Posti hii inahusu zaidi vyakula ambavyo wanapaswa kutumia watu wenye matatizo ya macho,ni vyakula ambavyo uhimalisha mishipa na sehemu nyingine za jicho na kufanya jicho lisiwe na matatizo kwa sababu tunajua wazi kuwa vyakula ni dawa.
Vyakula kwa wenye matatizo ya macho.
1. Matumizi ya samaki.
Samaki ni mojawapo ya chakula ambacho limependekezwa kutumiwa na wenye matatizo ya macho kwa sababu samaki ina acidi ambayo inaweza kuzuia macho kunyauka kwa hiyo matumizi ya samaki ni muhimu.
2. Mbogamboga za majani.
Matumizi mengi ya mboga za majani usaidia kwa wenye matatizo ya Ugonjwa wa macho kwa sababu kuna wingi wa vitamini C ambavyo usaidia kwenye macho, hasa hasa karoti inapendekezwa saba kutumika.
3. Matumizi ya mayai
Pia matumizi ya mayai ni ya muhimu sana kwa wenye matatizo ya macho kwa sababu mayai yana wingi wa vitamini A ambavyo usaidia sana kwenye watu wa matatizo ya macho.
4. Matumizi ya matunda.
Matumizi ya matunda ni muhimu sana kwa watu wenye matatizo ya macho hasa matunda aina ya zabibu yanapendekezwa sana ili yaweze kutumika kwa wingi na kwa kiasi kikubwa sana.
5. Matumizi ya karanga.
Pia wataalamu wamependekeza karanga kwa watu wenye matatizo ya macho kwa sababu karanga uwa na wingi wa vitamini E ambavyo ni muhimu kwa wenye matatizo ya macho.
6.kwa hiyo katika matumizi ya vyakula mbalimbali ambavyo usaidia kwenye wagonjwa wa macho tunapaswa kupunguza kiasi cha mafuta katika matumizi ya vyakula kwa sababu mafuta yanaweza kusababisha madhara mengine ambayo ni pamoja na kuziba mishipa ya mafuta na kufanya damu kushindwa kufanya kazi au kusafili kwa damu juwa kwa shida.
7.pamoja na kutumia vyakula hivi ni vizuri kwenda hospitalini ili kupata matibabu kama kuna Dalili mojawapo ya ugonjwa wowote wa jicho.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Kitunguu thaumu ni katika viungo vya mboga na chakula.
Soma Zaidi...Zitambue aina zote za vyakule na ufanye maamuzi yaliyo kuwa sahihi katika uandaaji wa chakula chako
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na Faida ambazo anaweza kupata mwanadamu Kama akila bamia Mara kwa mara. Bamia huliwa Kama tunda au Kama mboga pia na husaidia vitu vingi mwilini.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula fyulisi/peach
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula maboga
Soma Zaidi...Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...