Nabii Shu’ayb(a.
Nabii Shu’ayb(a.s) alitumwa kwa watu wa Madian waliokuwa wakikaa pande za pwani ya Shamu (Syria). Watu hawa walikuwa wafanyabiashara wakubwa wa zama hizo. Mji wao ulikuwa katika njia kuu (Highway) ya misafara ya biashara kutoka sehemu mbali mbali za Mashariki ya kati kuelekea pwani ya bahari ya Mediterranean.
Wamadian pamoja na kuwa wafanyabiashara mashuhuri walikuwa na tabia ya kupunja vipimo wakati wa kuuza. Pia walikuwa wababe wakifanya uharibifu katika ardhi, walikuwa majambazi wakipora na kunyang’anya watu mali zao. Vile vile walikuwa washirikina na kuzuia watu kufuata Dini ya Allah(s.w).
Nabii Shu’ayb(a.s) kama walivyofanya Mitume waliomtangulia aliwanasihi watu wake kumwamini na kumuabudu Allah(s.w) ipasavyo katika maisha yao ya kila siku na kusimamisha uadilifu katika jamii.
Na kwa watu wa Madian (tulimpeleka) ndugu yao, Shuaibu. Akasema: “Enyi watu wangu! Mwabuduni Mwenyezi Mungu, nyinyi hamna Mungu ila Yeye. Msipunguze kipimo (cha vibaba) wala (cha) mizani. Mimi nakuoneni mumo katika hali njema (basi msiiharibu kwa kufanya dhulma).Nami nakukhofieni adhabu ya siku (kubwa) hiyo itakayokuzungukeni.” (11:84)
Nabii Shu’ayb(a.s) aliendelea kuwaasa watu wake:
“Wala msikae katika kila njia kuogopesha (watu) na kuwazuilia na Dini ya Mwenyezi Mungu (wale) wenye kuamini, na kutaka kuipotosha Na kumbukeni mlipokuwa wachache, Naye akakufanyeni kuwa wengi (sasa).Na tazamneni jinsi ulivyokuwa mwisho wa waharibifu.” (7:86)HISTORIA YA NABII
Umeionaje Makala hii.. ?
KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake.
Soma Zaidi...Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Ibilis ni katika jamii ya majini aliyekuwa pamoja na Malaika wakati amri ya kumsujudia Adam inatolewa.
Soma Zaidi...Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 15. Hapa utajifunza kuhusu chimbuko la ndoa ya Mtume s.a.w na bi Khadija.
Soma Zaidi...