Menu



Dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji.

Posti hii inahusu zaidi Dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji, tukumbuke kuwa mtu aliyefanyiwa upasuaji anakuwa kwenye riski sana ya kupata magonjwa na mambo mengine mbalimbali kwa hiyo kuna dalili zikijitokeza kwa mgonjwa aliyepasuliwa Zinapaswa kuf

Dalili za hatari kwa aliyefanyiwa upasuaji.

1. Kutokwa na damu sehemu iliyopasuliwa.

Hii ni mojawapo ya Dalili ya hatari kwa sababu kwa kawaida sehemu iliyopasuliwa haipaswi kutokwa na damu kama damu ikitoka ni lazima kuiripoti mara moja, wahudumu wa afya wanapaswa kuwa makini na kujaribu kuzuia damu isitoke na ikiendelea kutoka mgonjwa anapaswa kurudishwa kwenye chumba cha upasuaji na pia damu ikiendelea kutoka mgonjwa anapaswa kuwekewa damu nyingine. Kwa kufanya hivyo tunaweza kuzuia kuzimia kwa mgonjwa.

 

2. Kuzimia hii pia ni Dalili ya hatari kwa mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji. Kuzimia utokana na  kupungua kwa damu na maji mwilini, Dalili zake ni pamoja na kubadilika kwa rangi ya vidole na macho kuwa vya njano, presha kushuka, mgonjwa kutotulia , kwa hiyo Dalili za kuzimia inabidi kutambuliwa mapema ili kuweza kumsaidia mgonjwa kwa sababu kuzimia usababisha matatizo kwenye figo, ubongo na moyo.

 

3. Kupungua kwa kiwango cha gasi ya oxygen kwenye damu.hii pia ni Dalili mojawapo ambayo haifai kabisa kwa mgonjwa mwenye upasuaji, hali hii ikitokea mtungi wa hewa ni lazima uwekwe kwa mgonjwa na kuendelea kupima mara kwa mara, hali hii utokea kwa mbambali kwa mfano kusukuma vitu kwenye mfumo wa hewa wakati wa upasuaji, ulimi kuanguka nyuma na kuziba hewa kwa hiyo Mgonjwa anapaswa kuangaliwa na kutambua sababu za kukosa hewa.

 

4. Kuwepo kwa damu au majimaji yoyote kwenye mfumo wa hewa.

Hii pia ni Dalili ya hatari kwa mgonjwa aliyepasuliwa kwa sababu hali hii utokea kwa sababu mgonjwa ukalishwa kwenye mkao mbaya wakati wa upasuaji kwa hiyo maji maji yanaenda kwenye mfumo wa hewa kwa hiyo tunapaswa kumweka mgonjwa kwenye mkao mzuri na wa uhakika ili kuepuka kurudi kwa maji au damu kwenye mfumo wa hewa, kwa hiyo wataalamu wa afya wanapaswa kuepusha hali hii ili kuokoa maisha ya mgonjwa.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Post File: Download PDF Views 2437

Share On:

Facebook WhatsApp

Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

UGONJWA WA MALARIA NA TAKWIMU ZA ATHARI YAKE KIDUNIA

Malaria ni katika maradhi ambayo husambazwa na na mbu jike aina ya anopheles.

Soma Zaidi...
KITABU CHA MATUNDA

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
afya somo la 10

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
kitabu cha afya

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
UTAMBUE UGNJWA WA UTI DALILI ZAKE, CHANZO NA TAHADHARI DHIDI YAKE

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Madhara ya kutumia tissue au toilet paper

Post hii inahusu zaidi madhara ambayo tunaweza kuyapata katika matumizi ya toilet paper au tisu kwenye sehemu za siri.

Soma Zaidi...
NYANJA ZA AFYA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
VYAKULA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
KITABU CHA MATUNDA

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...