Navigation Menu



image

Kibri cha Ibilis na Uadui Wake Dhidi ya Binadamu

Ibilis ni katika jamii ya majini aliyekuwa pamoja na Malaika wakati amri ya kumsujudia Adam inatolewa.

Kibri cha Ibilis na Uadui Wake Dhidi ya Binadamu

Kibri cha Ibilis na Uadui Wake Dhidi ya Binadamu


Ibilis ni katika jamii ya majini aliyekuwa pamoja na Malaika wakati amri ya kumsujudia Adam inatolewa. Iblis alitarajiwa kutii

amri hiyo ya Mola wake pamoja na Malaika, lakini hakufanya hivyo bali alitakabari kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:




“Basi Malaika wakatii (amri ya kusujudu) wote pamoja isipokuwa Ibliis, akajivuna na akawa katika makafiri.” (Allah) akamuuliza: “Ewe Ibilis! Kipi kilichokuzuia kumtii yule niliyemuumba kwa mikono yangu?” Je! Umetakabari au umo miongoni mwa wakubwa (kweli)? (38:73-75)




Akasema (Ibilis katika kujibu): “Mimi ni bora kuliko yeye, kwani mimi umeniumba kwa moto na yeye umemuumba kwa udongo” (38:76)

Ibilis badala ya kuzingatia amri ya Mola wake na kutii, amepeleka fikra zake kwenye asili ya umbile la Adam(a.s) na kuanza kujifananisha naye na kuona kuwa asili ya umbile lake ni bora kuliko ile asili ya umbile la Adam(a.s). Hatakama ingelikuwa kweli kuwa moto ni bora kuliko udongo, Iblis asingelipaswa kukataa kumsujudia Adam(a.s) kwa sababu si Adamu aliyetaka asujudiwe, bali aliyetoa amri ya kumsujudia Adam ni Allah(s.w) ambaye ni Muumba wa Adam na Ibilis.

Baada ya Ibilis kuvunja amri ya Mola wake kwa takaburi kiasi hicho, alilaaniwa na kubaidishwa (kufukuzwa) na rehema za Mola wake:



(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo kwani umetengwa na rehema. Na hakika laana yangu itakuwa juu yako mpaka siku ya malipo.”(38:77-78)

Badala ya Ibilis kukiri kosa lake na kumuelekea Mola wake kwa toba ya kweli, alielekeza lawama zake kwa Adam(a.s) na kuapa mbele ya Allah (s.w) kuwa atalipiza kisasi kwa Adam(a.s) na kizazi chake kwa kukipoteza na njia ya Allah(s.w):



“Akasema (Ibilis) Naapa kwa haki ya utukufu wako, bila shaka nitawapoteza wote (hao watoto wa huyu adui yangu – Adam)” (38:82)




“Akasema: “Kwa kuwa umenihukumia upotofu (upotevu) basi nitawakalia (waja wako). Katika njia yako iliyonyooka (ili niwapoteze) kisha nitawafikia kwa mbele yao na nyuma yao na kuumeni kwao na kushotoni kwao, wengi katika wao hutawakuta ni wenye kushukuru.(7:16-17)



Akasema (Mwenyezi Mungu). Toka humo, hali ya kuwa ni mwenye kudharauliwa na mwenye kufukuzwa. Atakayekufuata miongoni mwao (nitamtia motoni) niijaze Jahannamu kwa nyinyi nyote.”(7:18).

Iblis mwenyewe alikiri kuwa hataweza kuwapoteza wale waja wema waliomshika sawa sawa Mola wao kama tunavyojifunza katika Qur’an:



“Akasema Mola wangu! kwa sababu umenihukumu kupotea, basi nitawapambia(upotofu) katika ardhi na nitawapoteza wote. Isipokuwa wale waja wako waliosafika kweli kweli. Mwenyezi Mungu akasema: Hii njia yao ya kuja kwangu imenyooka wanaweza kunijia wakati watakao. Hakika waja wangu wewe hutakuwa na mamlaka juu yao isipokuwa wale wenyue kukufuata kwa khiari zao katika hao wapotofu.(15:39-42).



                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1260


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Imam Muslim na Sahihul Mslim
Soma Zaidi...

Historia ya Al-Khidhri
Jina Al-Khidhri halikutajwa mahali popote katika Qur’an. Soma Zaidi...

Taasisi za kisiasa za msingi alizotumia mtume (s.a.w) katika kuanzisha dola ya kiislamu madinah
Dola ya kiislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Darsa za Sira historia ya Mtume (s.a.w) Jaribio la 05
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII NUHU
Soma Zaidi...

Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)
Tukirejea Qur’an (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a. Soma Zaidi...

Upinzani Dhidi ya Ujumbe wa Mtume(s.a.w)
Mtume(s. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII SHUAIB
Soma Zaidi...

Kuandaliwa Mtume(s.a.w) maandalizi ya kimafunzo na maandalizi ya ki ilham
Mitume huzaliwa Mitume. Soma Zaidi...

Vipengele vya Mikataba ya ‘Aqabah na faida zake katika kuimarisha uislamu Maka na Madina
Katika Hija iliyofuatia katika mwaka wa 621 A. Soma Zaidi...

Chanzo cha vita vya Ngamia Vita Kati ya Bibi Aisha na Khalifa Ali
Soma Zaidi...

Mtume(s.a.w) Kulingania Uislamu Katika Mji wa Taif
Baada tu ya Mtume(s. Soma Zaidi...