Mpango wa kumuuwa Khalifa ally na Gavana Muawiya

Mpango wa kumuuwa Khalifa ally na Gavana Muawiya

Kutekwa kwa Makka, Madina na Yemen



Katika mwaka wa 40 A.H. Amir Muawiya alimtuma Busr Ibn Abi Artat na watu elfu tatu kwenda Hijazi ambako aliiteka Madina, Makka na mji wa Sanaa, Yemen na kuwataka wamtii Muawiyah. Huko Yemen aliua watoto wadogo wawili wa Gavana wa jimbo hilo Ubaidullah ambaye alikimbilia Kufa. Vile vile aliwaua wafuasi wengi wa Ali. Jariah Ibn Qudamah akiwa na askari elfu mbili alitumwa kurudisha maeneo yaliyotekwa.


Alifanikiwa kuirejesha Sanaa mikononi mwa Khalifa kwani wakati huu Busr alikwisharudi Syria. Lakini alipofika Makka alipata taarifa ya kuuwawa kwa Ali na huu ukawa ndio mwisho wa Ali. Kuuwawa kwa Ali Baada ya vita vya Nahrwan, Khawarij waliendesha mambo yao chini chini. Inadaiwa waliendelea kuisakama Serikali.


Hawakumpenda Ali wala Muawiyah kwa sababu wao ndiyo chanzo cha kugawanyika kwa Waislamu, katika kundi la Muawiyah na kundi la Ali. Amr bin al As naye walimuona ana makosa kwa vile ndiye mshauri na afisa mipango wa Muawiya. Hivyo walipanga kuwaua wote watatu alfajiri ya mwezi 17 Ramadhan 40 A.H. wakati wa swala ya Alfajiri. Ilipangwa Ali auliwe na Abdur-Rahman Muljam. Muawiya auliwe na Bark Ibn Abdullah na Amr bin al As auliwe na Amr ibn Bark.


Wauwaji hawa walitia sumu kali katika majambia yao na wote wakafanya kazi yao kama walivyopanga Misri, Syria na Kufa. Lakini matokeo hayakuwa mia kwa mia. Ali alijeruhiwa vibaya na jeraha lilisababisha kifo chake kilichotokea jioni ya mwezi 20 Ramadhan 40 A.H. Muljam alikamatwa na kuhojiwa. Kabla hajafa Khalifa Ali aliwaita watoto wake na kuwausia kumcha Mungu. Lakini alipoulizwa kama Hassan atawazwe Ukhalifa alisema, โ€œNawaachia Waislamu waamueโ€. Khalifa Ali alitawala kwa miaka mine na miezi tisa. Alikufa akiwa na miaka 63.



Baada ya Khalifa Ali kuuliwa, mtoto wake, Hassan, alichaguliwa kuchukua nafasi ya Ukhalifa lakini Muawiyah aliasi na kuandaa jeshi dhidi yake. Baada ya mapigano kidogo, Hassan alizidiwa nguvu na akaona amwachie Muawiyah Ukhaifa kwa makubaliano kuwa baada yake uongozi uchukuliwe na ndugu yake, Hussein bin Ali. Kinyume na makubaliano hayo, ambayo pia hayakuwa ya Kiislamu, Muawiyah kabla hajafa, alimteua mtoto wake, Yazid bin Muawiyah kushika uongozi wa Dola baada yake.




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 461

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰3 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰4 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Ibrahiim(a.s) Aomba Kupata Kizazi Chema

Nabii Ibrahiim na mkewe Sarah walikaa mpaka wakawa wazee bila ya kupata mtoto.

Soma Zaidi...
Malezi ya mtume

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mbinu walizotumia makafiri wa kiqureish katika kuupinga uislamu makkah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kuhifadhiwa kwa Quran

Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mafunzo yatokanayo na upinzani wa maquraish dhidi ya uislamu

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...