picha

Dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji.

Posti hii inahusu zaidi Dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji, tukumbuke kuwa mtu aliyefanyiwa upasuaji anakuwa kwenye riski sana ya kupata magonjwa na mambo mengine mbalimbali kwa hiyo kuna dalili zikijitokeza kwa mgonjwa aliyepasuliwa Zinapaswa kuf

Dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji.

1. Kutokwa na damu sehemu iliyopasuliwa.

Hii ni mojawapo ya Dalili ya hatari kwa sababu kwa kawaida sehemu iliyopasuliwa haipaswi kutokwa na damu kama damu ikitoka ni lazima kuiripoti mara moja, wahudumu wa afya wanapaswa kuwa makini na kujaribu kuzuia damu isitoke na ikiendelea kutoka mgonjwa anapaswa kurudishwa kwenye chumba cha upasuaji na pia damu ikiendelea kutoka mgonjwa anapaswa kuwekewa damu nyingine. Kwa kufanya hivyo tunaweza kuzuia kuzimia kwa mgonjwa.

 

2. Kuzimia hii pia ni Dalili ya hatari kwa mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji. Kuzimia utokana na  kupungua kwa damu na maji mwilini, Dalili zake ni pamoja na kubadilika kwa rangi ya vidole na macho kuwa vya njano, presha kushuka, mgonjwa kutotulia , kwa hiyo Dalili za kuzimia inabidi kutambuliwa mapema ili kuweza kumsaidia mgonjwa kwa sababu kuzimia usababisha matatizo kwenye figo, ubongo na moyo.

 

3. Kupungua kwa kiwango cha gasi ya oxygen kwenye damu.hii pia ni Dalili mojawapo ambayo haifai kabisa kwa mgonjwa mwenye upasuaji, hali hii ikitokea mtungi wa hewa ni lazima uwekwe kwa mgonjwa na kuendelea kupima mara kwa mara, hali hii utokea kwa mbambali kwa mfano kusukuma vitu kwenye mfumo wa hewa wakati wa upasuaji, ulimi kuanguka nyuma na kuziba hewa kwa hiyo Mgonjwa anapaswa kuangaliwa na kutambua sababu za kukosa hewa.

 

4. Kuwepo kwa damu au majimaji yoyote kwenye mfumo wa hewa.

Hii pia ni Dalili ya hatari kwa mgonjwa aliyepasuliwa kwa sababu hali hii utokea kwa sababu mgonjwa ukalishwa kwenye mkao mbaya wakati wa upasuaji kwa hiyo maji maji yanaenda kwenye mfumo wa hewa kwa hiyo tunapaswa kumweka mgonjwa kwenye mkao mzuri na wa uhakika ili kuepuka kurudi kwa maji au damu kwenye mfumo wa hewa, kwa hiyo wataalamu wa afya wanapaswa kuepusha hali hii ili kuokoa maisha ya mgonjwa.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/01/17/Monday - 04:22:05 pm Topic: Jifunze Main: Afya File: Download PDF Views 3394

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 web hosting    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

YANAYOATHIRI AFYA KATIKA MAZINGIRZ

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
KITABU CHA MATUNDA

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
ZIJUWE NYANJA KUU 6 ZA AFYA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
kitabu cha kanuni 100 za afya

Zijue kanuni 100 za afya ambazo watu wengi hawazijui. Laiti wangelizijua kwa hakika wangefaidika sana.

Soma Zaidi...
DARASA LA AFYA, AFYA YA UZAZI, MARADHI NA LISHE BORA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
darasa la lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...
Umuhimu wa kupiga push up kiafya

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kupiga push up kiafya, ni mambo au faida zipatikanazo ki afya kwa wapigaji wa push up kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
MAZINGIRA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...