Namna ya kutunza chumba cha upasuaji


image


Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza chumba cha upasuaji, chumba cha upasuaji ni tofauti na vyumba vingine kwenye hospitali kwa hiyo vinahitaji uangalizi wa hali ya juu sana ili kuepuka aina yoyote ya uchafu kuwepo kwenye chumba hicho, zifuatazo ni namna ya kutunza chumba cha upasuaji.


Namna ya kutunza chumba cha upasuaji.

1.Chumba cha upasuaji kinapaswa kuwa na mjengo wa aina yake , kinapaswa kiwe na hewa maalum inayohitajika, madirisha hayapaswi kuwa wazi yanapaswa walau kubwa na wavu ili kuzuia wadudu au uchafu wowote kuingia hasa wakati wa upasuaji na wavu huo ufanyiwe usafi mara kwa mara, pia panakuwepo na sehemu mbalimbali kwenye chumba hicho ili kuweza kuwaruhusu wahudumu kufanya kila kitu kwenye sehemu yake.

 

2.Chumba cha upasuaji kinapaswa kuwa kwenye hali ya usafi kwa wakati wote.

 Usafi kwenye chumba hiki unapaswa kufanyika kila siku walau mara mbili na zaidi kutegemeana na hali ya wagonjwa wanaohudumiwa kwenye sehemu hiyo na kila kitu kinapaswa kusafishwa iwe meza, sakafu na kufuta mavumbi kwenye sehemu mbalimbali na ikitokea labda kuna damu yoyote imetoka kwa mgonjwa inapaswa kutolewa mda huo huo na sehemu hiyo inapaswa kusafishwa na kemikali ambayo inaweza kuua wadudu wote kwa hiyo kemikali inapaswa iwe na nguvu sana.

 

3. Kutunza vizuri vifaa vilivyomo kwenye chumba cha upasuaji.

Tukumbuke kwamba vifaa vinavyotumika kwenye  chumba hiki uweza kutumika mara nyingi kwa hiyo usafishwa kwa utaalamu wote mpaka wadudu wanaungua wote na kuweza kutumika tena kwa mgonjwa mwingine kwa hiyo vinapaswa kubaki kwenye hali ya usafi wa hali ya juu sana ili kuweza kuepuka Maambukizi. Kwa hiyo mtunza vifaa na msafishaji wa vifaa wanapaswa kuwa na elimu ya kutosha kwa kazi hiyo ili kuzuia kusambaa kwa maambukizi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.

 

4.Chumba cha upasuaji kinapaswa kwa na kila aina ya nguo zinazotumika wakati wa upasuaji.

Nguo zenyewe ni pamoja na kofia inayozuia nywele zisianguke kwenye mwili wa mgonjwa wakati wa upasuaji, maski inayozuia uchafu wowote kutoka puani wakati wa kupiga chafya na uchafu kutoka mdomoni, gauni linazuia uchafu wowote kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa wahudumu inawezekana kuwa ni damu au majimaji yoyote, gloves ambazo zinazuia kugusa damu au majimaji ya wagonjwa ambayo yanaweza kuwa na virusi vinavyoweza kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mhudumu au kwa mhudumu kwenda kwa mgonjwa.

 

5.Kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa katika chumba cha upasuaji mgonjwa anayeingia pengine uweza kupasuliwa sehemu kubwa sana na ni rahisi wadudu wanaweza kuingia kwa namna moja au nyingine kwa hiyo wakiingia wanaweza kusababisha madhara makubwa zaidi kuliko ya kwanza kwa hiyo chumba hiki uwekwa kwenye hali ya juu kwa usafi na wahudumu wa hapo wanapaswa kuwa na maarifa makubwa kwa hiyo ni vizuri na haki kukiweka chumba hiki kwenye hali ya juu ya usafi.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    3 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    4 Jifunze Fiqh    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Asili ya Madini ya shaba
Posti hii inahusu zaidi asili ya madini ya Shaba, ni sehemu ambapo madini ya Shaba yanaweza kupatikana ni katika mimea na wanyama Soma Zaidi...

image Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyekunywa sumu
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyekunywa sumu Soma Zaidi...

image Ugonjwa wa bakteria unaoambukizwa na kupe.
Ugonjwa wa bakteria unaoambukizwa na kupe ambao husababisha dalili kama za mafua. Dalili na ishara za Ugonjwa huu ni kati ya kuumwa na mwili kidogo hadi homa kali na kwa kawaida huonekana ndani ya wiki moja au mbili baada ya kuumwa na kupe. Njia bora ya kuzuia maambukizi haya ni kuepuka kuumwa na kupe. Dawa za kuua tiki, ukaguzi wa kina wa mwili baada ya kuwa nje na uondoaji sahihi wa kupe hukupa nafasi nzuri ya kuepuka Maambukizi ya bakteria huyu. Soma Zaidi...

image Zijue faida za mate mdomoni
Post hii inahusu zaidi umuhimu wa mate mdomoni, mate ni majimaji ambayo hukaa mdomoni na husaidia katika kazi mbalimbali mdomoni. Soma Zaidi...

image Ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine. Soma Zaidi...

image Signs and symptoms of pregnancy.
In fact there is a lot of signs and symptoms of pregnancy a mother experiences throughout pregnant. These signs may start to be revealed immediately after conception or in the first week after conception. A term pregnancy is traditionally calculated by midwives as 9 months and 7 days or 120 days or 40 weeks but they all mean one thing. These signs are divided into three trimesters three months per each trimester because a term pregnancy is having nine months. Soma Zaidi...

image Upungufu wa damu unaosababishwa na minyoo.
Post hii inahusu zaidi upungufu wa damu unaosababishwa na minyoo dalili zake na namna ya kumsaidia mgonjwa mwenye tatizo hilo. Soma Zaidi...

image Kazi za homoni katika Mzunguko hedhi.
Post hii inahusu zaidi kazi za homoni katika Mzunguko wa hedhi, katika kipindi hiki kuna homoni mbalimbali ambazo ufanya kazi kama tutakavyoona. Soma Zaidi...

image Hatua tatu anazozipitia mgonjwa wa tauni
Posti hii inahusu zaidi njia au hatua tatu muhimu anazopitia Mgonjwa wa gauni, kuanzia kwa Maambukizi mpaka kwenye hatua ya mwisho hasa kama Ugonjwa huu haujatibiwa mapema. Soma Zaidi...

image Sababu za kutokea kwa maumivu ya jino
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za kutokea kwa maumivu ya jino Soma Zaidi...