Menu



Zijue sehemu kuu nne za chumba cha upasuaji

Post hii inahusu zaidi sehemu kuu nne za chumba cha upasuaji, chumba cha upasuaji kina sehemu kuu nne na sehemu hizo ufanya kazi tofauti tofauti kama ifuatavyo.

Sehemu kuu nne za chumba cha upasuaji.

1.sehemu ya kwanza ni sehemu ambayo kila mtu anaweza kuingia kwa kitaalamu huitwa unrestricted zone, hiii sehemu hata ndugu wa mgonjwa wanaweza kukaa na kusubiria mgonjwa wao na nguo za nyumbani uweza kutumika katika sehemu hii  na watu hawakatazwi kuingia kwenye sehemu huu kwa ujumla huitwa sehemu ambayo haijafanyiwa usafi  unaopaswa  kitaalamu.

 

2.Sehemu ya pili ni sehemu ambapo  wahudumu wa afya wanaohusika na upasuaji ubadilisha mavazi yao na kuvaa mavazi rasmi ya kwa ajili ya kazi ya upasuaji kwa hiyo watu wengine hawapaswi kufika sehemu hii  sehemu hii huwa karibu sana na uelekea sehemu ya upasuaji kwa hiyo hii sehemu imetengwa na watu hawapaswi kuingia kwa sababu ya kuweza kuingiza wadudu kwenye chumba cha upasuaji na kusababisha madhara mengine ambayo hayakutarajiwa.

 

3.Sehemu inayofuata ni sehemu ya chumba cha upasuaji chenyewe, katika chumba hiki wahudumu wa afya  ndio wanapaswa kuingia na wakiwa wamevaa mavazi rasmi na pia mgonjwa mwenyewe anakuwa na mavazi  rasmi na vyombo vyote vya kwenye chumba hiki huwa kwenye hali ya usafi, hiki chumba kinatengewa kwa sababu ya kuzuia wadudu na uchafu mwingine kuingia kwa mgonjwa na kusababisha madhara yasiyotarajiwa kwa mgonjwa.

 

4.Chumba kingine na cha mwisho ni chumba cha kuhifadhia uchafu , sehemu hii huwa na ndoo tatu na box moja kwa ajili ya kuhifadhia uchafu mbalimbali ndoo ya kwanza huwa na uchafu wa karatasi za kawaida ambayo ina rangi ya kijani, ndoo ya pili ina rangi ya njano ambayo ina uchafu wenye maji maji na ndoo ya tatu ni nyekundu yenye uchafu uliochanganyika na damu na box linakuwa na takataka zenye ncha kali kama vile sindano.

 

5.Tunapaswa kujua sehemu hizo nne za chumba cha upasuaji ili kuepuka kuingilia chumba hiki endapo tuna wagonjwa na kujua kuwa wanafunzi wanaojifunza mambo ya afya wanapaswa kujua sehemu hizo ili kuepuka hali ya kuleta wadudu na vitu vingine kwa wagonjwa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Post File: Download PDF Views 716

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

NAMNA AMBAZO MWILI HUPAMBANA NA MARADHI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
SHUGHULI ZA KILA SIKU

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
DALILI ZA KUTOKA AU KUHARIBIKA KWA MIMBA

Tafiti zinaonesha kuwa karibia asilimia 10% mpaka 25% ya wanawake wanaopata ujauzito, mimba zao hutoka.

Soma Zaidi...
VIZAZI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
afya somo la 10

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
kitabu cha afya

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
KWA NINI MBU HAWEZI KUAMBUKIZA HIV (UKIMWI)

Tumekusha kuona na kujua kuwa mbu anaweza kuambukiza maradhi mengi na ya virusi kama zika.

Soma Zaidi...
afya somo la 15

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
kitabu cha matunda

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...