picha

Kwanini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini?

Mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Kwa nini mwanaadamu hawezi kuishi bila ya dini?
Mwanaadamu yeyote hawezi kuishi bila ya dini hata kama atadai kuwa hana dini kwa sababu zifuatazo;
Maana halisi ya dini.
Dini ni utaratibu wa maisha anaofuata mwanaadamu katika kuendesha maisha yake ya kila siku kibinafsi na kijamii.

Umbile la mwanaadamu ni la kidini.
Umbile la mwanaadamu limefungamana na kanuni na sheria za maumbile yote yanayomzunguka.
Rejea Quran (30:30), (3:83).

Vipawa alivyotunukiwa mwanaadamu.
Tofauti na wanyama na viumbe wengine, mwanaadamu ametunukiwa vipawa vya ziada vifuatavyo;
Akili na Ufahamu wa hali ya juu.
Vinamsaidia kufikiri na kutafakari mambo yanayomhusu yeye mwenyewe na mazingira yanayomzunguka.

Utambuzi binafsi (self-consciousness).
Humuwezesha kuhusianisha yeye na mazingira (viumbe) yanayomzunguka.

Uwezo wa kujielimisha na kuelimika.
Elimu ni nyenzo pekee inayomuwezesha mwanaadamu kuyamudu mazingira kwa ufanisi.

Uhuru wa kufanya atakalo.
Mwanaadamu amepewa vipaji, elimu na ujuzi, ilivimuwezeshe kubainisha njia sahihi ya kufuata katika maisha yake ya kila siku.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Views 6317

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 web hosting     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Lengo la kushushwa vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nguzo za imani katika uislamu na mafunzo yake

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu nuzo 6 za imani ya uislamu na pia utajifunz akuhusu mafunzo yanayoweza kupatikana kwenye Nguzo hizi.

Soma Zaidi...
Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab

Bila shaka wanaume wenye kufuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanawake wanaozifuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanaume wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanawake wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanaume wanaotii, na wanawake wanaotii, na wanaume wa

Soma Zaidi...
Elimu Yenye Manufaa

Kwenye kipengele hiki tutajifunza elimu yenye manufaa kwenye jamii na pia tutajifunza sifa za elimu yenye manufaa.

Soma Zaidi...
Maswali juu ya mtazamo wa uislamu kuhusu dini

Mtazamo wa uislamu kuhusu dini (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...