Vyakula hatari kwa vidonda vya tumbo, na vyakula salama kwa vidonda vya tumbo

Makala hii inakwenda kufundisha vyakuna na vinjwaji salama anavyopaswa kutumia mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Pia utajifunza vyakula na vinywaji hatari kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo.

Vyakula hatari kwa vidonda vya tumbo, na vyakula salama kwa vidonda vya tumbo

VYAKULA HATARI NA VYAKULA SALAMA KWA VIDONDA VYA TUMBO

Vidonda vya tumbo ni moja kati ya maradhi yanayosumbuwa watu kutokana na kuchelewa kwake kupona hata baada ya kutumia dawa nyingi. Hali hii husababishwa kutokana na kutofata masharti ya vidonda vya tumbo vyema. Mgonjwa anatakiwa kufata masharti, ajuwa ni vyakula vipi atumie na vipi asitumie. Makala hii inakwenda kufundisha vyakuna na vinjwaji salama anavyopaswa kutumia mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Pia utajifunza vyakula na vinywaji hatari kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo.


Pia makala hii itakwenda kukufundisha vyakula ambavyo hutumuka kama dawa kwa ajili ya kutibu maradhi hususan vidonda vya tumbo. Mwisho wa makala hii utaweza kujifyunza ni kwa nini vidonda vingine haviponi, na vidonda sugu vinatokeaje.



Vyakula salama kwa wenye vidonda vya tumbo
1. Kabichi
2. Maepo
3. Karoti
4. Mboga za kijani
5. Asali
6. Kitunguu thaumu



Vyakula salama kwa vidonda vya tumbo pia ni dawa
1. Juisi ya kabichi
Kabihi ni katika mboga ambazo zina vitamini C. vitamini hii pia ni katika antioxidant ambayo husaidia katika kupambana na bakteria aina ya H.pylori ambao ndio chanzo kikuu cha vidonda vya tumbo.



2. Asali
Asali nikatika baadhi ya vyakula ambavyo huhusishwa na matibabu mbalimbali. Asali husaidia kuimarisha afya ya moyo, pia hutumika kama dawa kwenye majeraha na majeraha ya moto ili kuzuia bakteria. Asali inaweza pia kupambana na bakteria wa kusababisha vidonda vya tumbo



3. Kitunguu thaumu.
ni katika viungo vya mboga kama kinavyotumika.lakini pia ni katika tiba za asili ambazo hutumiwa maeneo mengi duniani. Tafiti zinaonyesha kuwa katika kitunguu thaumu kuna chembechembe ambazo husaidia katika kupambana na bakteria aina ya H.pylori ambao ndio chanzo kikuu cha vidonda vya tumbo.



4. Shubiri
Shubiri si katika vyakula ila hutumika sana katika viwanda vya vyakula, urembo na viwanda vya kutengeneza madawa. Shubiri ni katika tiba asili ambazo hutumiwa maeneo mbalimbali duniani. Tafiti zinaonyesha kuwa shubiri lina uwezo wa kuzuia mashambulizi ya bakteria kwenye ngozi. Pia shubiri limeonekana kuwa na uwezo wa kutibu vidonda vya tumbo.



Vyakula hatari kwa vidonda vya tumbo:
1. Maziwa.
Wagonjwa wa vidonda vya tumbo wanatambuwa kuwa akinywa maziwa maumivu yanapunguwa. Hii ni faida, lakini tafiti zinaonyesha kuwa maziwa yanaongeza uzalishwaji na utaji wa tindikali za tumboni. Tindikali hizi zina mchango sana katika kusababisha vidonda vya tumbo

2. Pombe
Unywaji wa pombe unaweza kuathiri na kuharibu kuta za tumbo na utumbo. Hali hii inaweza kuongeza hatari ya kuweza kupata vidonda vya tumbo. Ama inaweza kusababisha hali ya mgonjwa kuwa mbaya zaidi.

3. Kahawa;
Kahawa inaweza kusababisha kuongezeka kwa uzalishwaji wa tindikali za tumboni (stomach acid). tindikal hizi zikizalishwa kwa wingi tumboni zinaweza kuchubuwa ukuta wa tumbo na hatimaye kusababisha vidonda vya tumbo

4. Vyakula vyenye mafuta na fati kwa wingi.
5. Pilipili kali vyema kupunguza kuzitumia
6. Vyakula vyenye chumvi nyingi
7. Vyakula vya kuoka
8. Vyakula vyenye uchachu
9. Wacha kuvuta sigara



SABABU ZA VIDONDA VYA TUMBO SUGU
Vidonda vya tumbo ambavyo haviponi na matibabu huitwa vidonda sugu. Kuna sababu nyingi kwa nini kidonda kinaweza kushindwa kuponya, pamoja na:
1. kutokuchukua dawa kulingana na maelekezo
2. Kuwepo kwa bakteria sugu. Ukweli kwamba aina fulani za H. pylori ni sugu kwa antibiotics (dawa).
3. Matumizi ya mara kwa mara ya tumbaku (sigara)
4. Matumizi ya mara kwa mara ya dawa za kupunguza maumivu - NSAIDs na aspirini ambayo huongeza hatari ya vidonda.
5. Matumizi ya dawa isiyo sahihi. Vidonda vya tumbo vitibiwekutokana na asili. Kama asili ni bakteria kwanz amtu apewe dawa ya kuuwa bakteria.



SABABU NYINGINE
Wakati mwingine, vidonda sugu vinaweza kuwa matokeo ya:
1. Uzalishaji mkubwa wa asidi tumboni,
2. Maambukizo mengine yasiyokuwa ya bakteria aina ya H. pylori
3. Saratani ya tumbo
4. matumizi ya vyakula na vinywaji visivyo salama



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 11734

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Faida kuu 10 za kula matunda na mboga mwilini - kwa nini ni muhumu kula matunda?

Makala hii inakwenda kukutajia sababau kuu 10 ambazo zinaonyesha umuhimu wa kula matunda kiafya. kwa nini kiafya unashauriwa ule matunda na mboga mara kwa mara?

Soma Zaidi...
Faida za kula limao

Usiwashangae wanaokula lima, kwa hakika kuna faida kubwa kiafya kula limao, je unazijuwa faida hizo

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kunywa chai

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kunywa chai

Soma Zaidi...
Vitamini na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi vitamini mbalimbali na kazi zake kwenye mwili,vitamini ufanya kazi mbalimbali kwenye mwili kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Faida za kitunguu thaumu

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kitunguu thaumu

Soma Zaidi...
Matunda yenye vitamini C kwa wingi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu matunda yenye vitamin C kwa wingi

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula maboga

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula maboga

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula mahindi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula mahindi

Soma Zaidi...
Tufaha (apple)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula apple/tufaha

Soma Zaidi...
Faida za kula fyulisi/peach

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula fyulisi/ peach

Soma Zaidi...