Mafunzo yatokanayo na hijrah ya mtume na maswahaba wake

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Mafunzo yatokanayo na Hijrah ya Mtume (s.a.w) na Maswahaba wake.

  1. Hatuna budi kutunza na kurejesha amana za watu kwa wenyewe bila kujali uadui wao kwetu.

 

  1. Waislamu hawanabudi kuweka mipango na mikakati madhubuti juu ya namna ya kutekeleza mambo yao kabla ya utekelezaji wake.

 

  1. Waislamu hawana budi kuchukua tahadhari katika kuendesha harakati za kidini kwa kuzingatia kuwa dini ya Uislamu ina maadui wengi.

 

  1. Nusura ya Allah (s.w) na Ushindi hupatikana tu baada ya kufanyika jitihada za dhati katika kuusimamisha Uislamu katika jamii na kumtegemea yeye pia.

 

  1. Waislamu wanalazimika kufanya jitihada ya dhati ya kumuabudu Allah (s.w) ipasavyo kwa kila kipengele cha maisha yao, kama mazingira yatakuwa ndio kikwazo hawanabudi kuhama (kuhajiri) kwenda sehemu (ardhi) yenye wasaa.

Rejea Qur’an (4:97-99).

 

  1. Kuhajiri (kuhama) kwa ajili ya Uislamu sio ukimbizi, bali ni katika mikakati na mipango ya kwenda kujiimarisha huko na hatimaye kuja kukomboa sehemu mlikotoka.

 

  1. Kutokana na Hijrah ya Mtume (s.a.w), tunajifunza kuwa waislamu wote ni ndugu mmoja bila ya kujali kabila, rangi, taifa, n.k.

 

  1. Uislamu siku zote hauwezi kusimama katika jamii mpaka waislamu tuwe tayari kujitoa muhanga kwa mali na nafsi zetu kadri ya uwezo wetu.

 

  1. Ni haramu kwa muislamu kuishi katika nchi ya kikafiri au utawala wa kikafiri isipokuwa, itakapokuwepo jitihada ya kuundoa ukafiri na kuutawalisha Uislamu au yatakapokuwepo maandalizi ya kuhama sehemu hiyo

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1686

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 web hosting    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

tarekh 08

KULELEWA NA MAMA YAKE ALIPOFIKA MIAKA MINNEMtume (s.

Soma Zaidi...
Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga

Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.

Soma Zaidi...
Maana ya kusimamisha uislamu katika dini

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mafunzo kutokana na vita vya badri

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
tarekh

MAPIGANO YA AL-FIJAR (MAPIGANO YA UOVU).

Soma Zaidi...