Dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji.
Posti hii inahusu zaidi Dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji, tukumbuke kuwa mtu aliyefanyiwa upasuaji anakuwa kwenye riski sana ya kupata magonjwa na mambo mengine mbalimbali kwa hiyo kuna dalili zikijitokeza kwa mgonjwa aliyepasuliwa Zinapaswa kuf
Dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji.
1. Kutokwa na damu sehemu iliyopasuliwa.
Hii ni mojawapo ya Dalili ya hatari kwa sababu kwa kawaida sehemu iliyopasuliwa haipaswi kutokwa na damu kama damu ikitoka ni lazima kuiripoti mara moja, wahudumu wa afya wanapaswa kuwa makini na kujaribu kuzuia damu isitoke na ikiendelea kutoka mgonjwa anapaswa kurudishwa kwenye chumba cha upasuaji na pia damu ikiendelea kutoka mgonjwa anapaswa kuwekewa damu nyingine. Kwa kufanya hivyo tunaweza kuzuia kuzimia kwa mgonjwa.
2. Kuzimia hii pia ni Dalili ya hatari kwa mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji. Kuzimia utokana na kupungua kwa damu na maji mwilini, Dalili zake ni pamoja na kubadilika kwa rangi ya vidole na macho kuwa vya njano, presha kushuka, mgonjwa kutotulia , kwa hiyo Dalili za kuzimia inabidi kutambuliwa mapema ili kuweza kumsaidia mgonjwa kwa sababu kuzimia usababisha matatizo kwenye figo, ubongo na moyo.
3. Kupungua kwa kiwango cha gasi ya oxygen kwenye damu.hii pia ni Dalili mojawapo ambayo haifai kabisa kwa mgonjwa mwenye upasuaji, hali hii ikitokea mtungi wa hewa ni lazima uwekwe kwa mgonjwa na kuendelea kupima mara kwa mara, hali hii utokea kwa mbambali kwa mfano kusukuma vitu kwenye mfumo wa hewa wakati wa upasuaji, ulimi kuanguka nyuma na kuziba hewa kwa hiyo Mgonjwa anapaswa kuangaliwa na kutambua sababu za kukosa hewa.
4. Kuwepo kwa damu au majimaji yoyote kwenye mfumo wa hewa.
Hii pia ni Dalili ya hatari kwa mgonjwa aliyepasuliwa kwa sababu hali hii utokea kwa sababu mgonjwa ukalishwa kwenye mkao mbaya wakati wa upasuaji kwa hiyo maji maji yanaenda kwenye mfumo wa hewa kwa hiyo tunapaswa kumweka mgonjwa kwenye mkao mzuri na wa uhakika ili kuepuka kurudi kwa maji au damu kwenye mfumo wa hewa, kwa hiyo wataalamu wa afya wanapaswa kuepusha hali hii ili kuokoa maisha ya mgonjwa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina ๐2 Dua za Mitume na Manabii ๐3 Simulizi za Hadithi Audio ๐4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) ๐5 Kitabu cha Afya ๐6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
afya somo la 15
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...Vyumba vidogo vidogo kwenye chumba cha upasuaji
Post hii inahusu zaidi juu ya vyumba vidogo vidogo ambavyo Vimo kwenye chumba cha upasuaji, ingawa chumba cha upasuaji ni kimoja ila kuna vyumba vingine vidogo ambavyo vinatumika kwa kazi mbalimbali kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Faida za kiafya za kufunga
Simulizi yetu ya leo tutajifunza kuhusu faida za kiafya za kufunga kwa mtazamo wa kitabibu, kama anavyoeleza daktari. Tutaangalia namna kufunga kunavyoathiri na kusaidia viungo na mifumo mbalimbali ya mwili. Somo letu la leo litahusuโฆ faida za kiafya za kufunga katika figo, moyo, ini, mfumo wa kinga, kisukari, presha ya damu na mmengโenyo wa chakula.
Soma Zaidi...Sababu za Upungufu wa Nguvu za Kiume
Upungufu wa nguvu za kiume ni hali inayomtokea mwanaume kushindwa kupata au kudumisha nguvu ya uume inayotosha kwa ajili ya tendo la ndoa. Tatizo hili linaweza kuwapata wanaume wa rika tofauti, ingawa huonekana zaidi kadri umri unavyoongezeka. Sababu zake zinaweza kuwa za kiafya, kisaikolojia, kimazingira au mtindo wa maisha. Watu wengi huona aibu kuzungumzia tatizo hili, lakini kitaalamu ni hali inayoweza kutibika endapo chanzo chake kitagunduliwa mapema.
Soma Zaidi...