image

Mbinu Alizozitumia Nabii Shu’ayb(a.s) Katika Kufikisha Ujumbe Wake

Mbinu Alizozitumia Nabii Shu’ayb(a.s) Katika Kufikisha Ujumbe Wake

Mbinu Alizozitumia Nabii Shu’ayb(a.s) Katika Kufikisha Ujumbe Wake


Katika kuwafikishia ujumbe watu wake,Nabii Shu’ayb alifanya yafuatayo:



Kwanza, kuwafahamisha watu wake kwa uwazi kuwa yeye ni
Mtume wa Allah(s.w) aliye mfano wa kuigwa:




Akasema: “Enyi watu wangu! Mnaonaje kama ninayo dalili inayotokana na Mola wangu na ameniruzuku riziki njema (ya Utume) kutoka kwake (nitaacha haya, nishike upotofu wenu)? Wala sipendi kukukhalifuni nikafanya yale ninayokukatazeni. Sitaki ila kutengeneza, kiasi ninavyoweza. Na sipati kuwezeshwa haya ila na Mwenyezi Mungu (Mwenyewe). Kwake ninategemea, na Kwake naelekea.” (11:88)



Pili, aliwahofisha adhabu kali ya Allah(s.w) iwapo watakataa kumwamini na kumfuata.

Na kwa Madiani (tulimtuma) ndugu yao, (Nabii) Shu’ayb, naye akasema: “Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu na iogopeni siku ya akhera wala msende katika ardhi mkifisidi.” (29:36)



Tatu,aliwatahadharisha watu wake na adhabu ya Allah(s.w)
iliyowafika kaumu zilizopita za akina ‘Ad, Thamud na kaumu Lut.



“Na enyi watu wangu! Kukhalifiana nami kusikupelekeeni yakakusibuni kama yaliyowasibu watu wa Nuh au watu wa Saleh na watu wa Luti si mbali nanyi.” (Karibuni hivi wameangamizwa; na nchi zao ziko karibu na nyinyi pia). (11:89)



Nne, aliwatumainisha watu wa Madian kuwa endapo wataomba msamaha kwa Allah(s.w) na kutubu juu ya makosa yao, Allah(s.w) atawasamehe na kuwaepusha na balaa lililowafika watu wa kaumu za Mitume waliotangulia.



“Na ombeni msamaha kwa Mola wenu (kwa yaliyopita), kisha tubuni kwake . Hakika Mola wangu ni Mwenye kurehemu na Mwenye kuwapenda (waja Wake).” (11:90)



Tano, aliwaonyesha msimamo na utegemezi wake juu ya
Allah(s.w).

“Na enyi watu wangu! Fanyeni (mtakayo) kwa tamkini yenu; na mimi pia ninafanya (yangu kwa tamkini yangu). Karibuni hivi mtajua ni nani itakayemfikia adhabu ifedheheshayo na ni nani aliye muongo. Na ngojeeni; mimi pia ninangoja pamoja nanyi.” (11:93)



“Bila shaka tumemtungia Mwenyezi Mungu uwongo ikiwa tutarudi katika mila yenu baada ya Mwenyezi Mungu kutuokoa nayo. Wala haiwi kwetu sisi kurejea mila hiyo. Lakini akitaka (jambo) Mwenyezi Mungu, Mola wetu, (huwa). Mola wetu amekienea kila kitu kwa ilimu yake. Kwa Mwenyezi Mungu tunategemea. Mola wetu! Hukumu baina yetu na baina ya wenzetu (hawa) kwa haki, nawe ndiye mbora wa wanaohukumu.” (7:89)



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 436


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

tarekh 4
KUANGAMIZWA KWA JESHI LA TEMBOTukio la pili ni lile tukio la tembo, na ilikuwa hivi:- Kiongozi mmoja wa kiyemeni aliyetambulika kwa jina la Abrah aliona waarabu kutoka maeneo mbalimbali wanafunga misafara kuelekea Makkah kwa lengo la kwenda kuhiji. Soma Zaidi...

HISTORIA YA KUJENGWA UPYA KWA AL-KA'BAH (NYUMBA TUKUFU YA ALLAH)
KUJENGWA UPYA KWA AL-KA’ABAHItambulike kuwa Al-ka’abah ndio mjengo wa kwanza kujengwa duniani. Soma Zaidi...

Kifo cha Khalia Uthman kilivyotokea
Soma Zaidi...

HISTORIA YA WATU WAOVU WAKIOTAJWA KWENYE QURAN
Soma Zaidi...

Yunus(a.s) Kulingania Uislamu kwa Watu Wake
Nabii Yunus(a. Soma Zaidi...

Mtume alipoanza kulingania uislamu na changamoto alizokumbana nazo kutoka kwa maadua wa uislamu
7. Soma Zaidi...

Kuchimbwa upya kwa kisima cha Zamzam
Sura na historia ya mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 3.Hapa utajifunza kuhusu kufukuliwa kwa kisima cha Zamzam baada ya kufukiwa muda mrefu. Soma Zaidi...

Historia ya Vijana wa Pangoni
Makafiri wa Kiquraish walikuwa na tabia ya kumghasi Mtume(s. Soma Zaidi...

Upinzani Dhidi ya Dola ya Kiislamu Wakati wa Makhalifa
Soma Zaidi...

Imam Abu Daud na Sunan Abi Daud
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII SULEIMAN
Soma Zaidi...

Mtume Muhammad s.a.w analelewa na Babu yako ikiwa na umri wa miaka 6
Sura na historia ya Mtume Muhammad s.a. w sehemu ya 9. Soma Zaidi...