Vyakula vyenye madini kwa wingi

Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya vyakula vyenye madini kwa wingi

VYAKULA VYENYE MADINI KWA WINGI

Kwa kuwa umesha jifunza kazi za madini zilizotajwa hapo juu, basi tambuwa kuwa kuna aina nyingi za madini ambazo baadhi yake zimetajwa hapo juu. Madini haya unaweza kuyapata kwenye mchanganyiko wa vyakula vingi. Lakini kuna vyakula ambavyo madini huwa ni mengi kuliko vyakula vingine. Hapa chini ninakuletea vyakula ambavyo vina madini kwa wingi ambavyo ni:-

 

1. Kwenye mbegu kama mbegu za maboga. Mbegu za maboga zina madini mengi sana. Unaweza kula mbegu za maboga kwa kutafuna, kutumia unga wake kama kiungo cha mboga ama kukaanga na kula kama bisi. Mbegu za maboga na m,begu nyingine zenye mfano wake kama mbegu za matango zina madini kama magnesium, zinc, manganese, copper, selenium, na madini ya phosphorus.

 

2. Kwenye samaki hasa samaki wenye magamba magumu kama kobe (shellfish) jamii ya tondo. Kama umeshawahi kula tondo, utakuwa unaelewa nini klimaamnishwa.kama hutambui nitakujuza. Angalia mfano wa konokono, basi samaki wenye kufanana na konokono wanatembea na majumba yao, ukimshituwa anaingia ndani. Samaki hawa ndio wanaozungumziwa hapa. Samaki hawa wana madini kama selenium, zinc, copper na chuma

 

3. Mboga za majani jamii ya kabichi. Mboga hizi zina madini kama magnesium, potassium, manganese na calcium

 

4. Kwenye nyama hasa nyama za viungo maalumu kama maini na figo. Nyama hizi zina madini kama selenium, zinc, madini ya chuma, na phosphorus.

 

5. Mayai ni moja kati ya vyakula vyema virutubisho vingi sana. Katika mayai kuna madini ya chuma kwa wingi sana, phosphorus, zinc na selenium.

 

6. Maharagwe, maharage ya na madini kama cailcium, magnesium, madini ya chuma, phosphorus,potassium, madini ya shaba na zinc.

 

7. Palachichi, tunda hili lina madini kama magnesium, potasium, manganese na madini ya shaba.

 

8. Maziwa yana madini kama cailcium, potassium, phosphorus, zinc na selenium.

 

9. Viazi mbatat vina madii kama potassium, magnesium, manganese, calcium, madini ya chuma na madini ya shaba.

 

10. Pia madini kama potassium, manganese, shamba na magnesium tunaweza kuyapata kwenye matunda kama, ndizi, fenesi, machungwa, pasheni, nanasi na mapera.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 4727

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Faida za kiafya za stafeli/soursop

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za stafeli ama soursop

Soma Zaidi...
Faida za kula Tangawizi

tangawizi ni katika viungio vya mboga vyenye faida, pia ni kinywaji, zijuwe leo faida za tangawizi

Soma Zaidi...
Madhara ya mafuta mengi mwilimi

Post hii itakufundisha madhara ya kuwa na mafuta mengi mwilimi

Soma Zaidi...
Limao (lemon)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula limao

Soma Zaidi...
Sio salama kwa mtoto wa umri chini ya mwaka mmoja kupewa asali

Kwa nini hutakiwi kumpa mtoto wa umri wa chini ya mwaka mmoja kumpa asali?

Soma Zaidi...
Dawa ya kiungulia na njia za kuzuia kiungulia

utajifunza njia za kuzuia kiungulia, dalili za kiungulia na dawa ya kutibu kiungulia.

Soma Zaidi...
VYAKULA VYA PROTINI, FATI NA MAFUTA

Je! unatambuwa madhara ya vyakula vya protini na mafuta? ungana nasi kwenye somo hili

Soma Zaidi...
Faida za kula asali

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula asali

Soma Zaidi...