image

Kibri cha Ibilis na Uadui Wake Dhidi ya Binadamu

Ibilis ni katika jamii ya majini aliyekuwa pamoja na Malaika wakati amri ya kumsujudia Adam inatolewa.

Kibri cha Ibilis na Uadui Wake Dhidi ya Binadamu

Kibri cha Ibilis na Uadui Wake Dhidi ya Binadamu


Ibilis ni katika jamii ya majini aliyekuwa pamoja na Malaika wakati amri ya kumsujudia Adam inatolewa. Iblis alitarajiwa kutii

amri hiyo ya Mola wake pamoja na Malaika, lakini hakufanya hivyo bali alitakabari kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:




“Basi Malaika wakatii (amri ya kusujudu) wote pamoja isipokuwa Ibliis, akajivuna na akawa katika makafiri.” (Allah) akamuuliza: “Ewe Ibilis! Kipi kilichokuzuia kumtii yule niliyemuumba kwa mikono yangu?” Je! Umetakabari au umo miongoni mwa wakubwa (kweli)? (38:73-75)




Akasema (Ibilis katika kujibu): “Mimi ni bora kuliko yeye, kwani mimi umeniumba kwa moto na yeye umemuumba kwa udongo” (38:76)

Ibilis badala ya kuzingatia amri ya Mola wake na kutii, amepeleka fikra zake kwenye asili ya umbile la Adam(a.s) na kuanza kujifananisha naye na kuona kuwa asili ya umbile lake ni bora kuliko ile asili ya umbile la Adam(a.s). Hatakama ingelikuwa kweli kuwa moto ni bora kuliko udongo, Iblis asingelipaswa kukataa kumsujudia Adam(a.s) kwa sababu si Adamu aliyetaka asujudiwe, bali aliyetoa amri ya kumsujudia Adam ni Allah(s.w) ambaye ni Muumba wa Adam na Ibilis.

Baada ya Ibilis kuvunja amri ya Mola wake kwa takaburi kiasi hicho, alilaaniwa na kubaidishwa (kufukuzwa) na rehema za Mola wake:



(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo kwani umetengwa na rehema. Na hakika laana yangu itakuwa juu yako mpaka siku ya malipo.”(38:77-78)

Badala ya Ibilis kukiri kosa lake na kumuelekea Mola wake kwa toba ya kweli, alielekeza lawama zake kwa Adam(a.s) na kuapa mbele ya Allah (s.w) kuwa atalipiza kisasi kwa Adam(a.s) na kizazi chake kwa kukipoteza na njia ya Allah(s.w):



“Akasema (Ibilis) Naapa kwa haki ya utukufu wako, bila shaka nitawapoteza wote (hao watoto wa huyu adui yangu – Adam)” (38:82)




“Akasema: “Kwa kuwa umenihukumia upotofu (upotevu) basi nitawakalia (waja wako). Katika njia yako iliyonyooka (ili niwapoteze) kisha nitawafikia kwa mbele yao na nyuma yao na kuumeni kwao na kushotoni kwao, wengi katika wao hutawakuta ni wenye kushukuru.(7:16-17)



Akasema (Mwenyezi Mungu). Toka humo, hali ya kuwa ni mwenye kudharauliwa na mwenye kufukuzwa. Atakayekufuata miongoni mwao (nitamtia motoni) niijaze Jahannamu kwa nyinyi nyote.”(7:18).

Iblis mwenyewe alikiri kuwa hataweza kuwapoteza wale waja wema waliomshika sawa sawa Mola wao kama tunavyojifunza katika Qur’an:



“Akasema Mola wangu! kwa sababu umenihukumu kupotea, basi nitawapambia(upotofu) katika ardhi na nitawapoteza wote. Isipokuwa wale waja wako waliosafika kweli kweli. Mwenyezi Mungu akasema: Hii njia yao ya kuja kwangu imenyooka wanaweza kunijia wakati watakao. Hakika waja wangu wewe hutakuwa na mamlaka juu yao isipokuwa wale wenyue kukufuata kwa khiari zao katika hao wapotofu.(15:39-42).



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 622


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

HISTORIANA MAISHA YA MTUME ISA(A.S)
Nabii Isa(a. Soma Zaidi...

Yusufu Aokotwa na Kuuzwa nchini Misri
Huko nyuma wapita njia walikisogelea kisima kwa lengo la kuteka maji. Soma Zaidi...

Mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah.
Mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII HUD
Soma Zaidi...

Hali za bara arab zama za jahiliya karne ya 6 kabla ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad
7. Soma Zaidi...

Kuendeshwa kwa dola ya kiislamu, Uchumi, ulinzi, haki na sheria, siasa na vikao vya shura
Uendeshaji wa Dola ya Kiislamu Madinah. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Musa(a.s) na Harun(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Musa na Harun(a. Soma Zaidi...

HARAKATI ZA DINI WAKATI WA MATABIINA NA TABII TABIINA
Soma Zaidi...

Mtume Muhammad alelewa na mama yake mzazi akiwa na umri wa miaka 4.
Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 8. Hapa utajifunza malezi ya Mtume kutokakwa Halimavkuja kwa mama yake. Soma Zaidi...

Kukomeshwa kwa Riddah na Chokochoko Nyingine katika dola ya kiislamu
Soma Zaidi...

Imam Muhammad Idris al-Shafii
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ISA
Soma Zaidi...