha kwa ajili ya mgonjwa mgonjwa anapaswa  kuwa makini ili kuepuka matatizo baada ya upasuaji kama vile kuishiwa damu na mengine kama hayo.

 

4.Chumba maalum cha kusafishia vifaa.

Hiki ni chumba ambacho vifaa vyote vinavyotumika wakati wa upasuaji vinasafishiwa kwa hiyo chumba hiki kinapaswa kuwepo kwa maji safi ya sabuni, maji yenye chlorine, maji ya kusuuzia na baada ya kutoa uchafu huu vinapaswa kupelekwa ili kuingizwa na kuua bakteria wote na mtu anayefanya kazi kwenye chumba hiki anapaswa kuwa na Elimu  ya kutosha na awe amesomea kazi hiyo kwa kufanya hivyo wadudu wote wataweza kufa na kuzuiliwa kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

 

5. Chumba cha kubadilishia nguo.

Tukumbuke kuwa kabla ya kuanza upasuaji ni lazima kubadilisha nguo za nyumbani na kuvaa nguo za upasuaji hii ufanyika ili kuzuia kusambaa kwa bakteria kutoka kwa mhudumu kwenda kwa mgonjwa kwa hiyo ndo maana kuna chumba maalum kwa ajili ya kubadilisha nguo

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jifunze Main: Post File: Download PDF Views 1001

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

HUDUMA ZA KIAFYA KATIKA JAMII

Umuhimu wa huduma za kiafya katika jamii

Soma Zaidi...
dondoo za afya

Basi tambua haya;- 1.

Soma Zaidi...
AINA ZA VYAKULA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Dondoo za afya 1-20

Somo Hili linakwenda kukuletea dondoo mbalimbali za afya

Soma Zaidi...
ITAMBUE SARATANI CHANZO CHAKE, DALILI NA KUKABILIANA NAYO

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...