Namna ya kutunza chumba cha upasuaji

Namna ya kutunza chumba cha upasuaji

Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza chumba cha upasuaji, chumba cha upasuaji ni tofauti na vyumba vingine kwenye hospitali kwa hiyo vinahitaji uangalizi wa hali ya juu sana ili kuepuka aina yoyote ya uchafu kuwepo kwenye chumba hicho, zifuatazo ni na

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Namna ya kutunza chumba cha upasuaji.

1.Chumba cha upasuaji kinapaswa kuwa na mjengo wa aina yake , kinapaswa kiwe na hewa maalum inayohitajika, madirisha hayapaswi kuwa wazi yanapaswa walau kubwa na wavu ili kuzuia wadudu au uchafu wowote kuingia hasa wakati wa upasuaji na wavu huo ufanyiwe usafi mara kwa mara, pia panakuwepo na sehemu mbalimbali kwenye chumba hicho ili kuweza kuwaruhusu wahudumu kufanya kila kitu kwenye sehemu yake.

 

2.Chumba cha upasuaji kinapaswa kuwa kwenye hali ya usafi kwa wakati wote.

 Usafi kwenye chumba hiki unapaswa kufanyika kila siku walau mara mbili na zaidi kutegemeana na hali ya wagonjwa wanaohudumiwa kwenye sehemu hiyo na kila kitu kinapaswa kusafishwa iwe meza, sakafu na kufuta mavumbi kwenye sehemu mbalimbali na ikitokea labda kuna damu yoyote imetoka kwa mgonjwa inapaswa kutolewa mda huo huo na sehemu hiyo inapaswa kusafishwa na kemikali ambayo inaweza kuua wadudu wote kwa hiyo kemikali inapaswa iwe na nguvu sana.

 

3. Kutunza vizuri vifaa vilivyomo kwenye chumba cha upasuaji.

Tukumbuke kwamba vifaa vinavyotumika kwenye  chumba hiki uweza kutumika mara nyingi kwa hiyo usafishwa kwa utaalamu wote mpaka wadudu wanaungua wote na kuweza kutumika tena kwa mgonjwa mwingine kwa hiyo vinapaswa kubaki kwenye hali ya usafi wa hali ya juu sana ili kuweza kuepuka Maambukizi. Kwa hiyo mtunza vifaa na msafishaji wa vifaa wanapaswa kuwa na elimu ya kutosha kwa kazi hiyo ili kuzuia kusambaa kwa maambukizi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.

 

4.Chumba cha upasuaji kinapaswa kwa na kila aina ya nguo zinazotumika wakati wa upasuaji.

Nguo zenyewe ni pamoja na kofia inayozuia nywele zisianguke kwenye mwili wa mgonjwa wakati wa upasuaji, maski inayozuia uchafu wowote kutoka puani wakati wa kupiga chafya na uchafu kutoka mdomoni, gauni linazuia uchafu wowote kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa wahudumu inawezekana kuwa ni damu au majimaji yoyote, gloves ambazo zinazuia kugusa damu au majimaji ya wagonjwa ambayo yanaweza kuwa na virusi vinavyoweza kutoka kwa mgonjwa kwenda kwa mhudumu au kwa mhudumu kwenda kwa mgonjwa.

 

5.Kwa hiyo tunapaswa kujua kuwa katika chumba cha upasuaji mgonjwa anayeingia pengine uweza kupasuliwa sehemu kubwa sana na ni rahisi wadudu wanaweza kuingia kwa namna moja au nyingine kwa hiyo wakiingia wanaweza kusababisha madhara makubwa zaidi kuliko ya kwanza kwa hiyo chumba hiki uwekwa kwenye hali ya juu kwa usafi na wahudumu wa hapo wanapaswa kuwa na maarifa makubwa kwa hiyo ni vizuri na haki kukiweka chumba hiki kwenye hali ya juu ya usafi.

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Afya File: Download PDF Views 1635

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

AINA ZA VYAKULA
AINA ZA VYAKULA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Nini maana ya Afya
Nini maana ya Afya

Maana ya afya ni pana sana tofauti na vile ambavyo sisi tunajuwa. Afya inahusisha mambo mengi sana.

Soma Zaidi...
MAANA YA AFYA
MAANA YA AFYA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
YANAYOATHIRI AFYA KUTOKANA NA VIZAZI, FAMILIA NA KURITHI
YANAYOATHIRI AFYA KUTOKANA NA VIZAZI, FAMILIA NA KURITHI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
KITABU CHA MATUNDA
KITABU CHA MATUNDA

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
utaratibu wa lishe
utaratibu wa lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...
MAZINGIRZ
MAZINGIRZ

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...