image

Mafunzo ya sura zilizochaguliwa

Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Mafunzo ya sura zilizochaguliwa.

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.

  1. Imeangamia mikono ya Abulahab naye amekwisha angamia.
  2. Haitamfaa mali yake wala alivyovichuma (watoto).
  3. (Atakapokufa) Ataingia moto wenye muwako (mkubwa kabisa).
  4. Na mkewe (ni) mchukuzi wa kuni (za fitina).  
  5. (Kana kwamba) Shingoni mwake iko kamba iliyosokotwa (anayechukulia kuni za fitina).

 

 

      Mafunzo ya sura kwa ufupi.

  1. Binaadamu siku zote huamua kumkanusha Mwenyezi Mungu (s.w) kwa kibri na jeuri. 
  2. Mali na watoto havina msaada wowote pindi inapokuja adhabu ya Mwenyezi Mungu (s.w).
  3. Watu waovu na wenye kumuasi Mwenyezi Mungu (s.w) wana mwisho mbaya wa kuishia motoni.
  4. Maadui wa Uislamu na waislamu siku zote hawakati tamaa katika kuzuilia watu kuingia na kuufuata Uislamu.
  5. Uchochezi, fitina na uasi ni miongoni mwa makosa makubwa yenye kuangamiza. 


 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.

  1. Itakapofika Nusura ya Mwenyezi Mungu na Kushinda.
  2. Na ukawaona watu wanaingia katika Dini ya Mwenyezi Mungu makundi makundi.
  3. Basi (hapo) mtakase Mola wako pamoja na kumsifu na umuombe magh’fira (msamaha) hakika Yeye ndiye apokeaye toba.

   

          Mafunzo ya Sura kwa Ufupi.

  1. Nusura na mafanikio hutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w) pekee.
  2. Baada ya nusura na ushindi hatuna budi kumshukuru, kumtukuza na kumuomba msamaha Mwenyezi Mungu (s.w) bila ya kujivuna.
  3. Katika kufanya juhudi, hatuna budi kuchunga na kutii ipasavyo maarisho na makatazo ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake.
  4. Nusura na mafanikio ya kweli huja baada ya juhudi za dhati za kibinaadamu kufanyika na kumtegemea Mwenyezi Mungu (s.w) vilivyo.
  5. Mafanikio ya kweli sio kujilimbikizia mali na anasa za dunia tu, bali ni kuipigania Dini ya Mwenyezi Mungu (s.w) ipasavyo.  

 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.

  1. Sema: Enyi Makafiri.
  2. Siabudu mnachoabudu.
  3. Wala nyinyi hamuabudu ninayemuabudu. 
  4. Wala sitaabudu mnachoabudu.
  5. Wala nyinyi hamtaabudu ninayemuabudu (mimi).
  6. Nyinyi mna dini yenu na mimi nina dini yangu.

 

                  Mafunzo ya Sura kwa Ufupi.

  1. Dini ni utaratibu wowote ule wa maisha anaoufuata mtu.
  2. Kuna dini nyingi hapa Ulimwenguni, Ukafiri nao ni dini.
  3. Hakuna uwezekano wa mwanaadamu kufuata dini (utaratibu wa maisha) za ya moja kwa wakati moja, Uislamu na mifumo mingine.
  4. Waislamu wa kweli ni wale wasiochanganya haki na batili kwa kuwahofia makafiri.
  5. Ni wajibu kuitangaza haki kwa wengine bila kuhofia chuki na uadui wao dhidi ujumbe uliowapa.


 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.

  1. Hakika tumekupa kheri nyingi.
  2. Basi swali kwa ajili ya Mola wako na uchinje (kwa ajili yake pia).
  3. Hakika adui yako ndiye atakayekuwa mkiwa (atakatikiwa na kila kheri).

 

Mafunzo ya Sura kwa Ufupi.

  1. Mafanikio hayapimwi kwa wingi wa mali na watoto, bali ni kuridhiwa na Mwenyezi Mungu (s.w).
  2. Hakuna neema kubwa kama kujaaliwa kuupokea Uislamu, kuuelewa, kuufuata vilivyo na kuufikisha kwa wengine.
  3. Hatuna budi kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w) peke yake ipasavyo na kufanya kila jambo kwa ajili yake tu.
  4. Maadui na Wapinzani wa Uislamu ndiyo wenye kupata khasara na kufedheheka duniani na Akhera pia.
  5. Ushindi na mafanikio hupatikana kwa waislamu baada ya kutii na kufuata maamrisho ya Uislamu vilivyo.

