HISTORIA YA NABII YUSUFU(A.S.): Ndoto ya nabii Yusufu

HISTORIA YA NABII YUSUFU(A.S.): Ndoto ya nabii Yusufu

Mtume Yusufu(a.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

HISTORIA YA NABII YUSUFU(A.S.): Ndoto ya nabii Yusufu

HISTORIA YA NABII YUSUFU(A.S.)


Mtume Yusufu(a.s) alikuwa mtoto wa Mtume Ya’aquub bin Is- haq bin Ibrahiim. Kwa hiyo Yusufu(a.s) ni kijukuu cha (mjukuu wa mtoto wa) Mtume Ibrahiim(a.s) na mjukuu wa Mtume Is-haqa(a.s.).

Mtume Ya’aquub(a.s) alikuwa na watoto 12. Nabii Yusufu(a.s) alichangia mama na mmoja wa hao. Wengine 10 walikuwa na mama zao.


Ndoto ya Nabii Yusufu(a.s) Maisha ya Nabii Yusufu(a.s) yanaanza kusimuliwa ndani ya Qur’an pale alipomwambia babake kuwa:



Yusufu alipomwambia baba yake “Ewe babaangu! hakika nimeona katika ndoto nyota kumi na moja na jua na mwezi. Nimeviona hivi vikinisujudia(12:4)



Mtume Ya‘aquub, kwa ilimu aliyopewa na Mola wake alifahamu tafsiri ya ndoto ile kwamba inabashiri kuwa Yusufu atakuja kuwa mtu mwenye hadhi kubwa na Mtume. Akamtahadharisha kuwa:



Akasema (baba yake): “Ewe mwanangu! Usiwasimulie ndoto yako (hii) nduguzo wasije wakakufanyia vitimbi (kwa ajili ya husuda). Hakika Shetani kwa mwanadamu ni adui aliye dhahiri.(12:5)




Namna hivi Mola wako atakuchagua na kukufundisha hakika ya mambo. Na atatimiza neema zake juu yako na juu ya kizazi cha Ya‘aquub, kama alivyoitimiza zamani juu ya baba zako Ibrahim na Is-haqa. Bila shaka Mola wako ni Mjuzi na Mwenye hikima: (12:6).



                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 3714

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Ni nani alikuwa sahaba wa mwisho kufariki
Ni nani alikuwa sahaba wa mwisho kufariki

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu nani alikuwa wamwisho kufariki katika masahaba wa Mtume kwa mujibu wa historia

Soma Zaidi...
NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA
NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA

MKATABA WA AL-FUDHULBaada ya vita hivi viongozi wa pande mbili hizi waliamuwa wakae chini na wakubaliane kuweka kanun i na utaratibu utakaozuia kutotokea uonevu kama huuu tena.

Soma Zaidi...
NINI MAANA YA SWALA (SALA AU KUSWALI), KILUGHA NA KISHERIA KATIKA UISLAMU
NINI MAANA YA SWALA (SALA AU KUSWALI), KILUGHA NA KISHERIA KATIKA UISLAMU

Maana ya Swala Maana ya Swala kilugha(a) Kilugha Katika lugha ya Kiarabu neno Swalaat lina maana ya ombi au dua.

Soma Zaidi...
Maryam Apewa Habari ya Kumzaa Isa(a.s)
Maryam Apewa Habari ya Kumzaa Isa(a.s)

Baada ya maandalizi hayo ya kimalezi pamoja na hifadhi ya Allah(s.

Soma Zaidi...