Zijue sehemu kuu nne za chumba cha upasuaji
Post hii inahusu zaidi sehemu kuu nne za chumba cha upasuaji, chumba cha upasuaji kina sehemu kuu nne na sehemu hizo ufanya kazi tofauti tofauti kama ifuatavyo.
Sehemu kuu nne za chumba cha upasuaji.
1.sehemu ya kwanza ni sehemu ambayo kila mtu anaweza kuingia kwa kitaalamu huitwa unrestricted zone, hiii sehemu hata ndugu wa mgonjwa wanaweza kukaa na kusubiria mgonjwa wao na nguo za nyumbani uweza kutumika katika sehemu hii na watu hawakatazwi kuingia kwenye sehemu huu kwa ujumla huitwa sehemu ambayo haijafanyiwa usafi unaopaswa kitaalamu.
2.Sehemu ya pili ni sehemu ambapo wahudumu wa afya wanaohusika na upasuaji ubadilisha mavazi yao na kuvaa mavazi rasmi ya kwa ajili ya kazi ya upasuaji kwa hiyo watu wengine hawapaswi kufika sehemu hii sehemu hii huwa karibu sana na uelekea sehemu ya upasuaji kwa hiyo hii sehemu imetengwa na watu hawapaswi kuingia kwa sababu ya kuweza kuingiza wadudu kwenye chumba cha upasuaji na kusababisha madhara mengine ambayo hayakutarajiwa.
3.Sehemu inayofuata ni sehemu ya chumba cha upasuaji chenyewe, katika chumba hiki wahudumu wa afya ndio wanapaswa kuingia na wakiwa wamevaa mavazi rasmi na pia mgonjwa mwenyewe anakuwa na mavazi rasmi na vyombo vyote vya kwenye chumba hiki huwa kwenye hali ya usafi, hiki chumba kinatengewa kwa sababu ya kuzuia wadudu na uchafu mwingine kuingia kwa mgonjwa na kusababisha madhara yasiyotarajiwa kwa mgonjwa.
4.Chumba kingine na cha mwisho ni chumba cha kuhifadhia uchafu , sehemu hii huwa na ndoo tatu na box moja kwa ajili ya kuhifadhia uchafu mbalimbali ndoo ya kwanza huwa na uchafu wa karatasi za kawaida ambayo ina rangi ya kijani, ndoo ya pili ina rangi ya njano ambayo ina uchafu wenye maji maji na ndoo ya tatu ni nyekundu yenye uchafu uliochanganyika na damu na box linakuwa na takataka zenye ncha kali kama vile sindano.
5.Tunapaswa kujua sehemu hizo nne za chumba cha upasuaji ili kuepuka kuingilia chumba hiki endapo tuna wagonjwa na kujua kuwa wanafunzi wanaojifunza mambo ya afya wanapaswa kujua sehemu hizo ili kuepuka hali ya kuleta wadudu na vitu vingine kwa wagonjwa
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 ai web app ๐2 Simulizi za Hadithi Audio ๐3 Dua za Mitume na Manabii ๐4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) ๐5 Kitau cha Fiqh ๐6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
UTAMBUE UGNJWA WA UTI DALILI ZAKE, CHANZO NA TAHADHARI DHIDI YAKE
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...Faida za kiafya za kufunga
Simulizi yetu ya leo tutajifunza kuhusu faida za kiafya za kufunga kwa mtazamo wa kitabibu, kama anavyoeleza daktari. Tutaangalia namna kufunga kunavyoathiri na kusaidia viungo na mifumo mbalimbali ya mwili. Somo letu la leo litahusuโฆ faida za kiafya za kufunga katika figo, moyo, ini, mfumo wa kinga, kisukari, presha ya damu na mmengโenyo wa chakula.
Soma Zaidi...Dua Sehemu ya 02
Zijuwe nyakati ambazo dua inakubaliwa kwa haraka zaidi. Zijuwe nyakati ambazo ukiomba dua hitakubaliwa.
Soma Zaidi...KWA NINI MBU HAWEZI KUAMBUKIZA HIV (UKIMWI)
Tumekusha kuona na kujua kuwa mbu anaweza kuambukiza maradhi mengi na ya virusi kama zika.
Soma Zaidi...