MAWAKALA WA KUSABABISHA NA KUSAMBAZA MARADHI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

MAWAKALA WA KUSABABISHA NA KUSAMBAZA MARADHI

MAWAKALA WA MARADHI (PAHOGEN)
Hawa tumesema ndio mawakala wakubwa wa kuambukiza maradhi. Hawa husababisha maradhi haya ya kuambukiza. Wapo aina nyingi lakini tunaweza kuwagawanya katika bakteria, virus, fungi, protozoa na parasites.

1.Bakteria
Hawa ni vijidudu vidogo sana ambavyo haviwezi kuonekana kwa macho maavu bila ya kutumia hadubini (microscope). Vidudu hivi vina seli moja tu. Wapo bakteria ambao hawasababishi maradhi na wapo a,mbao husababisha maradhi. Bakteria karibia dunia nzima wamejaa na hata sehemu ambazo zana mabarafu bakteria pia wapo. Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa kuna aina zisizopungua 300 za bakteria ambao wanaishi kwenye mdomo wa binadamu. Ila karibia bakteria hawa wote hawana madhara kwetu kwa upande mwengine wengi wao ni msaada na ni faida kwetu.

Mfano mzuri ni kuwa kwenye utumbo mdogo kuna bakteria ambao wanatengeneza vitamini ambavyo ni msaada kwa afya zetu. Pia ijulikane bakteria wengine wana madhara makubwa wakiwa ndani ya miili yetu kwa mfano baktria aina ya tuberculosis hawa husababisha kifua kikuu. Tetanus hawa huleta tetenasi. 2.VIRUSI
Virusi ni vidogo zaidi kuliko hata bakteria. Virusi ni vijidudu vidogo sana ambavyo vyenyewe vina genetic material na protein coat. Genetic material ni chembechembe zinazowafanya waweze kuzaliana. Virusi vinaweza kushi tu kama vipo ndani ya kiumbe hai. Vyenyewe vinaweza kuzaliana kwa kutumia seli za kiumbe hai ambapowamo. Maradhi ya Ukimwi, mafua ni baadhi tu ya maradhi ya virusi.

3.FUNGI
Hawa huwa tumezoea kuwaita fangasi hawa wanakula kwenye seli za kiumbe hai. Mfano mzuri ni uyoga huu ni katika jamii ya viumbe hawa wanaokula kutokana na seli au kiumbe kilichokufa. Kama bakteria hata wadudu hawa wapo wanasababisha maradhi na wengine hawasababishi. Fangasi wa miguuni ni mfano mzuri wa maradhi ya wasudu hawa. Mfano mwengine ni wale wa sehemu za siri wanaopelekea kuchubua kwa koreodani kwa wanaume na madahra menginey wa wanawake.

4.PROTOZOA
Hawa pia ni vijidudu vidogo visivyoonekana kwa macho makavu. Hawa pia wana seli moja tu katika miili yao. Ila hawa ni wakubwa kuliko bakteia. Hawa wanasababishwa magonjwa ambayo yanaongoza kuuwa watu wengi sana dunianii. Kwa mfano malaria husababishwa na vijidudu hivi. Kwaribia watu milioni moja kila mwaka wanakufa kwa malaria katika nchi zilizopo kwenye uoto wa tropic.

5.PARASIT
5.Hawa ni wadudu wanaokula kiumbe hai. Mfano mzuri ni chawa, kupe, mbu na wengineo wenye mfano huu. Wadudu hawa wanajipatia chakula kwa kunyonyo viinilishe kwenye mwili wa kiumbe hai. Hawa wanaweza kuwa nche ya mwili kama chawa au ndani ya mwili kama minyoo.


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Download App yetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Afya File: Download PDF Views 286

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

CHUKUWA TAHADHARI HIZI KWENYE MAZINGIRA ILI KULINDA AFYA YAKO

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Ijue timu ya upasuaji

Posti hii inahusu timu ya upasuaji hii ni timu ambayo inahusika katika chumba cha upasuaji, kwa sababu ya kutunza usafi na usalama chumba hiki kinapaswa juwa na timu ya watu wanne na walio na elimu kuhusu kazi hiyo.

Soma Zaidi...
NJIA AMBAZO MARADHI HUAMBUKIZWA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
TAHADHARI KWENYE VYAKULA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
VIJUE VIDONDA VYA TUMBO, SABABU ZAKE NA DALILI ZAKE

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
YANAYOATHIRI AFYA KATIKA MAZINGIRZ

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
kitabu cha matunda

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
UTAMBUE UGNJWA WA UTI DALILI ZAKE, CHANZO NA TAHADHARI DHIDI YAKE

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...