picha

Vyakula na vinywaji hatari na vilivyo salama kwa mgonjwa wa kisukari

Hapa utajifunza vyakula hatari kwa mgonjwa wa kisukari, pia utajifunza vyakula salama anavyotakiwa ale mgonjwa wa kisukari, Pia ujajifunza njia za kujikinga na kisukari

Vyakula na vinywaji hatari na vilivyo salama kwa mgonjwa wa kisukari

VYAKULA SALAMA NA HATARI KWA MWENYE KISUKARI
Kisuari ni hali ya mwili kushindwa kudhibiti kiwango cha sukari hivyo kuachia sukari yote kuishia kwenye damu bila ya kuingia kwenye seli ili kutumika maeneo mbalimbali ya mwili. Na hutokea endapo uzalishwaji wa homoni ya insulini utakuwa katika shida. Eidha hutokea kwa sababu homoni ya insulini inayozalishwa si yenye kutosheleza ama mwili wenyewe unashindwa kuitumiahomoni ya insulini. Homoni ya insulin ndio ambayo hudhibiti kiwango cha sukari.



Vipi kisukari hutokea?
Mwili unahitaji sukari kwa ajili ya kuzalisha nishati yaani nguvu. Mwili pia unahifadhi sukari kwa matumizi ya baadaye. Endapo sukari mwilini itakuwa ni nyingi basi homoni ya insulini huzaliwa kwa wingi ili kupunguza sukari iliyozidi n akuihifadhi kwa matumizi yaa baadaye. Na endapo sukari itakuwa ni kidogo mwilili homoni ya insulini huzuiliwa hivyo mwili hutumua sukari iliyohifadhiwa. Kwa kufanya hivi kiwango cha sukari hudhibitiwa.



Sasa endapo kutatokea shida yeyote katika matumizi ya homoni ya insulini mwili utashindwa kuhifadhi sukari pia kuitumia sukari. Hivyo sukari itabakia kwenye damu bila ya kwenda kokote kwa matumizi. Hali hii ikitokea ndipo mtu huambiwa ana kisukari. Kisukari kinaweza kuwa ni kwa muda mfupi kama kwa baadhi ya wajawazito. Pia kinaweza kuwa ni cha kudumu, na hapa tunazungumzia type1 na type 2.



Mtu mwenye kisukari anatakiwa kuwa makini sana katika matumizi ya vyakula na vinywaji. Vinginevyo anaweza kuingia kwenye matatizo makubw aya kiafya. Je unavijuwa vyakula salama kwa nmwemye kisukari? Na je unavijuwa vyakula hatari kwa mwenye kisukari? Endelea na makala hii hadi mwisho:-



VYAKULA SALAMA KWA MWENYE KISUKARI
1. Samaki hasa wale wenye fati kwa wingi kama samlon na sardines
2. Mbogamboga za majani
3. Palachichi
4. Mayai
5. Mbegu za chia
6. Maharagwe
7. Kitunguu thaumu
8. Nyama yandege wafugwao kama kuku
9. Kahawa
10. Vinywaji visivyowekwa sukari
11. Jusi za mbogamboga
12. Usikoboe mahindi, mchele, na mtama
13. Matunda kwa uchache



VYAKULA HATARI KWA MWENYE KISUKARI
1. Nafaka zilizokobolewa
2. Nafaka zilizoongezwa sukari
3. Mikate yenye sukari
4. Nafaka zisizo na kini
5. Mboga zenye chumvi nyingi
6. Mboga zilizoongezwa maziwa
7. Vinywaji vyote vya sukari usitumie mpaka kiwango chako cha sukari kiwe kipo katika udhibiti hata asali epukana nayo kwanza
8. Juisi zilizowekwa sukari ama zenye utamu kama za matunda
9. Vinywaji vya energy (energy drink)
10. Nyama ya kuoka
11. Nyama zenye mafuta mengi
12. Nyama ya ngurue
13. Maziwa fresh
14. Samaki wa kuoka
15. Soda



Njia za kujikinga na kisukari
1. Dhibiti uzito wako. Hakikisha huna uzito w akupitiliza
2. Fanya mazoezi mara kwa mara
3. Kula mlo kamili
4. Punguza misongo ya mawazo
5. Kunywa maji kwa wingi
6. Wacha kuvuta sigara
7. Punguza ama wacha unywaji wa pombe
8. Punguza ulaji wa sukari kwa wingi
9. Pendelea kunywa kahawa
10. Tumia dawa za asili kiasi uwezavyo





                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 2717

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Zabibu (grapefruit)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za zabibu

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula kungumanga/nutmeg

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kungumanga/nutmeg

Soma Zaidi...
utaratibu wa lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...
Faida za kula Karoti

Umeshawahi kula karoti mbichi, ama ya kupikwa, je unazijuwa faida zake? soma makala hii

Soma Zaidi...
Karanga (groundnuts)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula karanga

Soma Zaidi...
Vyakula anavyopaswa kutumia mama mjamzito

Posti hii inahusu zaidi vyakula anavyopaswa kutumia mama mjamzito, mama mjamzito ni mama ambaye amebeba kiumbe ndani kwa hiyo anapaswa kutumia vyakula vyenye virutubisho mbalimbali vitakavyomsaidia mtoto kukua vizuri.

Soma Zaidi...
Faida za kula kachumbari

Posti hii inahusu zaidi faida mbalimbali ambazo anaweza kuzipata mtu anayetumia kachumbari, tunajua wazi kwamba kachumbari ni mchanganyiko wa nyanya, vitunguu maji,kabichi,na pilipili kidogo.

Soma Zaidi...
Faida za kula parachichi

Somo Hili linakwenda kukuletea faida za kula parachichi

Soma Zaidi...
Faida za kula Ukwaju

Zitambue faida kubwa za kula karanga kwa ajili ya afya yako

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula samaki

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula samaki

Soma Zaidi...