Ibilis ni katika jamii ya majini aliyekuwa pamoja na Malaika wakati amri ya kumsujudia Adam inatolewa.
Ibilis ni katika jamii ya majini aliyekuwa pamoja na Malaika wakati amri ya kumsujudia Adam inatolewa. Iblis alitarajiwa kutii
amri hiyo ya Mola wake pamoja na Malaika, lakini hakufanya hivyo bali alitakabari kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:
“Basi Malaika wakatii (amri ya kusujudu) wote pamoja isipokuwa Ibliis, akajivuna na akawa katika makafiri.” (Allah) akamuuliza: “Ewe Ibilis! Kipi kilichokuzuia kumtii yule niliyemuumba kwa mikono yangu?” Je! Umetakabari au umo miongoni mwa wakubwa (kweli)? (38:73-75)
Akasema (Ibilis katika kujibu): “Mimi ni bora kuliko yeye, kwani mimi umeniumba kwa moto na yeye umemuumba kwa udongo” (38:76)
Ibilis badala ya kuzingatia amri ya Mola wake na kutii, amepeleka fikra zake kwenye asili ya umbile la Adam(a.s) na kuanza kujifananisha naye na kuona kuwa asili ya umbile lake ni bora kuliko ile asili ya umbile la Adam(a.s). Hatakama ingelikuwa kweli kuwa moto ni bora kuliko udongo, Iblis asingelipaswa kukataa kumsujudia Adam(a.s) kwa sababu si Adamu aliyetaka asujudiwe, bali aliyetoa amri ya kumsujudia Adam ni Allah(s.w) ambaye ni Muumba wa Adam na Ibilis.
Baada ya Ibilis kuvunja amri ya Mola wake kwa takaburi kiasi hicho, alilaaniwa na kubaidishwa (kufukuzwa) na rehema za Mola wake:
(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo kwani umetengwa na rehema. Na hakika laana yangu itakuwa juu yako mpaka siku ya malipo.”(38:77-78)
Badala ya Ibilis kukiri kosa lake na kumuelekea Mola wake kwa toba ya kweli, alielekeza lawama zake kwa Adam(a.s) na kuapa mbele ya Allah (s.w) kuwa atalipiza kisasi kwa Adam(a.s) na kizazi chake kwa kukipoteza na njia ya Allah(s.w):
“Akasema (Ibilis) Naapa kwa haki ya utukufu wako, bila shaka nitawapoteza wote (hao watoto wa huyu adui yangu – Adam)” (38:82)
“Akasema: “Kwa kuwa umenihukumia upotofu (upotevu) basi nitawakalia (waja wako). Katika njia yako iliyonyooka (ili niwapoteze) kisha nitawafikia kwa mbele yao na nyuma yao na kuumeni kwao na kushotoni kwao, wengi katika wao hutawakuta ni wenye kushukuru.(7:16-17)
Akasema (Mwenyezi Mungu). Toka humo, hali ya kuwa ni mwenye kudharauliwa na mwenye kufukuzwa. Atakayekufuata miongoni mwao (nitamtia motoni) niijaze Jahannamu kwa nyinyi nyote.”(7:18).
Iblis mwenyewe alikiri kuwa hataweza kuwapoteza wale waja wema waliomshika sawa sawa Mola wao kama tunavyojifunza katika Qur’an:
“Akasema Mola wangu! kwa sababu umenihukumu kupotea, basi nitawapambia(upotofu) katika ardhi na nitawapoteza wote. Isipokuwa wale waja wako waliosafika kweli kweli. Mwenyezi Mungu akasema: Hii njia yao ya kuja kwangu imenyooka wanaweza kunijia wakati watakao. Hakika waja wangu wewe hutakuwa na mamlaka juu yao isipokuwa wale wenyue kukufuata kwa khiari zao katika hao wapotofu.(15:39-42).
Umeionaje Makala hii.. ?
Mayahud Mwanzoni Mayahud walipoona kuwa Waislamu wanafunga siku ya Ashura pamoja nao na wanaelekea Qibla cha Baitul- Muqaddas pamoja nao hawakuonyesha chuki ya dhahiri dhidi ya Mtume(s.
Soma Zaidi...Huko nyuma wapita njia walikisogelea kisima kwa lengo la kuteka maji.
Soma Zaidi...Mawaziri waliokuwa washauri wakuu wa Firauni wakataka wakusanywe magwiji waliobobea katika uchawi nchi nzima, kisha wapambanishwe na Nabii Musa(as).
Soma Zaidi...LAKINI UMRI WANGU MKUBWABaada ya kuwaza na kufikiri muda mrefu, bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) akafikia uamuzi wa kutaka kuolewa na Muhammad (Swalla Laahu alayhi wa sallam).
Soma Zaidi...Tukirejea Qur’an (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a.
Soma Zaidi...