Nabii Yunus(a.s) Amuomba Allah(s.w) Msamaha

Ndani ya tumbo la samaki, Nabii Yunus(a.

Nabii Yunus(a.s) Amuomba Allah(s.w) Msamaha

Nabii Yunus(a.s) Amuomba Allah(s.w) Msamaha


Ndani ya tumbo la samaki, Nabii Yunus(a.s) akiwa hai na akili timamu aligundua kosa lake la kuwakimbia watu wake bila ya ruhusa kutoka kwa Mola wake. Ilibidi Yunus (a.s) alalame ndani ya tumbo la samaki kumuomba msamaha Mola wake na kuomba msaada wake.



Na (Mtaje) Dhun-Nun (Yunusi) alipoondoka hali amechukiwa, na akadhani ya kwamba hatutatamdhikisha. Basi (alipozongwa)aliita katika giza (akasema):“Hakuna aabudiwaye isipokuwa Wewe Mtakatifu hakika mimi nilikuwa miongoni mwa wenye kudhulumu (nafsi zao).” (21:87)



Allah(s.w) alimsamehe mja wake Yunus(a.s) na kumuokoa katika janga lile kwa kumuelekeza samaki amrudishe pwani na kumtapika.



“Basi tukampokelea (toba na dua yake) na tukamuokoa katika huzuni ile. Na namna hivyo ndivyo tuwaokoavyo walioamini.” (21:88)



Lakini tukamtupa ufukoni (kwa kutapikwa na huyo samaki) hali ya kuwa mgonjwa.” (37:145)



Baada ya kufikishwa pale pwani, Yunus (a.s) alikuwa mgonjwa na dhaifu asiyejiweza kwa lolote. Mola wake alizidi kumrehemu kwa kumuoteshea mti wa mbarikhi ambao aliula ukampa afya ya kumuwezesha kuwarudia watu wake ambao aliwakuta wameshaamini na wanamngojea kwa hamu ili awape mafunzo na maelekezo waweze kumuabudu Mola wao inavyostahiki:



Na tukamuoteshea mmea wa mbarikhi (akawa anakula). (37:146) “Na tulimpeleka kwa (watu) laki moja au zaidi, (wale wale watu wake). Basi wakaamini na tukawastarehesha mpaka muda wao wa kufa.” (37:147-148)



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1557

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana: