image

Vyakula vyenye madini kwa wingi

Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya vyakula vyenye madini kwa wingi

VYAKULA VYENYE MADINI KWA WINGI

Kwa kuwa umesha jifunza kazi za madini zilizotajwa hapo juu, basi tambuwa kuwa kuna aina nyingi za madini ambazo baadhi yake zimetajwa hapo juu. Madini haya unaweza kuyapata kwenye mchanganyiko wa vyakula vingi. Lakini kuna vyakula ambavyo madini huwa ni mengi kuliko vyakula vingine. Hapa chini ninakuletea vyakula ambavyo vina madini kwa wingi ambavyo ni:-

 

1. Kwenye mbegu kama mbegu za maboga. Mbegu za maboga zina madini mengi sana. Unaweza kula mbegu za maboga kwa kutafuna, kutumia unga wake kama kiungo cha mboga ama kukaanga na kula kama bisi. Mbegu za maboga na m,begu nyingine zenye mfano wake kama mbegu za matango zina madini kama magnesium, zinc, manganese, copper, selenium, na madini ya phosphorus.

 

2. Kwenye samaki hasa samaki wenye magamba magumu kama kobe (shellfish) jamii ya tondo. Kama umeshawahi kula tondo, utakuwa unaelewa nini klimaamnishwa.kama hutambui nitakujuza. Angalia mfano wa konokono, basi samaki wenye kufanana na konokono wanatembea na majumba yao, ukimshituwa anaingia ndani. Samaki hawa ndio wanaozungumziwa hapa. Samaki hawa wana madini kama selenium, zinc, copper na chuma

 

3. Mboga za majani jamii ya kabichi. Mboga hizi zina madini kama magnesium, potassium, manganese na calcium

 

4. Kwenye nyama hasa nyama za viungo maalumu kama maini na figo. Nyama hizi zina madini kama selenium, zinc, madini ya chuma, na phosphorus.

 

5. Mayai ni moja kati ya vyakula vyema virutubisho vingi sana. Katika mayai kuna madini ya chuma kwa wingi sana, phosphorus, zinc na selenium.

 

6. Maharagwe, maharage ya na madini kama cailcium, magnesium, madini ya chuma, phosphorus,potassium, madini ya shaba na zinc.

 

7. Palachichi, tunda hili lina madini kama magnesium, potasium, manganese na madini ya shaba.

 

8. Maziwa yana madini kama cailcium, potassium, phosphorus, zinc na selenium.

 

9. Viazi mbatat vina madii kama potassium, magnesium, manganese, calcium, madini ya chuma na madini ya shaba.

 

10. Pia madini kama potassium, manganese, shamba na magnesium tunaweza kuyapata kwenye matunda kama, ndizi, fenesi, machungwa, pasheni, nanasi na mapera.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 3188


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Tango (cucumber)
Somo hili linakwenda kukuletea faida za kiafya za kula tango Soma Zaidi...

Faida za kula Palachichi
Palachichi lina virutubisho vingi na vitamini, kula palachichi uiokoe afya yako Soma Zaidi...

matunda
Soma Zaidi...

Faida za kula embe
Somo hili linakwenda kukuletea faida za embe na umuhimu wake kiafya Soma Zaidi...

Faida za kula magimbi (taro roots)
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula magimbi Soma Zaidi...

Ni nini maana ya mlo kamili?
Mlo kamili ni mkusanyiko kuu wa vyakula mbalimba kwa pamoja huimarisha na kuujenga  mwili wa binadamu na wanyama kwa sababu vinaleta virutubishi vyote vinavyohitajika.  Mkusanyiko wa vyakula vinavyotengeneza mlo kamili Kuna majina ya vyakula Soma Zaidi...

Vyakula gani ambavyo sitakiwi kula kama nina pressure ya kupanda
Post hii itakufundisha kwa ufupi vyakula vya kuviepuka kama una presha ya kupanda. Soma Zaidi...

Faida za kula limao
Usiwashangae wanaokula lima, kwa hakika kuna faida kubwa kiafya kula limao, je unazijuwa faida hizo Soma Zaidi...

Vyakula vyenye vitamini C kwa wingi
Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya vyakula vyenye vitamini C kwa wingi Soma Zaidi...

Hizi ndio kazi za madini mwilini mwako
Post huu inakwenda kukupa orodha ya madini muhimu kwa ajili ya afya yako. Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula Kunazi
Soma Zaidi...

Uyoga (mushrooms)
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula uyoga Soma Zaidi...