Menu



Mji wa Makkah na kabila la kiqureish

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

-    Mji wa Makkah ni mji mkongwe wa kihistoria ulioanzishwa na Nabii Ibrahiim miaka mingi iliyopita.

 

-    Nabii Ibrahim (a.s) na mwanae Nabii Ismail (a.s) ndio walioinua kuta za nyumba tukufu ya Ka’abah kwa amri ya Allah (s.w).

    Rejea Qur’an (2:127).

 

-    Ka’abah ni nyumba ya mwanzo na pekee ulimwenguni iliyowekwa kwa ya kuhiji wanaadamu wote ulimwenguni.

    Rejea Qur’an (22:27), (3:96) na (22:29).


 

-    Kutokana na jangwa na ukame wa mji huu, Allah (s.w) alijaalia chem.-chem ya maji ya zamzam kutokana dua ya Nabii Ibrahim (a.s).

    Rejea Qur’an (14:37).

 

-    Mji huu ulipata utukufu kutokana na uwepo wa nyumba tukufu ya Ka’aba ambapo kabila la Qureish ndio walikuwa walinzi wa nyumba hiyo.

    Rejea Qur’an (106:1-4).

 

-    Ni mji alikozaliwa Mtume Muhammad (s.a.w) mwaka 570 A.D katika kabila la Kiqureish mwaka wa ndovu.

    Rejea Qur’an (105:1-5).

 

-    Kabila la Kiqureish liliheshimika kuliko makabila mengine kwa huduma walizokuwa wakitoa kwa watu wanaohiji, misafara ya biashara na kule kuitumikia nyumba hiyo.

 

-    Kabila la Qureish ni miongoni mwa makabila ya waarabu yaliyojishughulisha sana na biashara mbali mbali ndani na nje ya Makkah kwa muda mrefu.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea

Ndio     Hapana     Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Views 1283

Share On:

Facebook WhatsApp

Post zinazofanana:

Nani alikuwa ni Sahaba wa kwanza kufariki akiwa Shahidi

Sahaba wa kwanz akufariki akiwa shahidi, alifariki kwa sababu ya mateso aliyoyapata kutoka kwa Makafiri wa ki Quraysh

Soma Zaidi...
Kuzaliwa kwa Mtume S.A.W

Sura na historia ya Mtume Muhammad s.sa. w, sehemu ya 5. Hapa utajifunza kuhusu kuzaliwa kwa Mtume.

Soma Zaidi...
Vita vya uhudi

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
tarekh11

KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara.

Soma Zaidi...