picha

Mafunzo yatokanayo na hijrah ya mtume na maswahaba wake

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Mafunzo yatokanayo na Hijrah ya Mtume (s.a.w) na Maswahaba wake.

  1. Hatuna budi kutunza na kurejesha amana za watu kwa wenyewe bila kujali uadui wao kwetu.

 

  1. Waislamu hawanabudi kuweka mipango na mikakati madhubuti juu ya namna ya kutekeleza mambo yao kabla ya utekelezaji wake.

 

  1. Waislamu hawana budi kuchukua tahadhari katika kuendesha harakati za kidini kwa kuzingatia kuwa dini ya Uislamu ina maadui wengi.

 

  1. Nusura ya Allah (s.w) na Ushindi hupatikana tu baada ya kufanyika jitihada za dhati katika kuusimamisha Uislamu katika jamii na kumtegemea yeye pia.

 

  1. Waislamu wanalazimika kufanya jitihada ya dhati ya kumuabudu Allah (s.w) ipasavyo kwa kila kipengele cha maisha yao, kama mazingira yatakuwa ndio kikwazo hawanabudi kuhama (kuhajiri) kwenda sehemu (ardhi) yenye wasaa.

Rejea Qur’an (4:97-99).

 

  1. Kuhajiri (kuhama) kwa ajili ya Uislamu sio ukimbizi, bali ni katika mikakati na mipango ya kwenda kujiimarisha huko na hatimaye kuja kukomboa sehemu mlikotoka.

 

  1. Kutokana na Hijrah ya Mtume (s.a.w), tunajifunza kuwa waislamu wote ni ndugu mmoja bila ya kujali kabila, rangi, taifa, n.k.

 

  1. Uislamu siku zote hauwezi kusimama katika jamii mpaka waislamu tuwe tayari kujitoa muhanga kwa mali na nafsi zetu kadri ya uwezo wetu.

 

  1. Ni haramu kwa muislamu kuishi katika nchi ya kikafiri au utawala wa kikafiri isipokuwa, itakapokuwepo jitihada ya kuundoa ukafiri na kuutawalisha Uislamu au yatakapokuwepo maandalizi ya kuhama sehemu hiyo

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Views 2070

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰2 web hosting     πŸ‘‰3 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)

Tukirejea Qur’an (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a.

Soma Zaidi...
Historia ya kujengwa kwa Alkabah (Maka)

Kama tulivyoona katika maisha ya Mtume Ibrahim(a.

Soma Zaidi...