picha

Dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji.

Posti hii inahusu zaidi Dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji, tukumbuke kuwa mtu aliyefanyiwa upasuaji anakuwa kwenye riski sana ya kupata magonjwa na mambo mengine mbalimbali kwa hiyo kuna dalili zikijitokeza kwa mgonjwa aliyepasuliwa Zinapaswa kuf

Dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji.

1. Kutokwa na damu sehemu iliyopasuliwa.

Hii ni mojawapo ya Dalili ya hatari kwa sababu kwa kawaida sehemu iliyopasuliwa haipaswi kutokwa na damu kama damu ikitoka ni lazima kuiripoti mara moja, wahudumu wa afya wanapaswa kuwa makini na kujaribu kuzuia damu isitoke na ikiendelea kutoka mgonjwa anapaswa kurudishwa kwenye chumba cha upasuaji na pia damu ikiendelea kutoka mgonjwa anapaswa kuwekewa damu nyingine. Kwa kufanya hivyo tunaweza kuzuia kuzimia kwa mgonjwa.

 

2. Kuzimia hii pia ni Dalili ya hatari kwa mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji. Kuzimia utokana na  kupungua kwa damu na maji mwilini, Dalili zake ni pamoja na kubadilika kwa rangi ya vidole na macho kuwa vya njano, presha kushuka, mgonjwa kutotulia , kwa hiyo Dalili za kuzimia inabidi kutambuliwa mapema ili kuweza kumsaidia mgonjwa kwa sababu kuzimia usababisha matatizo kwenye figo, ubongo na moyo.

 

3. Kupungua kwa kiwango cha gasi ya oxygen kwenye damu.hii pia ni Dalili mojawapo ambayo haifai kabisa kwa mgonjwa mwenye upasuaji, hali hii ikitokea mtungi wa hewa ni lazima uwekwe kwa mgonjwa na kuendelea kupima mara kwa mara, hali hii utokea kwa mbambali kwa mfano kusukuma vitu kwenye mfumo wa hewa wakati wa upasuaji, ulimi kuanguka nyuma na kuziba hewa kwa hiyo Mgonjwa anapaswa kuangaliwa na kutambua sababu za kukosa hewa.

 

4. Kuwepo kwa damu au majimaji yoyote kwenye mfumo wa hewa.

Hii pia ni Dalili ya hatari kwa mgonjwa aliyepasuliwa kwa sababu hali hii utokea kwa sababu mgonjwa ukalishwa kwenye mkao mbaya wakati wa upasuaji kwa hiyo maji maji yanaenda kwenye mfumo wa hewa kwa hiyo tunapaswa kumweka mgonjwa kwenye mkao mzuri na wa uhakika ili kuepuka kurudi kwa maji au damu kwenye mfumo wa hewa, kwa hiyo wataalamu wa afya wanapaswa kuepusha hali hii ili kuokoa maisha ya mgonjwa.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jifunze Main: Post File: Download PDF Views 3394

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Nina shida hiyo maumivu chini ya tumbo upande wa kushoto na mkojo wa kahawia sana na unatoa arufu

Kama unapatwa na maumivu ya tumbo na ilhali mkojo ni mchafu, ama una harufu sana, basi post hii ni kwa ajili yako.

Soma Zaidi...
dondoo 100 za Afya

Basi tambua haya;- 61.

Soma Zaidi...
kitabu cha afya

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
DALILI ZA KUTOKA AU KUHARIBIKA KWA MIMBA

Tafiti zinaonesha kuwa karibia asilimia 10% mpaka 25% ya wanawake wanaopata ujauzito, mimba zao hutoka.

Soma Zaidi...
Ukuaji wa mmea

Je wajua kwa nini mmea kama nyasi na miti hukua? Posti hii inahusuΒ  zaidi ukuaji wa mimea katika mazingira yetu kwa sababu watu hawatambui kwamba mimea .ni chanzo cha mahitaji kwa binadamu.

Soma Zaidi...