image

Vita vya Uhud na sababu ya kutokea kwake, Mafunzo ya Vita Vya Uhud

Vita vya Uhudi.

Vita vya Uhud na sababu ya kutokea kwake, Mafunzo ya Vita Vya Uhud

Vita vya Uhud na sababu ya kutokea kwake.

Vita vya Uhudi.
- Sababu ya kutokea vita vya Uhudi ni Maquraish kutaka kulipiza kisasi dhidi ya waislamu baada ya kushindwa katika vita vya Badri.

- Maquraish waliandaa msafara wa biashara wenye thamani ya Dirham 300,000 kuelekea Iraq kama maandalizi ya kulipiza kisasi vita vya Badri.

- Kikosi cha waislamu kikiongozwa na Zaid bin Harith (r.a) kiliteka msafara huo na kuchukua mali yenye thamani ya Dirham 100,000 na mateka 2.

- Vita vilipiganwa siku ya Jumamosi, mwezi 15 Shawwal, mwaka wa 3 A.H (625 A.D) katika milima ya Uhudi nje ya mji wa Madinah.

- Waislamu walikuwa 700 (baada ya wanafiki 300 kurudi nyuma wakiongozwa na Abdullah bin Ubayyi) na Maquraish wakiwa askari 3,000 waliojizatiti kivita, (700 wamevaa mavazi ya chuma), farasi 200 na ngamia 3,000.

- Kwa waislamu kiongozi alikuwa Mtume (s.a.w) na kwa Maquraish viliongozwa na Hindu bint Utbah mkewe Abu Sufyan.

- Mtume (s.a.w) aliteuwa kikosi cha watu 50 wakiongozwa na Abdullah bin Jubeir kukaa juu ya mlima ili kulinda kikosi cha maadui kikiongozwa na Khalid bin Walid.

- Vita vilipoanza waislam walipata ushindi lakini baadae kugeuka kipigo baada ya waislamu 43 kuondoka mlimani na kupelekea Mtume kuvunjwa meno 2.

- Waislamu 70 waliuuawa akiwemo shujaa Hamza bin Abdi Muttalib (r.a) aliyeuliwa na mtumwa Wahshi bin Harbi aliyeandaliwa na Hindu bint Utbah.

Mafunzo yatokanayo na Vita vya Uhudi.
1.Lengo la maadui wa Uislamu na waislamu kupigana ni kuwaangamiza wao, kuharibu miji yao na mali zao pia. Hivyo ni wajibu waislamu kuwa na tahadhari muda wote kupambana na maadui wao.

2.Kushauriana katika kupanga mambo ni jambo la busara sana, kama alivyoshauriana Mtume (s.a.w) juu ya sehemu ya kupiganwa vita vya Uhudi.
Rejea Qur’an (3:159) na (3:166-167).

3.Tunajifunza pia ni wajibu waislamu kutumia mbinu, ujuzi, uzoefu, na jitihada za kivita pamoja na kuwa wanapata msaada wa Mwenyezi Mungu (s.w).
Rejea Qur’an (8:60).

4.Msaada wa Mwenyezi Mungu (s.w) kwa waislamu unapatikana pale tu waislamu watakapotii amri zake na wakapigania dini vilivyo.
Rejea Qur’an (3:151-152).

5.Kuvunja na kutotii amri ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake hupelekea kutofikia mafanikio hata kama watajizatiti na kufanya jitihada ipasavyo.
Rejea Qur’an (3:152), (3:165) na (33:36).

6.Tunajifunza pia, makosa ya watu wachache yasipuuzwe na kufumbiwa macho bali yarekebishwe kwani athari yake itasibu jamii nzima.
Rejea Qur’an (8:25).

7.Mwenyezi Mungu (s.w) anatukumbusha kuwa pepo haipatikani kwa kutamani, lele mama na ushabiki bali, kufanya jitihada ya kweli.
Rejea Qur’an (3:142-150), (3:156-160) na (3:169-171).

8.Msamaha na nusura ya Mwenyezi Mungu (s.w) upo karibu kwa waislamu pindi watakapotubia na kurejea kwake na kupambana na maadui ipasavyo.
Rejea Qur’an (3:152-154), (3:166-167) na (3:139-141).

9.Ushindi wa waislamu katika vita unatoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w) na sio kutokana na ubora wa silaha na wingi wa askari.
Rejea Qur’an (3:123-124), (8:42-45).

10.Choko choko na mbinu za maadui dhidi ya Uislamu na waislamu ni zenye kuendelea na hazitaisha kamwe hadi siku ya Qiyama.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 641


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

HISTORIA NA MAISHA YA MTUME IDRISA (A.S)
Mtume aliyemfuatia Nabii Adam(a. Soma Zaidi...

Mkataba wa 'Aqabah na vipiengele vyake na mafunzo tunayoyapata katika mkataba wa aqaba
Mtume (s. Soma Zaidi...

Sababu ya uislamu kuwa ndiyo dini sahihi pekee
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HISTORIA YA MAISHA YA UTOTONI YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W)
MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S. Soma Zaidi...

Hali za bara arab zama za jahiliya karne ya 6 kabla ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad
7. Soma Zaidi...

Msimamo wa Nabii Hud(a.s) Dhidi ya Makafiri wa Kaumu Yake
Pamoja na kwamba alipingwa na nguvu za Dola ya makafiri wa kaumu yake, Mtume Hud(a. Soma Zaidi...

Nabii Yunus(a.s) Amuomba Allah(s.w) Msamaha
Ndani ya tumbo la samaki, Nabii Yunus(a. Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na kuanzishwa kwa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

NUHU(A.S) NA WATU WAKE NA UOVU WALIOKUWA WAKIUFANYA WATU WAKE
Mtume aliyemfuatia Nabii Idrisa(a. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Yusufu(a.s)
“Kwa yakini katika (kisa cha) Yusufu na ndugu zake yako mazingatio mengi kwa wanaouliza (mambo wapate kujua)”. Soma Zaidi...

HISTORIA YA KUJENGWA UPYA KWA AL-KA'BAH (NYUMBA TUKUFU YA ALLAH)
KUJENGWA UPYA KWA AL-KA’ABAHItambulike kuwa Al-ka’abah ndio mjengo wa kwanza kujengwa duniani. Soma Zaidi...

Mtume kumuoa bi khadija
Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 15. Hapa utajifunza kuhusu chimbuko la ndoa ya Mtume s.a.w na bi Khadija. Soma Zaidi...