Vyumba vidogo vidogo kwenye chumba cha upasuaji


image


Post hii inahusu zaidi juu ya vyumba vidogo vidogo ambavyo Vimo kwenye chumba cha upasuaji, ingawa chumba cha upasuaji ni kimoja ila kuna vyumba vingine vidogo ambavyo vinatumika kwa kazi mbalimbali kama tutakavyoona.


Vyumba vidogo vidogo kwenye chumba cha upasuaji.

1.chumba cha mapokezi na kuruhusu mgonjwa kutoka kwenye upasuaji.

Hiki ni mojawapo ya vyumba vidogo ambavyo Vimo kwenye chumba cha upasuaji katika chumba hiki mgonjwa upokelewa na kuangalia kama ana sifa za kuingia kwenye upasuaji na vile vile kwenye chumba hiki mgonjwa akimaliza kufanyiwa upasuaji upitia hapa ili kuhakikisha kuwa kama mgonjwa yu hai au ana tatizo lolote lililompata kama mgonjwa yuko vizuri huweza kupelekwa kwenye chumba muhimu kwa ajili ya kupona.

 

2.Chumba cha mtoa dawa ya usingizi,

Hiki ni chumba maalum ambako mtoa huduma ya usingizi ukutana na mgonjwa na kumuuliza pamoja na kujadiliana kuhusu dawa ya usingizi anayotaka kupewa kama ni ya mwili mzima au niya nusu kwa hiyo Mgonjwa uweza kuchagua, pamoja na uchaguzi wa mgonjwa na mtoa huduma hii anapaswa kumshauri kulingana na hali halisi ya mgonjwa.

 

3.Chumba cha kupumzika Mgonjwa baada ya upasuaji.

Hiki ni chumba ambacho mgonjwa anapumzika baada ya upasuaji katika chumba hiki mgonjwa uangaliwa zaidi na kupewa huduma zote mpaka pale atakapopona na kurudia kwenye hali yake ya kawaida kwenye chumba hiki panapaswa kuwepo na gasi ya oxygen, maji ya kutosha kwa ajili ya mgonjwa mgonjwa anapaswa  kuwa makini ili kuepuka matatizo baada ya upasuaji kama vile kuishiwa damu na mengine kama hayo.

 

4.Chumba maalum cha kusafishia vifaa.

Hiki ni chumba ambacho vifaa vyote vinavyotumika wakati wa upasuaji vinasafishiwa kwa hiyo chumba hiki kinapaswa kuwepo kwa maji safi ya sabuni, maji yenye chlorine, maji ya kusuuzia na baada ya kutoa uchafu huu vinapaswa kupelekwa ili kuingizwa na kuua bakteria wote na mtu anayefanya kazi kwenye chumba hiki anapaswa kuwa na Elimu  ya kutosha na awe amesomea kazi hiyo kwa kufanya hivyo wadudu wote wataweza kufa na kuzuiliwa kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

 

5. Chumba cha kubadilishia nguo.

Tukumbuke kuwa kabla ya kuanza upasuaji ni lazima kubadilisha nguo za nyumbani na kuvaa nguo za upasuaji hii ufanyika ili kuzuia kusambaa kwa bakteria kutoka kwa mhudumu kwenda kwa mgonjwa kwa hiyo ndo maana kuna chumba maalum kwa ajili ya kubadilisha nguo



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    2 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    4 Download App zetu hapa ujifunze zaidi    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Ni Nini husababisha kinjwaa kutoa harufu mbaya?
Posti hii inaelezea kuhusiana na sababu zinazosababisha kinjwa au mdomo kutoa harufu mbaya? Soma Zaidi...

image Upungufu wa vyakula vya madini
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vyakula vya madini Soma Zaidi...

image Ugonjwa wa kuharisha na sababu zake.
Kuharisha ni Hali ya kupitisha kinyesi Cha maji chenye damu au kisicho na damu Soma Zaidi...

image Baadhi ya maradhi yanayosababishwa na hali za maisha
Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya maradhi yanayosababishwa na hali za maisha Soma Zaidi...

image Mabadiliko ya Matiti kwa Mama mjamzito
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye Matiti kwa Mama mjamzito, hali hii utokea pale ambapo mama akibeba mimba Kuna mabadiliko kwenye Matiti kama ifuayavyo. Soma Zaidi...

image Jinsi mimba inavyotungwa mpaka mtoto kuingia kwenye mfuko wa uzazi
Post hii inahusu zaidi namna mimba inavyotungwa mpaka mtoto kuingia kwenye mfuko wa uzazi, mimba kutungwa ni kitendo ambapo mbegu za kiume kuungana na yai la kike na kutengeneza zygote. Soma Zaidi...

image Kazi za homoni katika Mzunguko hedhi.
Post hii inahusu zaidi kazi za homoni katika Mzunguko wa hedhi, katika kipindi hiki kuna homoni mbalimbali ambazo ufanya kazi kama tutakavyoona. Soma Zaidi...

image Fahamu Ugonjwa wa kifua kikuu kwa watoto chini ya miaka mitano
Posti hii inaonyesha mambo mbalimbali yanayoweza kusababisha Ugonjwa wa kifua kikuu kwa watoto chini ya miaka mitano. Soma Zaidi...

image Dalili za tetekuwanga
Tetekuwanga (varisela) ni maambukizi ya virusi ambayo husababisha kuwasha, upele kama vile malengelenge. Tetekuwanga huambukiza sana watu ambao hawajapata ugonjwa huo wala kupewa chanjo dhidi yake. Kabla ya chanjo ya kawaida ya tetekuwanga, karibu watu wote walikuwa wameambukizwa walipofika utu uzima. Soma Zaidi...

image Vitu vinavyochochea kuwepo kwa Ugonjwa wa ukimwi.
Posti hii inahusu zaidi vitu ambavyo vinasababisha kuongezeka kwa Ukimwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na baada ya watu kujua Ugonjwa huu na matokeo ila bado ugonjwa unazidi kuongezeka. Soma Zaidi...