 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.

  1. Je, Unajua yule anayekadhibisha dini (asiyeamini malipo ya Akhera)?
  2. Huyu ni yule anayemnyanyasa yatima.
  3. Wala hajihimizi (yeye wala wengine katika) kuwalisha maskini.
  4. Basi adhabu kali itawathubutikia wanaoswali.
  5. Ambao wanapuuza (maamrisho ya) swala zao.
  6. Ambao hufanya riyaa (ya kujionyesha kwa watu).
  7. Nao hunyima misaada (midogomidogo kwa wanaohitajia). 



 

Mafunzo ya Sura kwa Ufupi.

  1. Imani katika Uislamu hudhihirishwa katika matendo ya mtu na sio kauli au maneno tu.
  2. Kuwadhulumu, kuwasimanga au kuwatendea uovu wowote mayatima na wenye shida ni katika makosa makubwa.
  3. Swala ni lazima itekelezwe kwa kuzingatia ipasavyo nguzo, sharti zake pamoja na khushui (unyenyekevu).
  4. Kutenda jambo lolote kwa ajili ya kupata radhi za Mwenyezi Mungu (s.w) ndio uhai wa ibada ya muumini.
  5. Maisha ni jambo la kijamii ambalo linahitajia watu kuishi pamoja kwa kusaidiana inapobidi.
  6. Muumini wa kweli ni yule aliyemwepesi kutoa misaada kwa wanaadamu wenzie na mwenye kujali matatizo ya wengine yanapowapata.

 

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.

  1. Ili kuwafanya Maqureish waendelee.
  2. Waendelee na safari zao za wakati wa kusi (kwenda Yemen) na wakati wa kaskazi (kwenda Sham ndiyo maana tukajaalia jeshi la ndovu kushindwa).
  3. Basi na wa muabudu Bwana wa Nyumba hii (Al-Kaaba).
  4. Ambaye amewalisha (wakati wa) katika njaa na anawapa amani (wakati wa) katika khofu.

 

Mafunzo kwa Ufupi.

  1. Kwa hakika anayelisha na kulinda ni Mwenyezi Mungu (s.w) peke yake.
  2. Amani, Usalama na Ustawi wa kweli wa jamii hutokana na kushikamana na amri za Mwenyezi Mungu (s.w).
  3. Shukrani za kweli kwa Mwenyezi Mungu (s.w) ni kumuabudu ipasavyo.
  4. Maingiliano ya Mataifa kibiashara ni katika neema za Mwenyezi Mungu (s.w).





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1155


Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰2 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Mapambano ya Mtume Muhammad dhidi ya Wanafiki na hila zao Madina
Soma Zaidi...

Shukurani za Nabii Ibrahiim(a.s) kwa Allah(s.w)
Kwa neema hii ya kuruzukiwa watoto wawili - Ismail na Is- haqa(a. Soma Zaidi...

Imam Nasai na kitabu cha Sunan
Soma Zaidi...

Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)
Tukirejea Qur’an (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a. Soma Zaidi...

Mjadala juu ya ndoa ya Mtume Muhammad s.a.w na bi Khadija.
Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 16. Hapa utajifunza maandalizi wa mjadala wa ndoa hizi. Soma Zaidi...

CHANZO CHA VITA VYA VITA VYA AL-FIJAR NA ATHARI ZAKE
MAPIGANO YA AL-FIJAR (MAPIGANO YA UOVU). Soma Zaidi...

Hatua mbili kuu za kushuka kwa Quran
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Hawa ndio waaasi wakwanza wa Dola ya kiislamu wakati wa makhalifa
Soma Zaidi...

HISTORIA NA VISA VYA MITUME, MANABII NA WATU WEMA WALIOTAJWA KWENYE QURAN
Soma Zaidi...

Mtume amezaliwa mwaka gani?
Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake. Soma Zaidi...

Musa(a.s) Kuwaongoza Bani Israil Hadi Palestina
Baada ya matukio haya ndipo Musa(a. Soma Zaidi...

Msimamo wa Nabii Hud(a.s) Dhidi ya Makafiri wa Kaumu Yake
Pamoja na kwamba alipingwa na nguvu za Dola ya makafiri wa kaumu yake, Mtume Hud(a. Soma Zaidi...