Kuangamizwa Waovu na Kuokolewa Waumini
Baada ya kuonywa wasionyeke, Allah(s.
Kuangamizwa Waovu na Kuokolewa Waumini
Baada ya kuonywa wasionyeke, Allah(s.w) aliwaangamiza kama walivyoangamizwa akina Ad, Thamud, n.k.
Basi mtetemeko wa ardhi uliwatoa roho zao, wakawa wasiojimudu, (wamekufa) humo mjini mwao. Wale waliomkadhibisha Shu’ayb wakawa kama kwamba hawakuwako (mahala hapo). Wale waliomkadhibisha Shu’ayb ndio waliokuwa wenye khasara. (7:91-92)
Na ilipokuja amri yetu, tulimuokoa Shu’ayb na wale walioamini pamoja naye kwa rehema yetu. Na wale waliodhulumu ukelele (wa adhabu) ulinyakuwa roho zao. Wakawa majumbani mwao wametulia tu (wamekufa).(11:94)
Kama kwamba hawakuwamo humo. Sikilizeni. Wameangamia (watu wa) Madiana kama walivyoangamia (kina) Thamudu. (11:95)
Kwa mujibu wa aya hizi, watu wa Madian waliangamizwa kwa ukelele ukifuatiwa na tetemeko la ardhi. Tukikumbuka kuwa:
Na majeshi ya mbingu na ardhi ni ya Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu; Mwenye hikima. (48:7)
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 web hosting 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Nafasi ya Elimu katika uislamu
Elimu imepewa kipaumbele kikubwa kwenye uislamu. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nafasi ya Elimu katika uislamu.
Soma Zaidi...Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat al-Baqarah
Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini.
Soma Zaidi...Maana ya kumuamini mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Maswali juu ya dini anayostahiki kufuata mwanadamu
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...