Mafunzo yatokanayo na Hijrah ya Mtume (s.a.w) na Maswahaba wake.
Hatuna budi kutunza na kurejesha amana za watu kwa wenyewe bila kujali uadui wao kwetu.
Waislamu hawanabudi kuweka mipango na mikakati madhubuti juu ya namna ya kutekeleza mambo yao kabla ya utekelezaji wake.
Waislamu hawana budi kuchukua tahadhari katika kuendesha harakati za kidini kwa kuzingatia kuwa dini ya Uislamu ina maadui wengi.
Nusura ya Allah (s.w) na Ushindi hupatikana tu baada ya kufanyika jitihada za dhati katika kuusimamisha Uislamu katika jamii na kumtegemea yeye pia.
Waislamu wanalazimika kufanya jitihada ya dhati ya kumuabudu Allah (s.w) ipasavyo kwa kila kipengele cha maisha yao, kama mazingira yatakuwa ndio kikwazo hawanabudi kuhama (kuhajiri) kwenda sehemu (ardhi) yenye wasaa.
Rejea Qur’an (4:97-99).
Kuhajiri (kuhama) kwa ajili ya Uislamu sio ukimbizi, bali ni katika mikakati na mipango ya kwenda kujiimarisha huko na hatimaye kuja kukomboa sehemu mlikotoka.
Kutokana na Hijrah ya Mtume (s.a.w), tunajifunza kuwa waislamu wote ni ndugu mmoja bila ya kujali kabila, rangi, taifa, n.k.
Uislamu siku zote hauwezi kusimama katika jamii mpaka waislamu tuwe tayari kujitoa muhanga kwa mali na nafsi zetu kadri ya uwezo wetu.
Ni haramu kwa muislamu kuishi katika nchi ya kikafiri au utawala wa kikafiri isipokuwa, itakapokuwepo jitihada ya kuundoa ukafiri na kuutawalisha Uislamu au yatakapokuwepo maandalizi ya kuhama sehemu hiyo
Kwa kuzingatia aya zote tulizozipitia juu ya wanafikitunaweza kutoa majumuisho ya sifa za wanafiki kama ifuatavyo:- (1)Hutenda kinyume cha imani wanaodai kuwa nayo.